Heshima mbele wakuu! leo ninazungumzia upuuzi unaofanyika katika bar moja iliyopo wilaya ya kindondoni jijini Dsm ( Jina naihifadhi ). Mmiliki wa bar ni graduate kutoka chuo kimoja maarufu hapa mjini..Kwa sisi wadau tunaoishi karibu na bar hii huwa tunaenda pale kwan ajili ya kumsapoti tu jamaa na kubadilishana mawazo na wadau wengine..But kuna suala la kijinga sana linalofanyika ndani ya bar hii ambalo kama mmiliki asipokuwa makini, atakosa kabisa wateja...Hapo kwenye bar yake huwa kuna midume inakwenda pale kupiga soga, ( ipo kumi na mbili hivi na ushee ),, hawana hela ya kununua vinywaji, ukitokea mteja pale basi jamaa wanakufuata na kukuzoea zoea huku wakikuomba uwanunulie bia and all that,wakati mwingine wanaomba kununuliwa chakula ( " Kaka leo sina mzuka na pombe kabisa, coz nina dozi, ila napiga chips mayai, mishikaki miwili na soda moja tu! " ) hii ni sentensi ambayo binafsi nimekwisha tamkiwa zaidi ya mara tano na mmoja kati ya hao ma hardless poor excuses of male persons.....Wakati mwingine, jamaa huwa wanawanunulia watu wengine bia kwa kutumia bili za watu wengine. Kwa mfano, siku moja nimeenda pale na wadau wangu, kama kawaida jamaa wakajisogeza kwenye meza, na kuanza kujichekesha huku wakiomba bia, tukawapiga bia, baada ya kama dakika arobaini hivi, wakaja raia wengine kama wawili ( ambao wanajuana na hao majamaa ), jamaa mmoja akatoa order " weita wape bia mbilimbili hao jamaa, bili kwa hawa hapa ( anatusonta sisi ). Hii imeshatokea zaidi ya mara kumi na mbili.. Tumeshamlalamikia sana mwenye baa, tukimuomba apige marufuku hiyo tabia, but bila mafanikio yoyote, sasa tumeamua kutokwenda tena katika baa ya huyu jamaa, tangu tuazimie jambo hili ni mwezi mmoja sasa umekatika, na sio sisi tu, kuna wateja wengine wengi tu wameshakimbia baa, kuanzia alhamisi ya juzi jamaa amekuwa akitutext na kutupigia twende kwenye bar yake but tumekwisha kuwa disapointed......
ITS SO DISAPOINTED KUMUONA KIJANA WA KIUME AKIWA ANAOMBA OMBA VITU NA HELA KWA WANAUME WENZAKE...KAMA MAISHA YA MJINI YAMEKUSHINDA NENDA KIJIJINI UKALIME..SHAME UPON YOU, POOR EXCUSES OF MEN!