Banjul, Gambia: Watetezi wa Haki za Binadamu wamsifu Rais Magufuli kwa kupambana na Rushwa, wamkosoa kuminya Uhuru wa Kujieleza

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
Asasi za kiraia zinazotetea Haki za Binadamu zaidi ya 18 toka Tanzania zinashiriki mkutano wa 63 wa Tume ya Haki za Binadamu barani Afrika huko Mjini Banjul kuanzia leo tarehe 22 hadi 30 Oktoba 2018.

E625CD9A-DB22-40C7-A930-D44F9D25E267.jpeg


Kabla ya kuanza mkutano huu, watetezi jana wameadhimisha siku ya haki za Binadamu Afrika wenye ujumbe wa “Pambana na rushwa kama njia ya kulinda Haki za Binadamu”.

Mada mbalimbali zimejadiliwa leo zikiwemo usalama wa Watetezi wa Haki za Binadamu na waandishi, rushwa, haki za watu wenye ulemavu, haki za wanawake, wazee na makundi maalum.

Suala la rushwa limeelezwa kuwa ni adui mkubwa wa haki za binadamu na kikwazo kwa watetezi wa haki za binadamu.

B7488E5A-A7D3-4E43-B5E4-A87F89EA3F77.jpeg


Pamoja na changamoto nyingi za haki za binadamu, watetezi kutoka Tanzania wameeleza kutambua jitihada anazonyesha Rais Magufuli katika kupambana na rushwa. Watetezi hao wameueleza mkutano huo kuwa katika eneo rushwa, Rais Magufuli amejaribu sana kulifanyia kazi na mambo mengi ambayo wamekuwa wakiyalalamikia na kuwashauri marais wengine barani Afrika waige mfano huo.

Changamoto kubwa kwa sasa Tanzania imebainishwa kuwa ni ukiukwaji wa uhuru wa habari, kujieleza na uhuru wa kujumuika.

Aidha, imeelezwa kuwa Demokrasia imeshuka sana nchini huku hali ya watetezi ikizidi kuwa mbaya na ya kuogofya.
 
Nawaunga mkono Magufuli anachapa kazi Sana udhaifu wa serikali yake upo kwenye utawala Bora
Nikiwa kama mwananchi,mwana CCM naomba Magufuli aliangalie Sana eneo hilo
 
Mbona hakuna mapambano ya rushwa zaidi ya kushughulika na " wasiochangia chama " ?
 
Mbona kuna watu wana Uhuru wa kujieleza kuliko kipindi chochite kile kwenye historia ya nchi yetu.

Kilichobadilika ni njia ya kujieleza zamani ilikuwa majukwaani ila sasa Twitter na Instagram kwa njia ya digital.

Kwa mara ya kwanza Mange anaweza kujieleza huku akimtukana rais na mama yake.

Zitto na Lema wamekuwa wakijeleza bila mipaka achilia mbali hapa JF watu wanavyoruka sarakasi kwa kutumia internet yenye spidi Kubwa iliyofanikishwa na juhudi za serikali ya CCM
 
Zitto na Lema wamekuwa wakijeleza bila mipaka....
Lema leo mmemuita Polisi kufanya nini, umesahau Kangi Lugola na Zitto? Sugu alifungwa Marekani? Lisu alijipiga risasi? Watu wanajiteka wenyewe? Waziri wa habari kusema ukweli katumbuliwa na kutolewa bastola hadharani asiongee na media, nani yuko huru na salama?
 
Lema leo mmemuita Polisi kufanya nini, umesahau Kangi Lugola na Zitto? Sugu alifungwa Marekani? Lisu alijipiga risasi? Watu wanajiteka wenyewe? Waziri wa habari kusema ukweli katumbuliwa na kutolewa bastola hadharani asiongee na media, nani yuko huru na salama?
huwa wanaitwa kutoa maelezo kidogo inapotokea sintofahamu,ni utaratibu wa kawaida kabisa,hata baadhi ya vyama unao.

Mfano: Komu na Kubenea waliitwa kutoa maelezo kidogo mbele ya kamati kuu ya chama chao.kitu ni kile kile sema scale ndio inabadilika kutoka chama kwenda jeshi LA polisi
 
Nawaunga mkono Magufuli anachapa kazi Sana udhaifu wa serikali yake upo kwenye utawala Bora
Nikiwa kama mwananchi,mwana CCM naomba Magufuli aliangalie Sana eneo hilo
Sasa mkuu kutawala si Ndo kazi yake kuu? Au ulimaanisha nn? Maana ni sawa na useme nimeajiri mhasibu anachapa kazi kweli Ila udhaifu wa utendaji wake upo kwenye shughuli za kihasibu.
 
Hawa nao are less informed of what is taking place here. Hakuna cha kupambana na rushwa. Anawafanyia visa asiowataka lakini walio wake kama akina makonda wanapeta na rushwa. ...

Selective prosectuion ndiyo iliyopo hapa na si kupambana na rushwa.
 
Hawa nao are less informed of what is taking place here. hakuna cha kupambana na rushwa. Anawafanyia visa asiowataka lakini walio wake kama akina makonda wanapeta na rushwa. ... selective prosectuion ndiyo iliyopo hapa na si kupambana na rushwa.
Makonda kala Rushwa gani?
 
Hizo asasi 18 zijicheki zikizidi kibelembele zitapata zinachokitafuta; kama umbeya umbeya zikafanyie kwenye nchi zingine; wewe ni nani kukosoma fikra wakati wanachi wapo sawa wanafurahia maendeleo.
 
Back
Top Bottom