Baraza la mitihani liseme ukweli kuhusu kutoa list ya wanafunzi bora

LUS0MYA

JF-Expert Member
Aug 4, 2011
862
1,097
Kuna kitu hakipo sawa katika mitihani ya kidato cha nne na jinsi matokeo yalivyo. Nimeambatanisha matokeo ya shule moja ambayo wanafunzi wake wote wamepata daraja la kwanza lakini karibu wanafunzi wote wamepata pointi 7 ambazo ni Alama za juu kwa ufaulu kwa mwanafunzi.Na zipo shule nyingine za mfano huu...kama baraza la mitihani lilifanya makosa katika utungaji na upangaji wa maswali wahusika wachukuliwe hatua....haya siyo matokeo ya kawaida na kwa vyovyote vile utangazaji wa shule bora au wanafunzi ungefanya jamii kugundua hili....baraza la mitihani limenajisi elimu ya tanzania.
IMG-20230130-WA0024.jpg
 
Lusomya uko sahihi kabisa, kuna jambo haliko sawa (Limefichwa hapa na mamlala) kwenye utungaji, ufanyaji wa mitihani na hadi usahihisaji wa mitihani hii ya four four mwaka 2022. Nivema Wizara ya Elimu na Baraza la Mitihani wakawa wakweli tu na kutupa sababu za msingi za maamuzi waliyoyafanya kwa mwaka huu kutokutangaza shule zilizoongoza kufanya vizuri (top 10) na majina ya wanafunzi waliofanya vizuri (top 10).

Kwasababu ukifanya tathmini hii independently utaelewa kwanini waliona wafiche ukweli kwavile utaweza kuona ni shule nyingi sana zimepata alama zinazofanana na sio shule tu, hadi darasa zima linapata maksi sawa tena A's. Hii haiwezi kuwa sahihi, unawezaje kuwa na wanafunzi zaidi ya 50 kwamfano na wote wakawa nauelewa sawa na kujibu mtihani sasa.

Kwa tathmini ya haraka unaweza kupata hakuna top 10 tena ila kuna top 20 au 30 au zaidi kwa waliofaulu vizuri na vivyohivyo kwa walio feli mitihani hiyo. Nadhani waliona wakitanganza kama ilivyo kawaida, itaonyesha mapungufu makubwa sana katika process nzima ya mitihani hiyo kanzia utungwaji wa maswali, jinsi wanafunzi walivyojibu mitihani na hata na usahihishaji had wake.

Kwavile katika kusahihisa mapungufu haya yalipaswa kuonekana wazi na hatua kuchukuliwa na sio kutoa sababu ambazo hazina mashiko na kutotangaza kama ilivyokawaida.

Ushauri wangu ni kuwa, dawa ya jipu ni kulipasua na sio kuficha madhaifu haya, kwasababu madhara yake kwa Taifa ni makubwa zaidi huko baadae, kuliko faida ya muda mfupi wanayodhani wameipata sasa kwa kuficha ukweli. Pengine iundwe tume huru ya uchunguzi ili ukweli ujulikane na tupate mapendekezo ya tume hii ya hatua zinazostahili zichukuliwe kurekebisha mapungufu hayo kwa taasisi zote zilizohusika kwa namna moja au nyingine, hata ikibidi mtihani wote kurudiwa, ni heri tukaingia gharama sasa na kurekebisha kuliko kujidanganya kwa matokeo haya.
 
Nina mdogo wangu amesoma shule hizi za gharama kubwa ...nmewahi kumuuliza pepa la fom4 alikiri walisolve pepa 1 week b4
 
Wasiwasi wangu Zanzibar wameshika mkia kama kawiaida yao ila wanafichiwa aibu.
Hayawani na lazima awe na fikra zinazochochewa na hisia kama hizo zako hivyo hakuna cha kushangaza. Great thinkers ndo huwa na mijadala jadadivu kama hii.
 
Kuna kitu hakipo sawa katika mitihani ya kidato cha nne na jinsi matokeo yalivyo. Nimeambatanisha matokeo ya shule moja ambayo wanafunzi wake wote wamepata daraja la kwanza lakini karibu wanafunzi wote wamepata pointi 7 ambazo ni Alama za juu kwa ufaulu kwa mwanafunzi.Na zipo shule nyingine za mfano huu...kama baraza la mitihani lilifanya makosa katika utungaji na upangaji wa maswali wahusika wachukuliwe hatua....haya siyo matokeo ya kawaida na kwa vyovyote vile utangazaji wa shule bora au wanafunzi ungefanya jamii kugundua hili....baraza la mitihani limenajisi elimu ya tanzania.View attachment 2500495
Mtihani wa form four umevuja mbaya mwaka jana
 
Sababu nyingine ni kwamba kule anakotaka bi mkubwa shule zake zote zipo kweye Kumi za mwisho
 
Kuna kitu hakipo sawa katika mitihani ya kidato cha nne na jinsi matokeo yalivyo. Nimeambatanisha matokeo ya shule moja ambayo wanafunzi wake wote wamepata daraja la kwanza lakini karibu wanafunzi wote wamepata pointi 7 ambazo ni Alama za juu kwa ufaulu kwa mwanafunzi.Na zipo shule nyingine za mfano huu...kama baraza la mitihani lilifanya makosa katika utungaji na upangaji wa maswali wahusika wachukuliwe hatua....haya siyo matokeo ya kawaida na kwa vyovyote vile utangazaji wa shule bora au wanafunzi ungefanya jamii kugundua hili....baraza la mitihani limenajisi elimu ya tanzania.View attachment 2500495
Naona Saba saba tu
Hao wenye 8 na 9 ndio wanaonekana hawakuwa serious 😁😁
 
Aisee hapo kuna utata wa hali ya juu..so darasa zima uelewa ni mmoja kwa wanafunzi wote na majibu ni sawa kw kila mwanafunzi...upuuzi huu..
Hiyo shule mchujo unanza pre form one form two mchujo na wanaweka wastan wa juu ili asiyefika atoke

Vichwa timamu ndo vinabaki kuwa 1.7 sio ishu sana ya kujadili
Ndani yake humu wenye wanatengana A 85 zote hiyo tayat 1.7

Afu anakjja mpuzi anapata A97

Je tutafanana nafasi?
 
Zamani Div one point 7 ilikuwa inapatikana kwa mbinde tena kwa wale Joni visomo
Ila sasa hadi kilaza wa darasa anapata one ya 7
 
Back
Top Bottom