Barabara imejaa maji Tanga

Barabara imejaa maji Tanga

Kuna Magari yamekwama huko kutokana na barabara kujaa maji. Sijaona chombo chochote kimeripoti au wameshawachoka.
Kwa hiyo unatuambia sisi kwani sisi ndo tumeleta mvua? Au unataka tuje tuyanywe hayo maji ili nyie mpite? Wazigua mna tabu sana nyie
 
Baada ya kuusoma uzi huu nikajikuta nawakumbuka ndugu zangu walioko Tanga mashewa...Habar n mbaya nilizo zipata zaidi ya watoto wa 5 wamekufa maji...Huzuni sana...Ila wapo watu hufurahia hii hali
Mashewa nikifika Mara moja. Kwa jinsi kulivyo na hizi mvua, Mungu awasaidie Sana .
 
Kwamba helicopter inatua mjini mjini tu
Hapana. Kwamba watakaovushwa na helicopter watahitaji usafiri mwingine, na kama ni karibu na mjini inakuwa rahisi magari mengine kuja kuwabeba waliovushwa.

Kama sivyo, inabidi wenye mabasi wakubaliane kubadilishana abiria na kugeuza, kitu ambacho ni ngumu zaidi.
 
hatari sana
Nimeona na dereva wa basi la simba nae kaliingiza basi kibishi likazama kwenye korongo kisa kujifanya ujuaji mwingi hawa madereva sijui tuwaelimishe vipi kuwa mataili yana upepo yakiwa kwenye maji yanaelea shida wengi shule hamna so a simple physics theory wanashindwa kuijua
 
Handeni madaraja zaidi ya 3 yameenda na maji,

Daraja la Handeni kwenda Mziha Turiani Morogoro kule Kideleko limevunjika,

Daraja la Ndelema Handeni Kilindi kwenda Kiteto Mkoa wa Manyara limevunjika,

Daraja la Kati ya Handeni na Korogwe nalo limeenda na maji, nyumba zimeporomoka ,

Njia ya segera nayo ilikuwa haipitiki

Handeni wanahitaji misaada !
 
Back
Top Bottom