Bao la kisigino

Bao la kisigino

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,725
Reaction score
830,789
1472452018961.jpg


Ni aina ya bao kwenye soka ambalo hakuna anayetegea kama litafungwa, huja kiaina yake kimtindo na bila kipa kujiandaa au wale walinzi. Mpira hutikisa nyavu na hadhira kulipuka kwa shangwe na kelele za goooooo....!!!!

Hiki ndio kilichotokea wiki iliyopita Pale EL alipokutana uso kwa uso na Magufuli. Wengi hawakutarajia kile alichokifanya Lowassa, kwa tabasamu toka rohoni alimsabahi Magufuli bila chembe ya kinyongo! Katu Magufuli hakulitegemea hili na yeye bila kuficha hisia zake za ndani kabisa akakiita kitendo kile kama ni muujiza.

Ilikuwa ni 'brief moment' iliyoleta impact kubwa sana kisiasa hasa kwa upande wa Lowassa! Kwa kasi ya ajabu ikawa ni mjadala kila mahali lakini kote huko kete ikimwangukia Lowassa. Hamasa ya kumpongeza EL kwa kuonyesha uuungwana mkubwa kiasi kile umeikumba CCM hata kufikia nacho kutoa tamko rasmi la kumpongeza.

Kisiasa hili ni bao la kisigino na si la mkono
 
We nawe ni Mbulula tu,Fisadi wako kaenda kujipendekeza kwa wakubwa wake samaki ana nguvu akiwa majini lakini ukimtoa hana ujanja,nguvu ya Lowasa ilikua ndani ya CCM kwa sasa yupo kwenye foleni tu ya akina Mrema
Asante kwa kuja nadhani hii tune ya ufisadi wake ifanyieni kolabo sasa manake naona mnaishia kuponda huku mitandaoni nyuma ya ID bandia bila ithibati yoyote
 
Asante kwa kuja nadhani hii tune ya ufisadi wake ifanyieni kolabo sasa manake naona mnaishia kuponda huku mitandaoni nyuma ya ID bandia bila ithibati yoyote
Wewe huna chochote ukijuacho unafaa kuandika zile makala zako za uchawi ila kwenye siasa yaani kila siku unajiaibisha tu Magufuli kawatia wazimu
 
Asante kwa kuja nadhani hii tune ya ufisadi wake ifanyieni kolabo sasa manake naona mnaishia kuponda huku mitandaoni nyuma ya ID bandia bila ithibati yoyote
Kama kweli CCM ina ubavu, imuite LOWASSA kwenye hii mahakama mfu ya ufisadi ambayo kila kukicha wanashadidia.

Nakuhakikishia hakuna jiwe litasalia juu ya jingine, utashangaa Raisi amejishika mwenyewe
 
Kama kweli CCM ina ubavu, imuite LOWASSA kwenye hii mahakama mfu ya ufisadi ambayo kila kukicha wanashadidia.

Nakuhakikishia hakuna jiwe litasalia juu ya jingine, utashangaa Raisi amejishika mwenyewe
 
Watu hawawezi kupiga mawe kwenye mchongoma(mti wa miiba)
Mawe hurushwa kwenye mti
wenye matunda ili yadondoke, na ndipo mrusha mawe anapofaidi!
Kwa hiyo kujadiliana nao ni kuwapa faida waache wabwate Lowassa! Lowassa! Lowassa!
Wanamshangilia bila kujijua
 
Amemaliza kazi yake ya kujisafisha kutokana na ufisadi aliosingiziwa na chadema 2008. Sasa yupo tayari kurudi chama chake, anajiwekea mazingira safi. Safi sana Lowassa kwa kupiga bao la mkono, hivi sasa wewe ni mtu safi, Rais wao.
Sasa kwa nini asiruhusiwe kufanya mikutano ili "asafishike" vizuri zaidi?
 
Back
Top Bottom