GwaB
JF-Expert Member
- Mar 19, 2014
- 5,144
- 6,910
Tangu kuanza kwa utawala wa awamu ya nne kumekuwa na kasi kubwa ya ujenzi wa miundombinu karibu pande zote za nchi hii.
Pamoja na kwamba ujenzi huo ulianzia kwenye awamu ya tatu chini ya raisi mstaafu BWM,Waziri wa sasa miundombinu kwa kiasi kikubwa sana amebakia kuwa msimamizi na kiongozi wa wizara hii na kwa mtaji huo ameteuliwa na chama tawala kugombea nafasi ya urais katika awamu ya tano.
Pamoja na kuwa na sifa ya uchapakazi ambayo ndio sifa inayohusishwa na ujenzi wa barabara na madaraja katika ya awamu ya nne,Mhe.John Pombe Magufuri tayari amebatizwa kuwa ni BULLDOZER kwa kuwa yeye ndiye anatwishwa mzigo wa kukisafisha chama tawala,na hasa kunadi mafanikio yaliyopatikana katika kujenga miundombinu ya nchi hii,Nawauliza watanzania wenzangu kama kweli tunaridhishwa na viwango vya barabara tunazokabidhiwa kuwa zimekamilika,hapa nikilenga vigezo kama unene wa lami inayowekwa,upana wa barabara,kingo za barabara,elevation za barabara zetu na zaidi sana alama za barabarani.
Nimesafiri kwa barabara tanzania nzima kupitia kwenye hizi barabara zetu zinazonadiwa kuwa zinajengwa karibu nchi nzima lakini kwa masikitiko makubwa nashindwa kuelewa ni kwa nini wataalamu wetu walioaminiwa katika wizara ya miundombinu,pamoja na kuwa na exposure ya kutosha,kusafiri nje ya nchi kujifunza,Wanakubali vipi kupokea miradi ya barabara iliyokamilika lakini chini ya viwango?.
Ni kweli kabisa enzi za Mkapa ili kufika Mwanza,Musoma,Bukoba kwa lami ililazimu kupitia Kenya,vinginevyo vumbi ndiyo ilikuwa mpango mzima.
Pamoja kuwa sasa unaweza kusafiri kupitia kwenye barabara ya lami kutoka Dar hadi Mwanza,Mtwara,Songea,Mbeya,Rukwa,Tanga na Arusha.Je ni kweli kuwa tuna barabara za kujivunia tukilinganisha na majirani zetu?
Nadiriki kusema wazi kuwa barabara zetu ni finyu,ziko chini ya viwango na kwa ajili hiyo zinaharibika baada ya muda usiozidi hata miaka mitano.
Ningependa wadau tulijadili hili kwa kutumia uzoefu tuliowahi kuuona katika barabara za nchi mbali mbali ambazo baadhi yetu humu tumeziona na kuzipitia.Hasa wale waliowahi kusafiri nchi ulaya na asia watupe uzoefu wao.Nawasilisha.
Pamoja na kwamba ujenzi huo ulianzia kwenye awamu ya tatu chini ya raisi mstaafu BWM,Waziri wa sasa miundombinu kwa kiasi kikubwa sana amebakia kuwa msimamizi na kiongozi wa wizara hii na kwa mtaji huo ameteuliwa na chama tawala kugombea nafasi ya urais katika awamu ya tano.
Pamoja na kuwa na sifa ya uchapakazi ambayo ndio sifa inayohusishwa na ujenzi wa barabara na madaraja katika ya awamu ya nne,Mhe.John Pombe Magufuri tayari amebatizwa kuwa ni BULLDOZER kwa kuwa yeye ndiye anatwishwa mzigo wa kukisafisha chama tawala,na hasa kunadi mafanikio yaliyopatikana katika kujenga miundombinu ya nchi hii,Nawauliza watanzania wenzangu kama kweli tunaridhishwa na viwango vya barabara tunazokabidhiwa kuwa zimekamilika,hapa nikilenga vigezo kama unene wa lami inayowekwa,upana wa barabara,kingo za barabara,elevation za barabara zetu na zaidi sana alama za barabarani.
Nimesafiri kwa barabara tanzania nzima kupitia kwenye hizi barabara zetu zinazonadiwa kuwa zinajengwa karibu nchi nzima lakini kwa masikitiko makubwa nashindwa kuelewa ni kwa nini wataalamu wetu walioaminiwa katika wizara ya miundombinu,pamoja na kuwa na exposure ya kutosha,kusafiri nje ya nchi kujifunza,Wanakubali vipi kupokea miradi ya barabara iliyokamilika lakini chini ya viwango?.
Ni kweli kabisa enzi za Mkapa ili kufika Mwanza,Musoma,Bukoba kwa lami ililazimu kupitia Kenya,vinginevyo vumbi ndiyo ilikuwa mpango mzima.
Pamoja kuwa sasa unaweza kusafiri kupitia kwenye barabara ya lami kutoka Dar hadi Mwanza,Mtwara,Songea,Mbeya,Rukwa,Tanga na Arusha.Je ni kweli kuwa tuna barabara za kujivunia tukilinganisha na majirani zetu?
Nadiriki kusema wazi kuwa barabara zetu ni finyu,ziko chini ya viwango na kwa ajili hiyo zinaharibika baada ya muda usiozidi hata miaka mitano.
Ningependa wadau tulijadili hili kwa kutumia uzoefu tuliowahi kuuona katika barabara za nchi mbali mbali ambazo baadhi yetu humu tumeziona na kuzipitia.Hasa wale waliowahi kusafiri nchi ulaya na asia watupe uzoefu wao.Nawasilisha.