figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,714
- 59,241
Hatimaye Benk ya Barclay yainunua Benki ya Taifa ya Biashara (NBC Tanzania), Pasipo shaka yoyote naweza sema NBC tanzania ipo chini ya Barclays kutokana na mienendo ya bank hizo mbili.
Kitu cha kwanza, ni kukutana na majina ya Barclays katika Ofisi za Bank ya NBC wakati ni Mshindani wake, Hii inatia shaka.
Kitu cha pili ni kushare wafanyakazi. Yaani si ajabu mfanyakazi wa Barclays kumkuta NBC au Mfanyakazi wa NBC Tanzania Kumkuta kule Barclays.
Kitu cha tatu kinachofanya niseme Barclays imeinunua NBC Tanzania, ni Kitendo cha Managing Director wa Barclays Misri bwana Edward Marks, kuletwa NBC Tanzania na kuwa Managing Director wa NBC Tanzania.
Banki ya Taifa ya biashara (NBC) inao uzoefu usiopungua miaka 47 katika kutoa huduma za kibenk huku ikiwa na Mtandao wa Matawi yasiopungua 52 na Visa ATM zaidi ya 250 nchi nzima.
Kilichonifanya nianzishe hii Thread ni kutaka kujua;
1. Kwanini NBC isibadilishe mabango yao yawe Barclay wakati kiutendaji wapo kibarclays?
2. Kwani wajifanye NBC na Barclays ni washindani wakati ni kiini Macho?
3. Tanzania ina hisa NBC, Je wakibadilisha Jina na kuwa Barclay kuna Tatizo litakalotokea?
4. Je hii ni njia ya Kutuibia Tanzania au hakuna Tatizo?
Kitu cha kwanza, ni kukutana na majina ya Barclays katika Ofisi za Bank ya NBC wakati ni Mshindani wake, Hii inatia shaka.
Kitu cha pili ni kushare wafanyakazi. Yaani si ajabu mfanyakazi wa Barclays kumkuta NBC au Mfanyakazi wa NBC Tanzania Kumkuta kule Barclays.
Kitu cha tatu kinachofanya niseme Barclays imeinunua NBC Tanzania, ni Kitendo cha Managing Director wa Barclays Misri bwana Edward Marks, kuletwa NBC Tanzania na kuwa Managing Director wa NBC Tanzania.
Banki ya Taifa ya biashara (NBC) inao uzoefu usiopungua miaka 47 katika kutoa huduma za kibenk huku ikiwa na Mtandao wa Matawi yasiopungua 52 na Visa ATM zaidi ya 250 nchi nzima.
Kilichonifanya nianzishe hii Thread ni kutaka kujua;
1. Kwanini NBC isibadilishe mabango yao yawe Barclay wakati kiutendaji wapo kibarclays?
2. Kwani wajifanye NBC na Barclays ni washindani wakati ni kiini Macho?
3. Tanzania ina hisa NBC, Je wakibadilisha Jina na kuwa Barclay kuna Tatizo litakalotokea?
4. Je hii ni njia ya Kutuibia Tanzania au hakuna Tatizo?