kadendu
JF-Expert Member
- Mar 30, 2014
- 519
- 337
Nianze kwa kukupa pole na majukumu ya kitaifa pia nikupongeze kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, uwe Mkuu wa Jeshi la Polisi.
Sina shaka na utendaji wako uliotukuka, pichani ni Askari wako Inspekta Emmanuel Govella ambaye alikuwa Mkuu wa Kituo cha Poliso Mtumba, Mji wa Kiserikali ambapo zipo ofisi za Wizara za Serikali.
Askari huyu amepotea katika mazingira ya kutatanisha tangu Juni 26 2021 mpaka leo ni takribani mwaka mmoja na miezi mitatu (3) hakuna taarifa yoyote kutoka Jeshi la Polisi kwenda kwenye familia, nini tatizo? au jeshi lako linajua alipo?
Ni vema basi familia ikafahamishwa kwa barua maalumu, ndugu na jamaa majirani zake hapa Nkuhungu tunahitaji kujua hatima ya huyu jamaa ambae tuliishi nae vizuri sana.
Ndugu IGP, Emma ana mzazi mmoja ambaye ni mama, ni mjane alikuwa anamtegemea mwanaye kama nguzo kusaidia familia ikiwa ni pamoja na kusomesha wadogo zake.
Wakati anapotea wewe haukuwa IGP, nimeona nikuandikie BARUA hii sababu nafahamu utendaji wako na hautalipuuzia suala hili, nikutakie majukumu mema na Mwenyezi Mungu akuongoze uje na majibu ya kupotea kwa Emmanuelly Govella natanguliza shukrani.
Assalamu alaikum!