Barua ya Kazi Uhamiaji

Barua ya Kazi Uhamiaji

reginahope

Senior Member
Joined
Mar 26, 2013
Posts
163
Reaction score
30
Wadau napenda kuuliza barua za kazi kwa hawa jamaa wa uhamiaji tunatumia lugha gani sababu tangazo lao naona lipo kwa lugha ya kiswahili.

Je nikiandika kwa lugha ya kiingereza inaweza kuwa na shida.?

Natanguliza shukrani zangu
 
kwa ninavojua mimi lugha ya mawasiliano serikalini ni kiswahili..andika tu kiswahili si unaona hata tangazo ni kiswahili wasije wakakutupia barua yako kule kisa enlish yako ngumu
 
Kwa mfano tangazo la kazi uhamiaji limetangazwa kiswahili kwenye fani zote kuanzia wahitimu wa vyuo na hata form 4. je nisahihi kuandika kwa kiswahili barua ya kuomba kazi?
 
Nadhani, kama wametumia kiswahili, waweza andika kwa kiswahili.
Nifikiriavyo...
 
Kimsingi lugha rasmi zinazotumuika serikalini ni KISWAHILI NA KIINGEREZA hivyo si tatizo ukatumia lugha moja wapo kati ya hizo kikubwa ueleweke maana ukiandika kiswahili usipoeleweka haina maana. Ujumbe wako uwe wazi (Clear msg) ndio jambo la msingi sana
 
Kimsingi lugha rasmi zinazotumuika serikalini ni KISWAHILI NA KIINGEREZA hivyo si tatizo ukatumia lugha moja wapo kati ya hizo kikubwa ueleweke maana ukiandika kiswahili usipoeleweka haina maana. Ujumbe wako uwe wazi (Clear msg) ndio jambo la msingi sana

asanteni kwa mawazo yenu.Mungu awabariki wote
 
Mi nilishawahi kufanya interview na hawa uhamiaji mwaka jana mwezi wa tano tangazo lilikua kiswahili lakini mi barua niliandika kingereza ......na niliitwa kwenye usaili ...coz interview zao wanaendesha kithungu
 
ANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Kamishna Mkuu wa Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji. Nafasi hizo ni Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji.
A.----- MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI (Nafasi 70)
---------
SIFA ZINAZOHITAJIKA
Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa- na Serikali katika fani zifuatazo:
Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa Habari, Ualimu, Usafirishaji, Raslimali Watu, Sayansi ya Kompyuta, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi Majengo na Uhandisi Mitambo.
Awe na umri usiozidi miaka 35

MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
Kusimamia doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini
Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa Hati ya Mashitaka na kuendesha mashitaka
Kutoa na kupokea fomu mbali mbali za maombi ya Hati za Uhamiaji
----Kufanya Ukaguzi wa Mwanzo wa Maombi mbalimbali
Kuagiza ufunguaji wa Majalada ya watumiaji
-Kupokea na kukagua Hati za Safari, Fomu za Kuingia na Kutoka Nchini
Kuidhinisha malipo mbalimbali ya huduma za Uhamiaji kwa wanaostahili
Kutunza kumbukumbu za ruhusa za watu wanaoingia na kutoka nchini
Kukusanya, kusimamia na kutunza takwimu za Uhamiaji na Uraia
Kuandaa majibu ya maombi yote ya huduma za uhamiaji yaliyokubaliwa au kukataliwa


Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Unaomba level ipi? Kama ni Mkaguzi msaidizi wa uhamiaji mwaga ngeli mwanawane.
 
Nyie hilo tangazo mmelisomea wapi , tatizo watu wanali copy kwenye tovuti part yake tuu , tangazo limewekwa kwa lugha mbili , (kiswahili na kiingereza , tembelea ( www.immigration.go.tz/‎ ) utaliona ... saying so u can use either swahili or english as tangazo wamelipost kwa lugha zote mbili... NEWS AND EVENTS TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI Kamishna Mkuu wa Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji. Nafasi hizo ni Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji. A. MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI (Nafasi 70) SIFA ZINAZOHITAJIKA Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika fani zifuatazo: Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa Habari, Ualimu, Usafirishaji, Raslimali Watu, Sayansi ya Kompyuta, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi Majengo na Uhandisi Mitambo. Awe na umri usiozidi miaka 35 MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA Kusimamia doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa Hati ya Mashitaka na kuendesha mashitaka Kutoa na kupokea fomu mbali mbali za maombi ya Hati za Uhamiaji Kufanya Ukaguzi wa Mwanzo wa Maombi mbalimbali Kuagiza ufunguaji wa Majalada ya watumiaji Kupokea na kukagua Hati za Safari, Fomu za Kuingia na Kutoka Nchini Kuidhinisha malipo mbalimbali ya huduma za Uhamiaji kwa wanaostahili Kutunza kumbukumbu za ruhusa za watu wanaoingia na kutoka nchini Kukusanya, kusimamia na kutunza takwimu za Uhamiaji na Uraia Kuandaa majibu ya maombi yote ya huduma za uhamiaji yaliyokubaliwa au kukataliwa B: KOPLO WA UHAMIAJI (Nafasi 100) 1. SIFA ZINAZOHITAJIKA: Awe amehitimu Kidato cha Sita na kufaulu Awe na umri usiozidi miaka 30 C. KONSTEBO WA UHAMIAJI (Nafasi 100) 1. SIFA ZINAZOHITAJIKA: Awe amehitimu Kidato cha Nne na kufaulu Awe na umri usiozidi miaka 25 D: SIFA ZA ZIADA: KOPLO/KONSTEBO WA UHAMIAJI Cheti cha Ufundi Stadi (Full Technical Certificate) kwenye fani ya Umeme na Mitambo Cheti au Stashahada ya Uhaziri (Certificate or Diploma in Secretarial Studies) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali Cheti au Stashahada ya Kutunza Kumbukumbu (Certificate in Records Management) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali Cheti au Stashahada ya Takwimu (Certificate or Diploma in Statatistics ) Kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali. Cheti au Stashahada ya Vyombo vya Majini (Certificate or Diploma in Marine Transportation and Operations) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali Cheti au Stashahada katika fani ya Uchapaji (Printing) Ujuzi na Elimu ya Kompyuta na Uandishi mzuri utazingatiwa Cheti cha Ufundi Makanika,Kozi ya juu ya Udereva na Leseni ya Udereva Daraja C E. MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA Kufungua, kupanga na kutunza majalada ya huduma mbalimbali za Uhamiaji Kuandika Hati mbalimbali za Uhamiaji Kufanya doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini. Kusindikiza watuhumiwa wa kesi za Uhamiaji Mahakamani pamoja na wageni wanaofukuzwa nchini Kufanya ukaguzi kwenye mahoteli, nyumba za kulala wageni na sehemu za biashara. Kuchapa au kuandika kwa kompyuta barua au nyaraka mbalimbali zinazohusu kazi za kila siku za Uhamiaji. Kufanya matengenezo/ukarabati wa mitambo na vitendea kazi vya Uhamiaji Kuandaa na kutunza takwimu za huduma mbalimbali za uhamiaji F. MAOMBI YOTE YAWE NA VIAMBATISHO VIFUATAVYO: Nakala za vyeti vya kuhitimu masomo kwa mujibu wa sifa zilizotajwa Nakala ya Cheti cha Kumaliza Elimu ya Msingi Nakala ya Cheti cha Kuzaliwa Picha mbili (Passport Size) Barua ya Utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa G. UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI Maombi yote yapitie posta na barua za maombi ziandikwe kwa mkono. Maombi ya nafasi ya Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji yatumwe kwa: KATIBU MKUU, WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, S.L.P. 9223, DAR ES SALAAM Maombi ya nafasi ya Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji yatumwe kwa: KAMISHNA MKUU WA UHAMIAJI, S.L.P. 512, DAR ES SALAAM Mwisho wa kutuma maombi kwa nafasi zote ni tarehe 27/02/2014 VACANCY ANNOUNCEMENT The Principal Commissioner of Immigration Services announces vacant Posts in the Immigration Department. Any Tanzanian Citizen with minimum qualifications mentioned hereunder is encouraged to apply: A. ASSISTANT INSPECTOR OF IMMIGRATION SERVICES (70 Posts) Qualifications: Tanzania Citizens aged not above 35 years Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma from any University or Institution recognized by the Tanzania Government in the following disciplines: Law, Economics, Business, Administration, Journalism, Education, Transportation, Human Resource, Computer Science, Information and Communication Technology, Statistics, Printing, Civil Engineering and Mechanical Engineering Duties and Responsibilities: To supervise patrols along the border areas, sea ports, bus stands, highways, railway stations, business centres and other entry points To prepare charge sheets and prosecute in court all immigration related cases To issue and receive various application forms for immigration services To execute preliminary scrutinization of different application forms To authorize opening of customers application files To receive and scrutinize Passports and other travel documents To authorise collection of government revenues for various immigration services To keep records of all persons entering or leaving the country To collect, organize and keep statistics of immigration and citizenship services To notify customers in writing on the status of their applications B. CORPORAL OF IMMIGRATION SERVICES (100 Posts) Qualifications: Tanzania Citizens not above 30 years of age Holder of Advanced Certificate of Secondary Education C. CONSTABLE OF IMMIGRATION SERVICES (100 Posts) Qualifications: Tanzania Citizens not above 25 years of age Holder of Certificate of Secondary Education D. ADDED ADVANTAGES: Certificate or Diploma in Law Computer knowledge and typing Full Technician Certificate (FTC) in Electricity and Mechanical Engineering Certificate or Diploma in Secretarial duties Certificate or Diploma in Records Management Certificate or Diploma in Statistics Certificate or Diploma in Marine Transport and Operations Certificate in Trade Test Grade II, Advanced Drivers Course Grade II and Driving License Class C Certificate or Diploma in Printing Certificate or Diploma in Civil Engineering Certificate or Diploma in Statistics Duties and Responsibilities: To conduct patrols along the border areas, sea ports, bus stands, highways, railway stations, business centres and other entry points To conduct inspections in the hotels, guest houses and other business premises To issue Immigration forms and information on the requirements for the services sought To escort immigration accused aliens/citizens in court To escort deported aliens outside the country To open and keep customers’ files in good order To apprehend suspected immigration offenders To make maintenance and regular service of equipment To collect, organize and keep immigration related statistics NOTE: Selected applicants for the posts must attend a one year Basic Immigration Course prior to employment D. APPLICATION LETTERS MUST BE ACCOMPANIED WITH: Two recent passport size photographs Photocopy of Academic Certificates/Trainings Photocopy of Birth Certificate Letter of Introduction from Village/Ward Executive Officer or Sheha Secondary/Advanced Secondary School Leaving Certificate Primary school leaving Certificate E. MODE OF SUBMISSION All applications must be hand written and have to be submitted through Post Office All applications for the post of Assistant Inspector of Immigration Services should be channeled to: The Permanent Secretary, Ministry of Home Affairs, P.O. Box 9223, DAR ES SALAAM All applications for the post of Corporal and Constable of Immigration Services should be channeled to: The Principal Commissioner of Immigration Services, P.O. Box 512, DAR ES SALAAM Deadline for submission of applications: February 27, 2014.
 
wadau hebu nijuzeni kwawaliosoma hili taangazo kwenye tayoa employment portal wameweka hiki kipengele nanukuu note: "selected applicants for the post must attend one year Basic immigration course prior to employment" wadu hii ni depo nini? natnguliza shukrani.
 
wadau hebu nijuzeni kwawaliosoma hili taangazo kwenye tayoa employment portal wameweka hiki kipengele nanukuu note: "selected applicants for the post must attend one year Basic immigration course prior to employment" wadu hii ni depo nini? natnguliza shukrani.

Ukifaulu unapimwa afya then unaenda depo miezi tisa ndiyo unaanza ajira rasmi.
 
Back
Top Bottom