Balaa lingine lamwangukia Dr Slaa

Hivi hawa majamaa wa chama cha mafisadi wanadhani akili za watz ni kama zao? Ivi kuna sehemu yoyote fisadi kijana Nape Nauye ametaja popote kuwa mafisadi wamekuja cdm au kwa dr.slaa? Au kasema tu kwa mafumbo ya kitoto kuwa wanatumia wapinzani,au tukitaja wapinzani kashaga anaelewa ni dr Slaa na cdm tu?

Vile vyama popo havijui? Mfano kuna prof. anazunguka mikoa ya pwani akidai kuwa CDM nao ni mafisadi, waache kumkimbiza JK labda anafadhiliwa na hao mafisadi maana hata uyo juu yuko kwenye list of shame!

Kashaga kwa ubongo wako huo huo ufikirii kuwa ni ushindi mkubwa kwa dr.Slaa kama mafisadi wakubwa wamejisalimisha kwake na kuomba awasaidie kuwanasa hata wale maFisadi papa waliotaka wenzio wavue magamba,hapa yupo mangula,jk et all,sasa kuna tatizo gani kama RA, EL, CHENGE, et all wamejisalimisha kwa rais wa wananchi asiye ikulu? Mtakoma.

Nape anasema mafisadi wamekimbilia upinzani, mwambie ataje nani na nani Dr. Slaa kawapokea, tofauti na yule msafiri aliyesema CCM safiii! Chenge safiii! RA safiii! JK safiii! Leo hili wanaanza RA chafuuuuu! EL chafuuuuu! Chenge chafuuuuu!

Kwa upumbavu huu na upopo mtz gani atawakubali? Nadhani CCM mmefikia stage moja inaitwa dissolution and winding up of the partnership/CCM, cjui nani ataondoka na nini! Kashaga usicheze mbali, unga robo. Unaweza ukaambulia hata kalenda za ukutani pale Lumumba!!
 
Tambwe hiza ndo nani naona ametajwa humu tafadhali tufahamishwe tumjue ni nani na ana mchango gani katika kulinda mafisadi!
 
Propaganda tu hizi. Na hii ni style ya zamani sana ya siasa. Siku hizi wananchi wengi wanaelewa pumba na mchele.
 
Kwanza huyu jamaa tangu jana naona tunampa promo,cha muhmu tumwacheni aandike thread then achangie mwenyewe au yeye na wapuuzi wenzake
"wapuuzi"kama anavyopenda kulitumia speaker wao.
 
kweli CCM wameishiwa,,,, hata mseme nini this time tunawachana, mnafanya nchi yenu hii sio wakati yetu sote
 
kashaga........nimesoma post yako, lakini balaa mbona sijaiona? au unafail kutafuta heading / title inayofanana na content.
 
Stukeni watu...Jamaawa Magamba ndo washaingia kazini hivyo!...
Watakuwa wakiposti vitu vya kipumbavu kama hivi ili kuondoa attention kwenye MAGAMBA YAO!
Say NO to this crap men!
 
Sijuti Nape kupigwa chini katika Ubunge wa Ubungo....he was a wrong choice.Maskini Nape.Amewekwa hapo kueneza pumba kama hizo kweli?
 
Kwani slaa kutumiwa ni ajabu? Nape atakuwa ana data ndio maana kamtaja kibaraka wa mafisadi. Slaa
 
Naona NAPE ameanza kulewa madaraka aliopewa kajisahau alivyofanyiwa akiwa UVCCM????

Kweli Maskini akipata......... ss NAPE amepata......!!
 
Hili mbona sio balaa kaka hebu tuipe hadhi forum kwa kuandika vitu vya maana jamani...!!!

Balaa lingine limemwangukia katibu mkuu wa chama cha CHADEMA,baada ya kutuhumiwa na chama cha mapinduzi kuwa anatumika na mafisadi,hii inaweza chukuliwa kirahisi lakini ni swala nyeti ikizingatiwa Slaa amekuwa akijifanya kuwa mstari wa mbele kupambana na mafisadi,Slaa hana budi kukanusha hizi tuhuma au kutoa maelezo ya kujitosheleza kwasababu kukaa kimya inaweza kuleta tasfiri tofauti kwa wafuasi wake( silence means yes)

HABARI KAMILI
CHAMA Cha Mapinduzi kimesema Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa na chama chake, wanatumiwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi waliotakiwa kujiuzulu wenyewe ndani ya chama hicho.

Akihutubia umati wa watu katika viwanja vya Mwembe-Kisonge Zanzibar, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema kwa sasa watuhumiwa hao wameamua kutumia baadhi ya vyama vya siasa, magazeti na asasi za dini kujibu mapigo.

“Tumewapa miezi mitatu watuhumiwa wote wa ufisadi katika chama chetu wajiondoe wenyewe. Baadhi wanajaribu kupinga na kujibu mapigo kwa kutumia magazeti, vyama vya siasa na taasisi za dini...tunajua tutashinda na wao lazima waondoke,” alisema Nnauye.

Alisema, “Tumeandaa mkakati wa kusafisha chama kutoka ngazi za chini mpaka katika ngazi ya Taifa. Tumechunguza na tunajua wanaotakiwa kuondoka ndani ya chama chetu. Lakini baadhi ya watu wamejitokeza kutaja majina ya watuhumiwa ndani ya chama chetu, hiyo si kazi yao.”
 
Balaa lingine limemwangukia katibu mkuu wa chama cha CHADEMA,baada ya kutuhumiwa na chama cha mapinduzi kuwa anatumika na mafisadi,hii inaweza chukuliwa kirahisi lakini ni swala nyeti ikizingatiwa Slaa amekuwa akijifanya kuwa mstari wa mbele kupambana na mafisadi,Slaa hana budi kukanusha hizi tuhuma au kutoa maelezo ya kujitosheleza kwasababu kukaa kimya inaweza kuleta tasfiri tofauti kwa wafuasi wake( silence means yes)

HABARI KAMILI
CHAMA Cha Mapinduzi kimesema Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa na chama chake, wanatumiwa na baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi waliotakiwa kujiuzulu wenyewe ndani ya chama hicho.

Akihutubia umati wa watu katika viwanja vya Mwembe-Kisonge Zanzibar, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema kwa sasa watuhumiwa hao wameamua kutumia baadhi ya vyama vya siasa, magazeti na asasi za dini kujibu mapigo.

“Tumewapa miezi mitatu watuhumiwa wote wa ufisadi katika chama chetu wajiondoe wenyewe. Baadhi wanajaribu kupinga na kujibu mapigo kwa kutumia magazeti, vyama vya siasa na taasisi za dini...tunajua tutashinda na wao lazima waondoke,” alisema Nnauye.

Alisema, “Tumeandaa mkakati wa kusafisha chama kutoka ngazi za chini mpaka katika ngazi ya Taifa. Tumechunguza na tunajua wanaotakiwa kuondoka ndani ya chama chetu. Lakini baadhi ya watu wamejitokeza kutaja majina ya watuhumiwa ndani ya chama chetu, hiyo si kazi yao.”

Kazi kweli kweli, hivi kumbe hata kamati kuu na skretarieti mpya, hawana hoja bado, sorry for them, watuhumiwa wote wa ufisadii anasafishwa wanaweza kuana na top 5 in the list of shame?!!
 
C C M =Chama Cha Mafisadi aka Chama Cha Majambazi aka Chama Cha Magamba aka Chama Cha Majuha aka Chama Cha Mataahira...........................
 
Back
Top Bottom