Makaimati
JF-Expert Member
- Apr 4, 2011
- 462
- 87
Balozi Seif Iddi na Waziri Nahodha jibuni hoja hizi za Uamsho
May 18, 2011 by zanzibardaima
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu ya Zanzibar imetoa taarifa rasmi leo hii kuhusiana na masuala matatu makubwa yanayohusu hatima ya Zanzibar kwa sasa: kuchomwa kwa moto mabanda ya wafanyabiashara huko Pwani-Mchangani, mwenendo wa serikali ya Umoja ya Kitaifa na maoni ya Wazanzibari kuelekea Muungano. Hoja inayoibuliwa na Uamsho ni kuwa, pana upotoshaji mkubwa wa makusudi unafanywa na watu kuhusiana na hayo yote matatu, ambao ni mbaya kwa mustakabali wa Zanzibar. Zanzibar Daima inaichapisha taarifa hiyo kwa imani kwamba watu wanapaswa kuambiwa ukweli kuhusiana na masuala haya na kwamba hapa kuna wahusika wanaopasa kuwajibika.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 18/05/2011
Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehma. Rehma na amani zimshukie kipenzi chetu, Mtume Muhammad (S.A.W.) na ahli zake na jamaa zake na walio wema katika Uislamu.
Kutokana na matukio yaliyojitokeza katika nchi na ambayo yanaweza kuleta mgawanyiko na chuki na kuiingiza katika mgogoro usio wa lazima, Jumuiya ya UAMSHO imeona nayo ichukuwe nafasi kuelezea uoni wake juu ya hayo yaliyojiri.
Kimsingi, kuna matukio matatu yaliyotokea Zanzibar ambayo sasa yanaonekana kuwa gumzo Zanzibar na Bara: kwanza, suala la kuchomwa moto kwa mabanda ya biashara huko Pwani Mchangani; pili, suala la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya mfumo wa Umoja wa Kitaifa na, tatu, maoni ya Zanzibar kuhusu Mswada wa Mapendekezo ya Marekebisho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. TUKIO LA PWANI MCHANGANI
Suala la tukio la Pwani Mchangani la kuchomwa moto mabanda ya wafanyabiashara linapotoshwa kwa makusudi na watu wasioitakia kheri Zanzibar.
Kwanza, si kweli kama mabanda hayo yaliyochomwa ni 70 kama livyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, idadi halisi ni 29.
Pili, wamiliki wa mabanda hayo si Wabara kama inavyoelezwa. Ukweli ni kuwa 27 kati yao ni ya Wazanzibari na mawili tu ndio ya Wabara.
Tatu, si kweli kuwa tukio hilo ni la kisiasa, bali ni la kijamii, baada ya malalamiko ya wananchi kulalamika kutokana na vitendo vya ubakaji, umalaya, ulevi, mauaji na biashara ya unga katika eneo hilo.
Nne, si kweli kwamba tukio hili linahusiana na suala la kuvunja Muungano, kwani baada ya malalamiko hayo na kuthibitishwa na vyombo husika, serikali za mitaa ziliwataka wafanya biashara hao kuondoka katika eneo hilo ifikapo tarehe 01/05/2011. Sasa je, serekali za mitaa zilitaka kuuvunja Muungano?
Tano, si kweli kuwa Wabara wanafukuzwa au kunyanyaswa Zanzibar. Ukweli ni kuwa wapo wafanyabiashara wengi katika maeneo mengi ya Zanzibar, ukiwemo Mji Mkongwe, Marikiti Kuu Darajani wakifanya shughuli mbalimbali, zikiwemo kuuza njugu, matunda na bidhaa nyengine za mikononi mitaani mwetu, na kuna wanaofanya kazi za kulima mashambani. Mbona hawa hawajabughudhiwa? Jibu ni kuwa hawajafanya vitendo au biashara za uhuni, unga, ulevi, n.k.
Hata ile hoja kuwa eti Wazanzibari wapo kila sehemu Bara, lakini hawabughudhiwi, haina mashiko. Maana suali ni Wazanzibari gani wanaofanya biashara ya ulevi, unga, ubakaji, ukahaba, halafu serikali ikawaachia kwa kisingizio cha Muungano?
Sita na mwisho kuhusiana na hili, maswali ya nani amechoma na kwa nini amefanya hivyo yako mahakamini. Ni busara kuiwachia mahakama iamuwe kwa mujibu wa sheria.
Masikitiko yetu makubwa na yenye masuala mengi bila jawabu, ni kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, kukurupaka na kusema kuwa hawa waliochoma ni wahalifu, wanataka kuvunja Muungano na yeye, kama waziri, atahakikisha waliohusika wanachukuliwa hatua. Sasa suala kuhusu hawa wafanyabiashara kharamu, ambao wanachi na vyombo vya serikali vimeamua wahame, mbona hawahakutaja sababu zilizopelekea kupewa amri ya kuhama?
Kauli za Mhe. Nahodha zimewachukiza Waislamu na Wazanzibari na wameanza kumtafsiri kuwa naye ni miongoni mwa wasioitakia mema Zanzibar.
Tunawasihi Waislamu na wananchi kwa jumla kutokubali, katika kipindi hichi, kupokea fitna za kutaka kuwagawa na kupandikiza chuki baina yetu.
Pia tunaiomba serikali kuchukuwa khatua zinazofaa kwa gazeti la NIPE HABARI kutokana na taarifa zake za kuhatarisha amani ya nchi za tarehe 13-19 Mei 2011, kama habari iliyopewa nafasi ya mbele UZANZIBARI, UZANZIBARA SASA WANUKIA ZANZIBAR. Ni taarifa zinazo weza kulitia taifa katika khatari ya vita vya kikabila na kidini.
2. SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR CHINI MFUMO WA UMOJA WA KITAIFA
Kumeanza kujitokeza watu kutaka kujenga fitna ili Wazanzibari waanze chuki na viongozi wao na kuidhoofisha serikali na kuirejesha nchi ya Zanzibar katika matatizo yale ya nyuma.
Kidogo tukumbushe angalau watu wajielewe tunapotoka na tulipo sasa: Kwa miaka 46, kuanzia 1961 hadi 2005, Zanzibar imeshaingia katika chaguzi sita zinazohusisha vyama vingi vya siasa, lakini matokeo ya chaguzi zote hizo ni kudhalilika kwa Waislamu, dini yao na utamaduni wao. Hakuna uchaguzi wowote wa vyama vingi ambao umepita Zanzibar bila ya kuwacha athari mbaya kwa Wazanzibari. Matokeo yake ni kuwa kila uchaguzi mmoja unapofanyika, huwa msingi umechimbwa kwa jengo la mateso na mfarakano kwa uchaguzi ujao.
Kwa mfano, chuki ya utumwa na ubwana, na Uarabu na Uafrika iliyopandikizwa kwa makusudi katika uchaguzi wa pili wa Juni 1961, ilipelekea Waislamu zaidi ya 70 kuuliwa huku watoto wa Kiislamu katika kijiji cha Bambi, wakiteketezwa kwa moto.
Uchaguzi wa 1995 uliofanyika baada ya miaka zaidi ya 30 tangu Mapinduzi ya 1964 na kufutwa kwa vyama vingi, haukupunguza chochote katika madhila ya Waislamu wa Zanzibar, isipokuwa kuongeza.fitna ya Upemba na Uunguja iliyopaliliwa na taasisi za dola na matokeo yake yakawa ni kuwafanya Waislamu wa nchi hii waangaliane kwa misingi ya maeneo wanayotoka, na sio kwa Mungu Mmoja wa Haki wanayemuuamini na kumuuabudu. Badala ya kusimama na kalima tukufu ya "Laa Ilaah Illallah, Muhamadarasuulullah", Waislamu wa Zanzibar wakawa wanasimama na kauli za Upemba na Uunguja, Uarabu na Uafrika na ubwana na utumwa!
Chaguzi za mwaka 2000 na 2005 mambo yakawa ni yale yale. Tena majeshi yakamwagwa mitaani yakiwa na silaha za kivita. Rais wa wakati huo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, Benjamin Mkapa, alipoulizwa na waandishi wa habari sababu za kupeleka majeshi na vifaru Zanzibar, naye aliwauliza kulikuwa na sababu gani kwa Wamarekani kupeleka wanajeshi Iraq!
Kwa hivyo, nchi ya Waislamu ya Zanzibar ikawa imevamiwa na majeshi ya kigeni kama vile Iraq ilivyokuwa imevamiwa na Marekani. Matokeo yake ikawa ni muendelezo wa kile Rais Jakaya Kikwete alichokuja kukiita "mpasuko" wa Zanzibar.
Hata baada ya matokeo ya chaguzi hizo na matokeo kutangazwa, Waislamu wakawa wakifuatwa majumbani na misikitini kupigwa na kudhalilishwa kupita kiasi. Matokeo yake, makundi ya vijana wa Kiislamu
wakaanza kuhama visiwa hivi na kukimbilia ughaibuni, ambako wameselelea hadi leo. Miongoni mwa athari za vijana hao wa Kiislamu wa Kizanzibari kuselelea ugenini, ni kupoteza maadili ya dini yao na hivyo kuudhoofisha Uislamu.
Kwetu sisi, huu ni mpasuko baina ya Waislamu ambao mashiko yake hayako katika Uislamu lakini ambao athari zake zinawapata Waislamu wa Zanzibar. Tunaamini kwamba Zanzibar inapigwa vita kwa sababu ya Uislamu wake.
Tukumbuke kulijitokeza taasisi za kigeni Jumuiya ya Madola na pia kamati ya vyama vya siasa vyote vilishindwa kuziba mpasuko huo. Hii imetokana na kuwa wengine hawakuwa na nia nzuri na Zanzibar.
Baada ya madhara yote haya, ambayo yamegharimu maisha ya watu, mali kupotea na mateso ya kila aina, Wazanzibari wenyewe wenye uchungu na nchi yao, wakaona huku inakoelekea Zanzibar ni kubaya na wa kuionea huruma Zanzibar ni Wazanzibari wenyewe.
Mhe. Amani Karume na Mhe. Maalim Seif wakaamua kuzika yale yote tuliyoyaeleza kwa ufupi. Yakaja Maridhiano, na nia ni kujenga Zanzibar mpya yenye amani utulivu umoja na maendeleo. Sote tukakubali kufuta tafauti zetu na kujenga umoja na tukaahidi kushirikiana na viongozi kujenga Zanzibar mpya yenye maendeleo. Na hilo litafanikiwa kwa kuwepo serikali ya umoja, wengi wa Wazanzibari wakawafiki hilo.
Sasa matunda ya Maridhiano tumeanza kuyaona katika Uchaguzi Mkuu 2010, namna ya amani utulivu ulivyotawala. Hata baada ya matokeo, Wazanzibari wote walisherehekea kwa pamoja. Hakuna aliyepingwa, kubakwa, kuuliwa wala kuharibiwa mali. Haya ndio maamuzi ya Wazanzibari.
Sasa kumeanza kujitokeza watu kutaka kuidhoofisha juhudi hii yote, kwa kisingizio cha kuwa serikali iliyopo haina la maana. Wameanza kuwakashifu viongozi wa juu kuwa waregevu. Hawa tunawahisabu ni maadui wa Zanzibar. Na upo wasisiwasi kuwa baadhi ya viongozi wa Bara hawakupendezewa na hali hii, na wengine wakataka kuwafurahisha kwa vitendo na kauli ili waonekane wao wema.au bora kuliko wengine.
Na hii imetutia wasiwasi zaidi baada ya Afisa wa Ubalozi wa Marekani aliyeko Zanzibar, kuanza kupita kuhoji watu kuhusu uwoni juu ya serikali na tukio la Pwani Mchangani. Hatua ya afisa huyu inaweza kusababisha mgawanyiko. Tuko macho na hatua za ya afisa huyo na tukibaini kuna uchochezi au fitna hatutoweza kumvumlia.
Tunatamka wazi, hatuko tayari kumnyamazia kiongozi au yoyote awe wa nje au ndani kutaka kuleta fitna na mgawanyiko miongini mwetu.
Suala la ugumu wa maisha na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu, serikali inalielewa na tunaamini Rais wa Zanzibar na Baraza lake wako makini kulitafutia ufumbuzi, huku tukiamini mabadiliko yatapatikana.
Si kweli kwamba serikali haina la maana inalofanya. Wanaosema hivyo wanataka kujenga fitna kwa Wazanzibari waanze kuichukia serikali yao. Tunasema nafasi hiyo haipo tena Zanzibar. Wito wetu kwa Wazanzibari ni kuwa tuwe macho na maadui!
3. MUUNGANO
Kumekuwa na kauli nyingi tokea Kamati ya Bunge kuja Zanzibar kukusanya maoni kuhusu Rasimu ya Marekebisho ya Katiba na Wazanzibari wakaonesha msimamo wao kuhusu mustakbali wa nchi yao kwa kuukataa katakata mswada huo.
Imekuwa ni kosa mpaka viongozi wa Dini wakaitwa wahuni. Mengi yamesemwa na hoja mbali mbali zinatolewa kulazimisha Wazanzibari kuukubali Muungano. Tunasema, miaka 47 ya kudumu kwa Muungano ni kwa heshima na ustahamilivu wa Wazanzibari. Na kwa muda wote wamezibwa watu midomo kuhoji au kukosowa kuhusu Muungano. Tunasema karne hizo zimekwisha.
Muungano huu tokea kuundwa kwake umekuwa na kasoro nyingi na kuundiwa tume 21 na bado kasoro zipo pale pale.
Nasaha zetu ni kuwa iko haja kujadiliwa upya Muungano na pande zote mbili; na kushauriwa Watanganyika na Wazanzibari kuhusu mfumo wa Muungano wanaoutaka. Kinyume na hivyo kunaweza kukazuka mgogoro mkubwa na unaoweza kuleta uvunjifu wa amani
MWISHO
Tunatowa wito kwa serikali ya Zanzibar kulitatuwa tatizo la wafanyabiashara wa Jua Kali ambao kwa muda wa miezi minne sasa maduka yao yamefungwa. Ingawa shauri lao lipo mahakamani, serikali ifikirie njia ya kuwaokowa wafanyabiashara hao ili kuondosha dhana potofu na maadui wakapata njia ya kuitia sumu jamii.
May 18, 2011 by zanzibardaima
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu ya Zanzibar imetoa taarifa rasmi leo hii kuhusiana na masuala matatu makubwa yanayohusu hatima ya Zanzibar kwa sasa: kuchomwa kwa moto mabanda ya wafanyabiashara huko Pwani-Mchangani, mwenendo wa serikali ya Umoja ya Kitaifa na maoni ya Wazanzibari kuelekea Muungano. Hoja inayoibuliwa na Uamsho ni kuwa, pana upotoshaji mkubwa wa makusudi unafanywa na watu kuhusiana na hayo yote matatu, ambao ni mbaya kwa mustakabali wa Zanzibar. Zanzibar Daima inaichapisha taarifa hiyo kwa imani kwamba watu wanapaswa kuambiwa ukweli kuhusiana na masuala haya na kwamba hapa kuna wahusika wanaopasa kuwajibika.
JUMUIYA YA UAMSHO NA MIHADHARA YA KIISLAMU
للجنة الدعوة الإسلامية
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 18/05/2011
Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehma. Rehma na amani zimshukie kipenzi chetu, Mtume Muhammad (S.A.W.) na ahli zake na jamaa zake na walio wema katika Uislamu.
Kutokana na matukio yaliyojitokeza katika nchi na ambayo yanaweza kuleta mgawanyiko na chuki na kuiingiza katika mgogoro usio wa lazima, Jumuiya ya UAMSHO imeona nayo ichukuwe nafasi kuelezea uoni wake juu ya hayo yaliyojiri.
Kimsingi, kuna matukio matatu yaliyotokea Zanzibar ambayo sasa yanaonekana kuwa gumzo Zanzibar na Bara: kwanza, suala la kuchomwa moto kwa mabanda ya biashara huko Pwani Mchangani; pili, suala la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya mfumo wa Umoja wa Kitaifa na, tatu, maoni ya Zanzibar kuhusu Mswada wa Mapendekezo ya Marekebisho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. TUKIO LA PWANI MCHANGANI
Suala la tukio la Pwani Mchangani la kuchomwa moto mabanda ya wafanyabiashara linapotoshwa kwa makusudi na watu wasioitakia kheri Zanzibar.
Kwanza, si kweli kama mabanda hayo yaliyochomwa ni 70 kama livyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari, idadi halisi ni 29.
Pili, wamiliki wa mabanda hayo si Wabara kama inavyoelezwa. Ukweli ni kuwa 27 kati yao ni ya Wazanzibari na mawili tu ndio ya Wabara.
Tatu, si kweli kuwa tukio hilo ni la kisiasa, bali ni la kijamii, baada ya malalamiko ya wananchi kulalamika kutokana na vitendo vya ubakaji, umalaya, ulevi, mauaji na biashara ya unga katika eneo hilo.
Nne, si kweli kwamba tukio hili linahusiana na suala la kuvunja Muungano, kwani baada ya malalamiko hayo na kuthibitishwa na vyombo husika, serikali za mitaa ziliwataka wafanya biashara hao kuondoka katika eneo hilo ifikapo tarehe 01/05/2011. Sasa je, serekali za mitaa zilitaka kuuvunja Muungano?
Tano, si kweli kuwa Wabara wanafukuzwa au kunyanyaswa Zanzibar. Ukweli ni kuwa wapo wafanyabiashara wengi katika maeneo mengi ya Zanzibar, ukiwemo Mji Mkongwe, Marikiti Kuu Darajani wakifanya shughuli mbalimbali, zikiwemo kuuza njugu, matunda na bidhaa nyengine za mikononi mitaani mwetu, na kuna wanaofanya kazi za kulima mashambani. Mbona hawa hawajabughudhiwa? Jibu ni kuwa hawajafanya vitendo au biashara za uhuni, unga, ulevi, n.k.
Hata ile hoja kuwa eti Wazanzibari wapo kila sehemu Bara, lakini hawabughudhiwi, haina mashiko. Maana suali ni Wazanzibari gani wanaofanya biashara ya ulevi, unga, ubakaji, ukahaba, halafu serikali ikawaachia kwa kisingizio cha Muungano?
Sita na mwisho kuhusiana na hili, maswali ya nani amechoma na kwa nini amefanya hivyo yako mahakamini. Ni busara kuiwachia mahakama iamuwe kwa mujibu wa sheria.
Masikitiko yetu makubwa na yenye masuala mengi bila jawabu, ni kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, kukurupaka na kusema kuwa hawa waliochoma ni wahalifu, wanataka kuvunja Muungano na yeye, kama waziri, atahakikisha waliohusika wanachukuliwa hatua. Sasa suala kuhusu hawa wafanyabiashara kharamu, ambao wanachi na vyombo vya serikali vimeamua wahame, mbona hawahakutaja sababu zilizopelekea kupewa amri ya kuhama?
Kauli za Mhe. Nahodha zimewachukiza Waislamu na Wazanzibari na wameanza kumtafsiri kuwa naye ni miongoni mwa wasioitakia mema Zanzibar.
Tunawasihi Waislamu na wananchi kwa jumla kutokubali, katika kipindi hichi, kupokea fitna za kutaka kuwagawa na kupandikiza chuki baina yetu.
Pia tunaiomba serikali kuchukuwa khatua zinazofaa kwa gazeti la NIPE HABARI kutokana na taarifa zake za kuhatarisha amani ya nchi za tarehe 13-19 Mei 2011, kama habari iliyopewa nafasi ya mbele UZANZIBARI, UZANZIBARA SASA WANUKIA ZANZIBAR. Ni taarifa zinazo weza kulitia taifa katika khatari ya vita vya kikabila na kidini.
2. SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR CHINI MFUMO WA UMOJA WA KITAIFA
Kumeanza kujitokeza watu kutaka kujenga fitna ili Wazanzibari waanze chuki na viongozi wao na kuidhoofisha serikali na kuirejesha nchi ya Zanzibar katika matatizo yale ya nyuma.
Kidogo tukumbushe angalau watu wajielewe tunapotoka na tulipo sasa: Kwa miaka 46, kuanzia 1961 hadi 2005, Zanzibar imeshaingia katika chaguzi sita zinazohusisha vyama vingi vya siasa, lakini matokeo ya chaguzi zote hizo ni kudhalilika kwa Waislamu, dini yao na utamaduni wao. Hakuna uchaguzi wowote wa vyama vingi ambao umepita Zanzibar bila ya kuwacha athari mbaya kwa Wazanzibari. Matokeo yake ni kuwa kila uchaguzi mmoja unapofanyika, huwa msingi umechimbwa kwa jengo la mateso na mfarakano kwa uchaguzi ujao.
Kwa mfano, chuki ya utumwa na ubwana, na Uarabu na Uafrika iliyopandikizwa kwa makusudi katika uchaguzi wa pili wa Juni 1961, ilipelekea Waislamu zaidi ya 70 kuuliwa huku watoto wa Kiislamu katika kijiji cha Bambi, wakiteketezwa kwa moto.
Uchaguzi wa 1995 uliofanyika baada ya miaka zaidi ya 30 tangu Mapinduzi ya 1964 na kufutwa kwa vyama vingi, haukupunguza chochote katika madhila ya Waislamu wa Zanzibar, isipokuwa kuongeza.fitna ya Upemba na Uunguja iliyopaliliwa na taasisi za dola na matokeo yake yakawa ni kuwafanya Waislamu wa nchi hii waangaliane kwa misingi ya maeneo wanayotoka, na sio kwa Mungu Mmoja wa Haki wanayemuuamini na kumuuabudu. Badala ya kusimama na kalima tukufu ya "Laa Ilaah Illallah, Muhamadarasuulullah", Waislamu wa Zanzibar wakawa wanasimama na kauli za Upemba na Uunguja, Uarabu na Uafrika na ubwana na utumwa!
Chaguzi za mwaka 2000 na 2005 mambo yakawa ni yale yale. Tena majeshi yakamwagwa mitaani yakiwa na silaha za kivita. Rais wa wakati huo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, Benjamin Mkapa, alipoulizwa na waandishi wa habari sababu za kupeleka majeshi na vifaru Zanzibar, naye aliwauliza kulikuwa na sababu gani kwa Wamarekani kupeleka wanajeshi Iraq!
Kwa hivyo, nchi ya Waislamu ya Zanzibar ikawa imevamiwa na majeshi ya kigeni kama vile Iraq ilivyokuwa imevamiwa na Marekani. Matokeo yake ikawa ni muendelezo wa kile Rais Jakaya Kikwete alichokuja kukiita "mpasuko" wa Zanzibar.
Hata baada ya matokeo ya chaguzi hizo na matokeo kutangazwa, Waislamu wakawa wakifuatwa majumbani na misikitini kupigwa na kudhalilishwa kupita kiasi. Matokeo yake, makundi ya vijana wa Kiislamu
wakaanza kuhama visiwa hivi na kukimbilia ughaibuni, ambako wameselelea hadi leo. Miongoni mwa athari za vijana hao wa Kiislamu wa Kizanzibari kuselelea ugenini, ni kupoteza maadili ya dini yao na hivyo kuudhoofisha Uislamu.
Kwetu sisi, huu ni mpasuko baina ya Waislamu ambao mashiko yake hayako katika Uislamu lakini ambao athari zake zinawapata Waislamu wa Zanzibar. Tunaamini kwamba Zanzibar inapigwa vita kwa sababu ya Uislamu wake.
Tukumbuke kulijitokeza taasisi za kigeni Jumuiya ya Madola na pia kamati ya vyama vya siasa vyote vilishindwa kuziba mpasuko huo. Hii imetokana na kuwa wengine hawakuwa na nia nzuri na Zanzibar.
Baada ya madhara yote haya, ambayo yamegharimu maisha ya watu, mali kupotea na mateso ya kila aina, Wazanzibari wenyewe wenye uchungu na nchi yao, wakaona huku inakoelekea Zanzibar ni kubaya na wa kuionea huruma Zanzibar ni Wazanzibari wenyewe.
Mhe. Amani Karume na Mhe. Maalim Seif wakaamua kuzika yale yote tuliyoyaeleza kwa ufupi. Yakaja Maridhiano, na nia ni kujenga Zanzibar mpya yenye amani utulivu umoja na maendeleo. Sote tukakubali kufuta tafauti zetu na kujenga umoja na tukaahidi kushirikiana na viongozi kujenga Zanzibar mpya yenye maendeleo. Na hilo litafanikiwa kwa kuwepo serikali ya umoja, wengi wa Wazanzibari wakawafiki hilo.
Sasa matunda ya Maridhiano tumeanza kuyaona katika Uchaguzi Mkuu 2010, namna ya amani utulivu ulivyotawala. Hata baada ya matokeo, Wazanzibari wote walisherehekea kwa pamoja. Hakuna aliyepingwa, kubakwa, kuuliwa wala kuharibiwa mali. Haya ndio maamuzi ya Wazanzibari.
Sasa kumeanza kujitokeza watu kutaka kuidhoofisha juhudi hii yote, kwa kisingizio cha kuwa serikali iliyopo haina la maana. Wameanza kuwakashifu viongozi wa juu kuwa waregevu. Hawa tunawahisabu ni maadui wa Zanzibar. Na upo wasisiwasi kuwa baadhi ya viongozi wa Bara hawakupendezewa na hali hii, na wengine wakataka kuwafurahisha kwa vitendo na kauli ili waonekane wao wema.au bora kuliko wengine.
Na hii imetutia wasiwasi zaidi baada ya Afisa wa Ubalozi wa Marekani aliyeko Zanzibar, kuanza kupita kuhoji watu kuhusu uwoni juu ya serikali na tukio la Pwani Mchangani. Hatua ya afisa huyu inaweza kusababisha mgawanyiko. Tuko macho na hatua za ya afisa huyo na tukibaini kuna uchochezi au fitna hatutoweza kumvumlia.
Tunatamka wazi, hatuko tayari kumnyamazia kiongozi au yoyote awe wa nje au ndani kutaka kuleta fitna na mgawanyiko miongini mwetu.
Suala la ugumu wa maisha na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu, serikali inalielewa na tunaamini Rais wa Zanzibar na Baraza lake wako makini kulitafutia ufumbuzi, huku tukiamini mabadiliko yatapatikana.
Si kweli kwamba serikali haina la maana inalofanya. Wanaosema hivyo wanataka kujenga fitna kwa Wazanzibari waanze kuichukia serikali yao. Tunasema nafasi hiyo haipo tena Zanzibar. Wito wetu kwa Wazanzibari ni kuwa tuwe macho na maadui!
3. MUUNGANO
Kumekuwa na kauli nyingi tokea Kamati ya Bunge kuja Zanzibar kukusanya maoni kuhusu Rasimu ya Marekebisho ya Katiba na Wazanzibari wakaonesha msimamo wao kuhusu mustakbali wa nchi yao kwa kuukataa katakata mswada huo.
Imekuwa ni kosa mpaka viongozi wa Dini wakaitwa wahuni. Mengi yamesemwa na hoja mbali mbali zinatolewa kulazimisha Wazanzibari kuukubali Muungano. Tunasema, miaka 47 ya kudumu kwa Muungano ni kwa heshima na ustahamilivu wa Wazanzibari. Na kwa muda wote wamezibwa watu midomo kuhoji au kukosowa kuhusu Muungano. Tunasema karne hizo zimekwisha.
Muungano huu tokea kuundwa kwake umekuwa na kasoro nyingi na kuundiwa tume 21 na bado kasoro zipo pale pale.
Nasaha zetu ni kuwa iko haja kujadiliwa upya Muungano na pande zote mbili; na kushauriwa Watanganyika na Wazanzibari kuhusu mfumo wa Muungano wanaoutaka. Kinyume na hivyo kunaweza kukazuka mgogoro mkubwa na unaoweza kuleta uvunjifu wa amani
MWISHO
Tunatowa wito kwa serikali ya Zanzibar kulitatuwa tatizo la wafanyabiashara wa Jua Kali ambao kwa muda wa miezi minne sasa maduka yao yamefungwa. Ingawa shauri lao lipo mahakamani, serikali ifikirie njia ya kuwaokowa wafanyabiashara hao ili kuondosha dhana potofu na maadui wakapata njia ya kuitia sumu jamii.
WABILAH TAUFIQ
AZZAN KHALID HAMDAN
NAIBU AMIRI (JUMIKI)
NAIBU AMIRI (JUMIKI)