Kweli technolojia imepanuka,nilienda Mwanza siku moja.
Nikashuka Stendi Moja ya mabasi,saa 12.30jioni hivi.Nikaenda kutafuta chumba cha kulala gest house ya jirani na stendi.
Nilipokaribia tu,dada mmoja akanidaka.Karibu kaka,tuna vyumba vizuri kwa bei nafuu,kila huduma inapatikana.
Akaomba kupokea begi langu nikagoma.
Nikamfuata nikijua ni muhudumu wa gesti hiyo,bahati yangu kumbe pale best vyumba vimekwisha,wakamwambia jaribu kwa Jirani.
Nikatoka usingizini,nikajua naingizwa town.
Akanisihi twende gest nyingine,nikaona nikikataa pale pale anaweza kupiga yowe za mwizi au kufanya vinginevyo ili tu anitoe pesa.
Nikamwambia twende sehemu nyingine.
Kwa furaha akatangulia hadi gesti iliyofuata,akauliza chumba na kuambiwa 20,000 self room.Akaniambia nilipe kwani kimebakia hicho tu.
Nikajidai kuchungulia,yeye kasimama ndani akijua atavuna kitu!
Nikamwambia mhudumu mimi nina sh.10,000/- tu.
Akanisihi sana hiyo dada nilipe.
Nilivuta kiti pale mapokezi nikakaa na kumuuliza,hivi wewe ni nani mbona unanifuata kila mahali unanijua?
Akapigwa mshangao,kwa aibu aliondoka.Baada ya dakika kama kumi,muhudumu yule akaniambia leo ungeingia mjini.Ila usilale hapa maana ataita vijana wakufuate usiku.
Niliondoka nikapanda Boda boda nikahama mtaa.
Mjini shule!