KERO Barabara Tegete A ni kero, kama wameshindwa kuboresha watuambie Wananchi tujichange

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Wakazi wa Tegeta A (maarufu kwa Bedui) tuna kero ya Barabara, huu ni mwezi wa tano sasa unaelekea wa sita, barabara ni mbovu na inatuumiza Watumiaji.

Barabara ninayoizungumzia hapa ni ile ya vumbi kutoka kwenye lamı ya kwenda Madale mpaka Centre maarufu kwa jina la Bedui.

Barabara imechimbika, mashimo kila siku yana maji, imemeguka pembeni yaani hata kupishana na Bodaboda ni shida, kila siku magari tunayapeleka services kutokana na kuharibika, ikinyesha mvua ndio kabisa hali inazidi kuwa mbaya.

TARURA wapo; Mbunge yupo, Diwani yupo lakini hakuna kinachofanyika.

Yaani kuna muda unatamani hata Wananchi tuchangishwe ili itengenezwe kwa nguvu zetu kama barabara haiwezi kuchongwa walau kuziba mashimo yaliyopo.

Mamlaka husika waangalie hili linatuumiza kwa kiwango kikubwa sana.
WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.54_7608e6bb.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.50_0054701c.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.48_d2f0466c.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.53_ad43a561.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.46_ad1e6b8d.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.47_6ffd51ff.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.54_2591f868.jpg

WhatsApp Image 2024-03-23 at 15.11.46_ea8d24b6.jpg
 
Mjichange tu achaneni kuwa subiria serikali maana wao watakuja hapo 2050

Ova
 
Wakazi wa Tegeta A (maarufu kwa Bedui) tuna kero ya Barabara, huu ni mwezi wa tano sasa unaelekea wa sita, barabara ni mbovu na inatuumiza Watumiaji.

Barabara ninayoizungumzia hapa ni ile ya vumbi kutoka kwenye lamı ya kwenda Madale mpaka Centre maarufu kwa jina la Bedui.

Barabara imechimbika, mashimo kila siku yana maji, imemeguka pembeni yaani hata kupishana na Bodaboda ni shida, kila siku magari tunayapeleka services kutokana na kuharibika, ikinyesha mvua ndio kabisa hali inazidi kuwa mbaya.

TARURA wapo; Mbunge yupo, Diwani yupo lakini hakuna kinachofanyika.

Yaani kuna muda unatamani hata Wananchi tuchangishwe ili itengenezwe kwa nguvu zetu kama barabara haiwezi kuchongwa walau kuziba mashimo yaliyopo.

Mamlaka husika waangalie hili linatuumiza kwa kiwango kikubwa sana.
Hii ina afadhali sana,ungeziona barabara za kwembe,malamba mawili na king'azi sijui ingekuaje
 
Tatizo hata ukarabati unaofanyika hauna kiwango wanaenda kumwaga tu kifusi juu juu wanapiga hela wanaondoka mvua ikinyesha yanarudia pale pale mfano pia barabara ya kutoka bunju A mpaka madale ni mbovu sana ila ukarabati uliofanywa ni WA hali ya chini sana .
 
Back
Top Bottom