Si hii nchi haina dini kabisa?
Na vyombo vya dini vinatakiwa kuwa huru kabisa?
Sasa Rais anakwenda kwenye baraza la Iddi anatoa briefcase yenye pesa taslimu...why? kuna nini?
Sasa mkuu wa mkoa anakuja na mradi wa kujenga makao makuu ya BAKWATA.Mradi wa bilioni 5.....
Je, haya yote yanafanyika kwa mapenzi mema au kuna kitu?
Hiko kitu ni nini hasa?
Serikali inajaribu ku achieve nini kwa 'kuisaidia huku' BAKWATA?
Uhuru wa BAKWATA kuikosoa na kuikemea serikali kama zilivyo taasisi zingine za dini ndo 'umeshakwenda'?
Nani muathirika wa haya yoote?
The Boss iko hivi,
Bwana mkubwa ni mkatoliki na alionesha hilo dhahiri siku ya ijumaa kuu kwa kwenda kubusu msalaba pale saint Peters,
Hii nini maana yake? Kwa Wakatoliki hawana tatizo lolote na utawala huu, kondoo wao ndio yuko kwenye usukani.
Bwana mtukufu akatoka hapo akaibukia Lutheran kwenye ibada ilikuwa ni timing agongane na Laigwani pale lakini timing ilikuwa mbovu.
Hakuishia hapo akaibukia kwa Mzee wa upako ukiangalia vizuri ziara hizi kwa upande wa makafiri deal done.
Akawageukiwa wenye deen ya haki with cash money ndani ya briefcase na kuwaahidi kuzirudisha mali za wakfu za waislamu.....
Leo Makondeko kijana wa nyumbani Kawekamo anakaa na Bakwata kuwawezesha ujenzi wa ofisi.
Mmekwisha, ukimya wa kina Deus Kibamba na taasisi zote zenye kelele ukitaka kupata jibu sahihi Google Mussolini halafu angalia utawala wake Italy ulifanikiwaje na wakati alikuwa Fashisti?
Jibu ni rahisi tu aliliweka mfukoni kanisa katoliki na kanisa kwa neema ilizomwagiwa na huyu fashisti Papa na makadinali wake wakavaa miwani ya mbao kama vile hawaoni nchi ilivyokuwa inaendeshwa, mapadre walilipwa mishahara na serikali ya Italy na kama haitoshi kanisa likapewa nchi yake ndani ya Rome, nchi hiyo inaitwa Vaticano.
Hili ndilo linakuja kutokea huku tusipokuwa makini, wanaanza taratibu tu hivihivi ila ikifika wanataka waungwe mkono hadi na maradical kama Mohamedi Said basi Waislamu watapewa mahakama ya kadhi na makadhi wataingizwa kwenye payroll ya serikali, hapo unakuwa umeshawatia mfukoni waislamu na kuwaziba mdomo.
Huwa sipati jibu mpaka leo chuo cha Tanesco kidato kilichokuwa kinazalisha wataalam wa umeme kupewa waislamu kana kwamba hii nchi wapagani hawana haki.
Tuendelee tu kupiga makofi muda utaongea.