Barrick Gold kuuzwa...

Big up waziri wa madini. Waenda zao, huwezi kuacha kunya eti unaogopa kusikia njaa.
 
Kwani matatizo ya umeme Bongo yameanza leo au jana? Mbona tangu walipoingia nchini tangu mwaka 2000 hawakuona kama ni tatizo hadi miaka 12 baadaye!? Hawa naona wamestukia agizo la kulipa kodi ya 30% lililotolewa na Waziri mpya wa Madini na Nishati Sospeter Muhongo.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ng-companies-to-pay-30-pct-corporate-tax.html

hawana lolote hao, wameshaiba vya kutosha na sasa wanaona hakutakuwa na faida kama enzi zile za kuachwa wafanye wanalotaka.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Waungwana,

Mie sikumbuki kusoma mahali popote au kusikia hawa Barrick kununua machimbo ya Tanzania ya dhahabu. Ninachokumbuka kusoma na kusikia ni kwamba waliingia mkataba na Serikali ya Tanzania (mwenye mali) kuchimba madini hayo na wao kuchukua 97% ya mapato na kulipa mrahaba (Royalties) wa 3% kwa Serikali.

Sasa inakuwaje wanataka kuuza kitu ambacho hawakununua? Je Barrick wana ushahidi wowote kwamba walinunua machimbo yote ambayo waliingia mkataba na Serikali ya Tanzania? Je walimlipa nani na kiasi gani walicholipa? Mbona hili la kuuzwa machimbo hayo Watanzania hatukuwahi kulisikia? Isije kuwa wanataka kutucheza shere kwa kuuza machimbo ambayo si ya kwao.

Waziri wa madini S. Muhongo alipotoa kauli kwamba walipe 30% ya kodi bila kutoa excuses zozote vinginevyo wafunge virago alitoa kauli ambayo inaonyesha Tanzania ndio mmiliki wa machimbo yote ambayo makampuni mbali ya uchimabji dhahabu wanachimba dhahabu hiyo.

Serikali inabidi ifafanue haraka kuhusu hii kauli ya Barrick kutaka kuuza machimbo ya dhahabu. Ni nani mmiliki halali wa machimbo ya dhahabu nchini? Ni makampuni kutoka nje ya Tanzania au ni ya Watanzania?
 
Safi sana, ni vyema wote ambao hawataki/hawakubaliani/hawajisikii vizuri na taratibu mpya waondoke maramoja.:hat:
 
Mkuu Nakubaliana na wewe lakini kwa kuongezea huenda mawe yameanza kuisha wanawuzia wachina hayo mapango na hiyo mivifaa Yao tu
yawezekana kabisa wameshaona mawe hayatoshi tena, sasa wanataka kukwepa kulipa mafao yetu na kodi zetu. mie binafsi sijaona faida ya owepo wao hapa zaidi ya hasara ya kutuulia ndugu zetu na then kutuachia mashimo matupu.
 
Wamestukia kuwa 2015 mgodi utakuwa hauuziki. Hivyo wameamua kuwaingiza mkenge Wachina ili waikimbie nguvu ya umma mapema.
 
Wamestukia kuwa 2015 mgodi utakuwa hauuziki. Hivyo wameamua kuwaingiza mkenge Wachina ili waikimbie nguvu ya umma mapema.


Kuondoka kwa Barrick kwa vyovyote vile itakuwa baraka kwa Tanzania. Wamefika mahali hawa jamaa wanaua ndugu zetu (kwa kushirikiana na serikali - polisi) kama wanavyotaka. Kisa ni madini waliyotunyang'anya. Wakiondoka itakuwa ahueni kwani tuna fursa ya kupata ambao labda wataheshimu haki yetu ya msingi ya kuishi yaani uhai wetu. Barrick wamefika mahali ambapo uongozi wao unatamba waziwazi kuwa umeiweka serikali mfukoni. Hili si jambo jema hata kidogo kwa nchi yetu hata kama serikali yenyewe ingependa ibaki mifukoni mwa wawekezaji hawa. Wakiondoka serikali yetu itakuwa haina namna ila kutoka mifukoni mwa Barrick.
Hata hivyo ujio wa Wachina inabidi uchukuliwe kwa tahadhari kubwa. Moja kati ya "vijinufaa" tunavyopata kwa wawekezaji wa sekta ya madini ni ajira. Lakini miradi mingi ya wachina (ujenzi kwa mfano) imejaza wachina wengi kwelikweli na kutuacha watanzania tukiwa vibarua wao tu. Hali hii ikihamia kwenye madini basi manufaa yake kwetu yatapungua mno kiasi cha kutokuwa na maana. Ila kuhusu uwepo wa madini, hatuna haja ya kuwa na wasiwasi wowote, madini bado ni mengi sana. Waliyochimba kwa miaka kadhaa sasa ni sehemu ndogo sana ya hazina ambayo Mungu ameikirimia nchi yetu. Sasa hivi watakuwa wanamalizia Tulawaka (pengine wana miaka mitatu au zaidi kidogo) lakini huko kwingine hazina ni kubwa hasa Bulya ambako hata miaka 30 ijayo waweza kukuta bado kunachimbwa.
Serikali nayo imetukuka kwa uzembe na ujuha katika sekta hii. Makampuni yanauza ardhi na madini yetu bila serikali kupata walau kodi yake? Sababu hasa ni nini? Mwekezaji anakuwaje na haki ya kuuza madini yetu bila wenye madini kuambulia chochote? Kama alivyoeleza mmoja wa wanabodi humu ni kweli kuwa kampuni kadhaa za Canada zilifaidi sana kuuza migodi yetu bila nchi yetu kuambulia chochote. Mpaka sasa hali itakuwa hivyohivyo. Huu sijui tuuiteje maana ni zaidi ya udhaifu.
Suala lingine ambalo serikali imezembea ni kodi. Hebu angalia ni kodi kiasi gani matajiri hawa wa Barrick wamesamehewa kwenye mafuta na ile ya makampuni? Hii yote eti ilikuwa kuwabembeleza wasiondoke. Matokeo yake hao wanauza hisa zao na kuishia. Kwa bahati mbaya kodi wanayokwepeshwa makampuni haya si hiyo tu ya kuuza na ya makampuni wana mchezo mwingine. Mchezo wenyewe ni wa kuhakikisha kuwa wafanyakazi wageni nao hawalipi kodi. Wafanyakazi hao hulipwa mishahara yao hukohuko kwao na wawapo Tanzania hupewa posho tu ya kijikimu ambayo hailipiwi kodi. Hasara tunayopata hapo ni kubwa sana kwani kwa kawaida mishahara ya hawa wageni ni mikubwa mara kadhaa ya wenyeji wenye ujuzi unaofanana. Hivyo sehemu kubwa ya gharama za malipo ya mishahara kwa kampuni hizi huenda kwa wageni hata kama ni wachache kuliko wenyeji. Kwa hali hiyo kodi inayopatikana ya mapato ni ndogo kwani ni wenyeji tu ndio wanaotozwa kodi hiyo. Pili, uwepo wa wageni ni sawa na kuwanyima wenyeji fursa za ajira na kuongeza gharama za uendeshaji wa kampuni hivyo kuchelewesha ulipaji wa kodi ya makampuni. Hali hii ikiachwa iendelee chini ya menejimenti ya Wachina itakuwa mbaya zaidi kwani wao kwa desturi yao wanasaka ajira ya watu wao ambao ni wengi mno ulimwengu mzima.
Tanzania ili angalau iongeze manufaa yanayotokana na madini inalazimika kuweka sheria mahususi kwa ajili ya kuyapata maufaa hayo. Naungana na profesa kuwa madini hayaozi na yakiondoka yameondoka, hayachipui tena kama mimea. Lazima wawekezaji waachwe wafanye biashara zao bila kudekezwa. Muda wa misamaha ya kodi umepita. Kama mwekezaji hajahamasika tu mpaka leo huyo hatufai, aondoke tu hata kama kwa mtindo wa Barrick. Tusiachiwe mashimo ambayo madini yaliyotoka humo hayakutusaidia.
 
Tunayo STAMICO, na inalipa watu kila mwezi. Sijui wanafanya kazi gani.

Ndugu, huwatendei haki STAMICO. Taarifa zilizopo ni kwamba kabla hata Barick hawajauziwa huo mgodi, tayari ilikuwepo kampuni ya Kahama Gold Mine na bodi yake ya wakurugenzi. Lakini kwa ufisadi mgodi ukauzwa kinyemela kwa mwekezaji "mjanja" ambaye naye aliuuza kwa Barick kwa bei ya kufa mtu? Watanzania wenzangu tusilaumu tulipoangukia, tuangalie kwanza ni wapi tulipojikwaa.
 
China National Gold, the state-owned miner, is in talks to buy Barrick Gold’s stake in London-listed African Barrick, in a move that could lead to a full takeover and underscores the interest of Chinese miners in acquiring international assets.

Canada’s Barrick confirmed on Thursday that it was in preliminary talks about its 74 per cent holding in African Barrick, prompting an 8 per cent jump in the shares of Tanzania’s largest gold miner to 425.13p.

“Discussions are at an early stage,” Barrick said, adding that there is no certainty the sides will reach a deal. Shares in Barrick, which under its recently appointed chief executive Jamie Sokalsky has pledged a new focus on spending discipline and returns, rose 3.7 per cent to C$35.53.

Barrick has been working with investment bank UBS to consider a sale of its African Barrick stake, according to people familiar with the matter, which would trigger a full takeover offer for the London company under UK rules.

Zijin Mining Group, another state-backed Chinese company which has been seeking a higher profile on the world stage, had expressed an interest in African Barrick, people familiar with the matter told the Financial Times.

But Zijin’s preliminary approach was not considered sufficiently attractive to merit further consideration, they added, and the Canadian group was now talking only to China Gold.

Wu Zhanming, head of the overseas operations department at China Gold, confirmed the talks: “We are in a very preliminary phase of contact and discussion [with Barrick Gold Corporation].”

China Gold, the country’s largest gold producer, focuses on non-ferrous metals including gold, silver, copper and molybdenum and is directly controlled by China’s central government.

Should any party acquire more than 30 per cent of African Barrick, the buyer would have to make an offer for the whole company, under UK rules. If an offer for the company materialises – either from China Gold or another party – a committee of African Barrick’s independent directors would be charged with safeguarding minority owners’ interests.

African Barrick was floated in London by its parent in 2010 at 575p a share. But the miner has since struggled to hit production targets and has been battling power disruptions in Tanzania which have also pushed up costs.

With about 17m in reserves, the sheer size of Barrick’s resource base could be appealing to possible buyers, as could the miner’s sizable position in Tanzania to other African miners seeking diversification.

Source: FT.com

Link: China Gold in talks to buy African Barrick - FT.com
 
Ndugu, huwatendei haki STAMICO. Taarifa zilizopo ni kwamba kabla hata Barick hawajauziwa huo mgodi, tayari ilikuwepo kampuni ya Kahama Gold Mine na bodi yake ya wakurugenzi. Lakini kwa ufisadi mgodi ukauzwa kinyemela kwa mwekezaji "mjanja" ambaye naye aliuuza kwa Barick kwa bei ya kufa mtu? Watanzania wenzangu tusilaumu tulipoangukia, tuangalie kwanza ni wapi tulipojikwaa.
Labda sikusomeka vizuri. Nilichokusudia kusema ni kuwa kwanini serikali yetu inashindwa kuitumia STAMICO kuchimba haya madini badala yake wanawapa wezi kwa kisingizio cha wawekezaji? Mara nyingi kisingizio kimekuwa uwezo mdogo wa mtaji, lakini ukiwa na mali hii unashindwaje kukopa ili kupata mtaji huo unaouhitaji?

Kuna ushahidi usiotiliwa shaka kuwa makampuni haya yameweka kiasi kikubwa sana cha hongo kwenye akaunti za tuliowaamini kutuongoza. Nimesikitishwa na kitendo cha Zitto kushindwa kuwataja wenye mapesa hayo pamoja na kinga aliyonayo annapokuwa bungeni.
 
Huu ni utapeli wa mchana kweupe,mchezo wanaocheza ni kuwa wakimaliza tax excemption ya miaka mitano wanamuuzia mwingine naye pia anapewa excemption,same story ya zain,alafu airtel etc,hiyo kampuni ilanzihswa na wacanada waitwao PRACEDOM nao walipomaliza miaka mitano wakawauzia Barrick na wao sasa wamechoka kulipa kodi wanataka kummuzia mwingine,yawezekana pia wamesoma upepo wa 2015 kuwa kuna uwezekano wa kuja Govt serious zaidi na hivo kuwabana kwenye kodi.Ngoja anunue Mchina naye apewe excemtion ya miaka 5 naye akimaliza amuuzie mwingine.Hakuna issue ya umeme hapa.
 
Friday 17th August 2012, 1:43am
CATHY ADAMS
SHARES in African Barrick Gold (ABG) jumped by eight per cent in trading yesterday on news that it could be the subject of a £1.5bn bid battle.

A source close to the company said several bidders were circling the London-listed gold producer, which is 74 per cent-owned by its parent Barrick Gold, but only a bid from China Gold was being taken seriously.

Canada’s Barrick Gold, which is the world’s largest gold producer, confirmed yesterday that it was in preliminary discussions with China Gold regarding a sale of its stake in ABG, as part of its global asset review.

It is thought that another China gold producer, Zijin, was also looking at ABG, but the bid was considered too low for consideration. Randgold Resources has also been rumoured to be circling around Barrick Gold’s African arm.

FTSE 250 company ABG was floated on the London Stock Exchange in 2010 by the Canadian producer at 575p a share.

It is understood that Barrick would consider a deal at around 500p a share, which values it at £1.5bn.

If China Gold acquires more than 30 per cent of ABG, it will be required to make a formal offer for the whole company.

Cailey Barker, mining analyst at Numis Securities, said there was “a good chance of a sell-down”.

Barrick is being advised by Simon Lyons, Sam Roberts and Paul Knight from investment bank UBS on the deal. Lyons and Roberts have previously advised on the BA and Iberia merger and Vodafone’s acquisition of CWW respectively.
 
Hahaha kalagabaho tushaachiwa mahandaki wanataka kuja kwa staili na majina mengine au wameona M4C watachukua nchi na kutaifisha mali zao ndio wanataka kumuachia mngine kesi wajinga ndio waliwao naililia nchi yangu na kizazi changu natamani 2015 iwe kesho Kama sio keshokutwa
 
Kwani matatizo ya umeme Bongo yameanza leo au jana? Mbona tangu walipoingia nchini tangu mwaka 2000 hawakuona kama ni tatizo hadi miaka 12 baadaye!? Hawa naona wamestukia agizo la kulipa kodi ya 30% lililotolewa na Waziri mpya wa Madini na Nishati Sospeter Muhongo.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ng-companies-to-pay-30-pct-corporate-tax.html


Hawa wanatishia nyau tu; hawawezi kuondoka. Unajua kuwa Minelife ni ndefu sana Tulawaka na Bulyanhulu. Sina Uhakina sana na Minelife ya Buzwagi lakini najua kwamba ndo kwanza kunakucha pale. Nani atakatua matuta kwenye eneo lenye miti mingi kisha amwachie mwingine kupanda na kuvuna? Halafu eneo lenye mali kupindukia ni pale North Mara, ambako ratio ya gold katika tani ya mawe ni maeneo ya wakia kati ya 7 na 9 nadhani--ambayo ni kubwa kuliko sehemu nyingi sana duniani wanakochimba Gold.

Wataondoka wana kichaa? Wanatishia nyau tu hawa, ingawa panaweza kuwapo hofu ya Administration mpya ambayo ipo in the offing nchini. Walishazowea kujiamria cha kufanya kutokana na kuiweka administration iliyopo mfukoni. So Hili la hofu linaeza kuwapo so labda wanatishia tu Watanzania waseme hee?! Wanaondoka ! Wanataka kuondoka? Waache waondoke tuone kama wana ubavu huo....
 
Kama wazungu wanafunga virago kwa sababu ya Umeme na wanasema hawawezi kulipia wafanyakazi wao michango ya NSSF je hawa wachina walivyo mabahili umeme watatoa wapi na pia wanajulikana kuwa huwa hawalipi michango ya mafao.

Katika hali ya kawaida ingekuwa nchi zilizoendelea au zenye nia ya kuendelea waziri wa uwezekaji kama Mary Nagu angekuwa anaenda mbio ili hawa jamaa wasiondoke lakini kama sikosei Mary Nagu atakuwa bize kutafuta misafara ya mikutano ya nje ya nchi ili apate per diem.

Ripple effect ya hawa jamaa kuondoka ni kubwa mno...imagine watu wangapi watakosa ajira, tazama supply chain yao locally ikoje, serikali pia itakosa mapato

Lakini kwa sababu sisi hayo sio muhim kwetu HILI NALO LITAPITA

Wachina mpaka leo hawajaleta ripoti ya mgodi waliopewa wa Kiwira.

kazi kwenu

That's Capitalism in Highest Stage Profit
Maximization, they don't keep business for the rest of the business breakdown

F.Y.I the deal is note done yet... they are talking on selling but not sold as per your heading refers..
 
Hakuna cha umeme au nini, hawa jamaa wamekuwepo hapa nchini zaidi ya miaka 10 na tatizo hili la umeme lina karibia miaka 20 sasa, kimsingi wameshtuka faida nono sasa itapungua baada ya waziri kuwataka walipe kodi.
 
kila media nakuta "barrick in talks with.." nilitegemea kuona serikali ya tz ikiwa regulator wa wawekezaji wa madini kama ilivyo BOT kwa mabank yote ya tz, sasa kama hawa barrick wanajifungia vyumbani kudiscuss deals na makampuni mengine pasipo kuihusisha tz kwenye mazungumzo kati ya pande mbili basi naona kuna uwezekano mkubwa sana wa kufanya biashara haram kwa kuishusha thamani halisi ya mgodi kimaandishi ili wao wawili wapige fedha ndefu na govt yetu kuambulia kiduchu.

Kwanini tusiwe na sheria kama ilivyo baadhi ya nchi za africa, asia na euro ambapo hata kama investor anashare 99% akitaka kuuza share zake ni lazima kuwaconsult govt then govt itoe go ahead na govt ndiyo itahusika kupanga bei ya hisa, na si kama hii deal la ajabu la kupanga bei kwa mkoloni london
 
Back
Top Bottom