BARUA YA WAZI KWENDA KWA DKT MWIGULU LAMECK NCHEMBA
Anaandika Hassan Ruangwa
Wasalaam Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, Natumai ubukheri wa afya ya akili na Mwili, Dhumuni la Barua yangu kwako ni kusisitiza kuwa lazima uendelee kuonesha ukomavu huohuo bila kupepesa maneno, Kodi ya Serikali lazima ilipwe bila kujalisha nani ataumia, natambua Kwasasa wewe unakutana na Vita Kali ila Kwa msaada wa Rais Samia Suluhu Hassan na Maombi ya watanzania unaendelea kusonga mbele.
Vita yako imepamba Sasa, usiogope Wala kutishika, hao waliozoea kuwadanganya watanzania kuwa wao ni wazalendo kumbe ni wakwepa Kodi wakubwa Sasa wameanza kuumbuka, umma mzima wa Wananchi umetambua dhulma zao. Naambiwa kuwa wameanza kutafutia kashfa za ku-ungaunga ilmradi tu wakuvunje Moyo, wakutishe lakini nakusihi Songa mbele, msaidie Rais Samia Suluhu Hassan lisaidie Taifa lako maana uzalendo wako tunaujua, usafi wako tunaujua, wewe ni mtu muadilifu usiyekuwa na hata chembe Moja ya udokozi. Wala usiangaishwe na hao wapika majungu waliozoea kuwa-brainwash watanzania, ila kwasasa wamekwama maana tumestuka na kuwatambua nyuso zao halisi. Kodi lazima walipe bila kujali vyeo vyao, bila kujali uwezo wao wa kupakazia watu uongo, bila kujali uwezo wao wa kujivika ngozi ya kutia huruma na hakuna nafasi ya mtu kutumia jina lake kuliingizia Taifa hasara tena.
Kazi zako twaziona, misimamo yako twaiona. Mimi Leo nimeamua kukuandikia hii barua kukupa shime, kukupa Moyo na Pongezi, Lazima usonge mbele, Mishale sio migeni kwako, umekomaa sasa na ukumbuke vita hii umeianza toka ukiwa Naibu Waziri wa Fedha awamu ya Nne, uliwatikisa wakwepa Kodi wakubwa Kwa wadogo hivyo lazima uendelee vivyo hivyo maana hapa unatetea maslahi ya vizazi na vizazi.
Kongole Kwako Rais Samia Suluhu Hassan, umekuwa Mwanasiasa mkongwe tena ulieiva kisawasawa, unatambua Kila mbinu za hovyo za wanasiasa waotengeneza hujuma Kwa wenzao, Umemlinda kijana wako huyu ambae wahafidhina walipanga wamle nyama Kipindi Cha Tozo, wamepanga Sasa wamchafue na kibaya zaidi wanaogopa Future yake, wanahofia uhai wa dhulma zao uko mbeleni, Ahsante Mama hakika ulistahili nafasi hii tangu zamani.
Ndugu watanzania wazalendo wenzangu tunaopigana usiku na mchana Kuhakikisha future ya wajukuu yetu haiharibiwi na walafi wachache waliojivika nyuso za uzalendo uchwara, tuendelee kumwombea Rais wetu kipenzi Jemedari Samia Suluhu Hassan na Kijana Wake Dkt Mwigulu Lameck Nchemba ambao Kwasasa wanasagiwa meno na makundi ya waasi, wezi na wakwepa Kodi wakubwa, tuwalinde Kwa namna yoyote Ile Ili Kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele kimaendeleo na kiuchumi.
Anaandika Hassan Ruangwa
Wasalaam Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, Natumai ubukheri wa afya ya akili na Mwili, Dhumuni la Barua yangu kwako ni kusisitiza kuwa lazima uendelee kuonesha ukomavu huohuo bila kupepesa maneno, Kodi ya Serikali lazima ilipwe bila kujalisha nani ataumia, natambua Kwasasa wewe unakutana na Vita Kali ila Kwa msaada wa Rais Samia Suluhu Hassan na Maombi ya watanzania unaendelea kusonga mbele.
Vita yako imepamba Sasa, usiogope Wala kutishika, hao waliozoea kuwadanganya watanzania kuwa wao ni wazalendo kumbe ni wakwepa Kodi wakubwa Sasa wameanza kuumbuka, umma mzima wa Wananchi umetambua dhulma zao. Naambiwa kuwa wameanza kutafutia kashfa za ku-ungaunga ilmradi tu wakuvunje Moyo, wakutishe lakini nakusihi Songa mbele, msaidie Rais Samia Suluhu Hassan lisaidie Taifa lako maana uzalendo wako tunaujua, usafi wako tunaujua, wewe ni mtu muadilifu usiyekuwa na hata chembe Moja ya udokozi. Wala usiangaishwe na hao wapika majungu waliozoea kuwa-brainwash watanzania, ila kwasasa wamekwama maana tumestuka na kuwatambua nyuso zao halisi. Kodi lazima walipe bila kujali vyeo vyao, bila kujali uwezo wao wa kupakazia watu uongo, bila kujali uwezo wao wa kujivika ngozi ya kutia huruma na hakuna nafasi ya mtu kutumia jina lake kuliingizia Taifa hasara tena.
Kazi zako twaziona, misimamo yako twaiona. Mimi Leo nimeamua kukuandikia hii barua kukupa shime, kukupa Moyo na Pongezi, Lazima usonge mbele, Mishale sio migeni kwako, umekomaa sasa na ukumbuke vita hii umeianza toka ukiwa Naibu Waziri wa Fedha awamu ya Nne, uliwatikisa wakwepa Kodi wakubwa Kwa wadogo hivyo lazima uendelee vivyo hivyo maana hapa unatetea maslahi ya vizazi na vizazi.
Kongole Kwako Rais Samia Suluhu Hassan, umekuwa Mwanasiasa mkongwe tena ulieiva kisawasawa, unatambua Kila mbinu za hovyo za wanasiasa waotengeneza hujuma Kwa wenzao, Umemlinda kijana wako huyu ambae wahafidhina walipanga wamle nyama Kipindi Cha Tozo, wamepanga Sasa wamchafue na kibaya zaidi wanaogopa Future yake, wanahofia uhai wa dhulma zao uko mbeleni, Ahsante Mama hakika ulistahili nafasi hii tangu zamani.
Ndugu watanzania wazalendo wenzangu tunaopigana usiku na mchana Kuhakikisha future ya wajukuu yetu haiharibiwi na walafi wachache waliojivika nyuso za uzalendo uchwara, tuendelee kumwombea Rais wetu kipenzi Jemedari Samia Suluhu Hassan na Kijana Wake Dkt Mwigulu Lameck Nchemba ambao Kwasasa wanasagiwa meno na makundi ya waasi, wezi na wakwepa Kodi wakubwa, tuwalinde Kwa namna yoyote Ile Ili Kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele kimaendeleo na kiuchumi.