Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,494
- 113,590
Wanabodi,
Hatimaye huu mtanange wa Acacia kununuliwa na Barrick, hatimaye umefika mwisho leo, kwa Barrick kutoa tangazo la kuinunua Acacia, na Acacia kutoa tango la kukubali kununuliwa na Barrick.
Tangazo la Barrick la Kifo cha Acacia ni Hili
PRESS RELEASES
Recommended Final Offer For Acacia Mining Plc By Barrick Gold Corporation – July 19, 2019
Tangazo la Acacia kukubali kununuliwa na Barrick ni hili
Hii maana yake ni
Hongera Kabudi, Hongera Magufuli, Hongera Watanzania, ila kwenye makinikia, bado kuna lakini!.
Leo tupongezane kwanza, lakini tuzijadili baada ya kusainiwa makubaliano yenyewe!.
Paskali
Hatimaye huu mtanange wa Acacia kununuliwa na Barrick, hatimaye umefika mwisho leo, kwa Barrick kutoa tangazo la kuinunua Acacia, na Acacia kutoa tango la kukubali kununuliwa na Barrick.
Tangazo la Barrick la Kifo cha Acacia ni Hili
PRESS RELEASES
Recommended Final Offer For Acacia Mining Plc By Barrick Gold Corporation – July 19, 2019
Tangazo la Acacia kukubali kununuliwa na Barrick ni hili
Hii maana yake ni
- Sasa mgogoro wa Acacia na serikali yetu, umemalizika rasmi kwa sababu sasa Acacia doesnt exist anymore.
- Migodi yote mitatu iliyokuwa chini ya Acacia, sasa itakuwa chini ya Barrick
- Yale makubaliano ya serikali yetu sasa yatatekelezwa.
- Kwa kuanzia tutalipwa dola milioni 300 zilizokuwa ni kishika uchumba, lakini sasa sio kishika uchumba tena bali ni kifuta machozi cha kusamehe lile deni kubwa la kodi la dola bilioni 190.
- Barrick ataunda kampuni mpya ya ubia na Tanzania kuchukuwa shughuli za Acacia
- Kwenye hiyo kampuni mpya, serikali ya Tanzania itakuwa na shares asilimia 16%.
- Bodi ya hiyo kampuni mpya itakuwa na Watanzania.
- Makao Makuu yatakuwa Tanzania
- Menejiment itakuwa na Watanzania.
- Tutagawana manufaa ya kiuchumi pasu kwa pasu, yaani 50/50.(NB.Manufaa ya kiuchumi ni economic benefits na sio faida profits)
Hongera Kabudi, Hongera Magufuli, Hongera Watanzania, ila kwenye makinikia, bado kuna lakini!.
Leo tupongezane kwanza, lakini tuzijadili baada ya kusainiwa makubaliano yenyewe!.
Paskali