MchunguZI
Platinum Member
- Jun 14, 2008
- 4,047
- 2,239
Nimempokea kijana wangu aliyekuwa anamalizia mitihani yake ya fomu siksi na swali langu la kwanza kama kawaida ya mzazi ikawa ni juu ya hali ya mitihani. Jibu la kijana ni kwamba mitihani ilikuwa ya kawaida. Baada ya mazungumzo ya muda kidogo, kijana amefunguka na kunihakikishia kwamba atashinda maana maswali mengi yalijulikana kabla ya muda.
Mimi ni baba, imebidi niulize aliipata wapi? Je, ni waalimu wanawasidia vijana wao? Jibu ni kwamba maswali yote walikuwa wakiyapokea kwa njia ya whatsapp toka Dar es Salaam. Kwa hakika kabisa kijana kawataja wanafunzi wa shule ya Tusiime kwamba ndo yalikokuwa yakitokea. Somo la jiografia ametaja kwamba hilo waliletewa picha halisi kabisa ya mtihani ingawa mengine ilikuwa ni swali moja moja. Nakumbuka shule hii mwaka jana imepongezwa kwa ufaulu mzuri, sasa kumbe mambo yenyewe ndo yalivyo.
Lawama zangu ni siasa iliyoingizwa NECTA na miaka miwili tu tangu Ndalichako kuondoka, sasa mitihani inazidi kuwa ni njugu barabarani!
Ndalichako alikuwa na mipango ya kuondokana na tatizo hili sasa naona liko palepale na hisia yangu litakuzwa na ushindani wa shule za private zikishindana kuvuta wateja. Je, tutafika?
Mimi ni baba, imebidi niulize aliipata wapi? Je, ni waalimu wanawasidia vijana wao? Jibu ni kwamba maswali yote walikuwa wakiyapokea kwa njia ya whatsapp toka Dar es Salaam. Kwa hakika kabisa kijana kawataja wanafunzi wa shule ya Tusiime kwamba ndo yalikokuwa yakitokea. Somo la jiografia ametaja kwamba hilo waliletewa picha halisi kabisa ya mtihani ingawa mengine ilikuwa ni swali moja moja. Nakumbuka shule hii mwaka jana imepongezwa kwa ufaulu mzuri, sasa kumbe mambo yenyewe ndo yalivyo.
Lawama zangu ni siasa iliyoingizwa NECTA na miaka miwili tu tangu Ndalichako kuondoka, sasa mitihani inazidi kuwa ni njugu barabarani!
Ndalichako alikuwa na mipango ya kuondokana na tatizo hili sasa naona liko palepale na hisia yangu litakuzwa na ushindani wa shule za private zikishindana kuvuta wateja. Je, tutafika?