Bakhresa anakwepa kodi?


Kwanini umtaje Bahkresa mkuu?
Kama kuna unalolijua kuhusu Bahkresa, ni vema ukakiweka wazi ili tupate pa-kuanzia kumjadili.
 
Swali la msingi sana.
...kwanini bakhresa hayupo kwenye orodha ya walipa kodi wakubwa ?

bakhresa ni group of companies, jumuisha kodi za kampuni zote kujua ukweli, vinginevyo yeye binafsi anaweza kuwa analipa p.a.y.e. kama mwajiriwa wa kampuni yake.
 
Bakhresa kwenye vitabu vyake vya hesabu anase anapata hasara! Hii nchi hii
 

kwa taarifa yako amna mfanyabiashara anayefanya biashara zake kwa uwazi kama bakhresa , hapata tanzania , biashara zake ziko wazi kabisa na ni rahisi mno kufuatilia , wafanyakazi wanalipwaje, kodi kiasi gani inalipwa ,njoo huku kwa MENGI vibarua wa kutosha , huku wakiingiza superprofi , . mengi ana campuni inaitwa tanzanite africa na kwa kwa makusudi kabisa AMEJIRENK kama mchinbaji mdogo ili asilipi kodi , kwanzia 2007
hadi hii leo anazalisha tone za tanzanite lakini anajificha nyuma ya wachimbaji wadogowadogo
 
Swali la msingi sana.
...kwanini bakhresa hayupo kwenye orodha ya walipa kodi wakubwa ?


mtaji wa biashara yake naskia et alipewa na rais mstaaf mzee ruksa mwinyi enzi zilee, so mwinyi nae ana hisa zake pale,,sijui kama watamgusa,
ila kinyume na hapo labda jamaa hayupo kwenye orodha hiyo labda analipa kodi stahiki ndo maana humuoni kwenye orodha ya wakwepa kodi
 
Bakhresa kwenye vitabu vyake vya hesabu anase anapata hasara! Hii nchi hii
Weka ushaidi wa hayo maneno yako badala ya kupambana na makampuni ya madini hayalipi kodi wewe unapambana na Bakhresa bila data zozote zaidi ya chuki zako tu.

Mitanzania bana.
 

Hapo kwenye PAYE makampuni mengi yanapiga pesa unaweza ukafanyakazi kwenye kampuni za wahidi unakatwa PAYE kumbe haiendi mpaka hata kwenye mifuko ya kijamii kuna makampuni hayapeleki....
 

ACHA UNAFIKI,BAKHRESA NI MLIPAJI KODI MKUU
i
 
Superman alileta thread mwaka jana, kuhusu walipaji kodi wakubwa


Mleta mada hebu tupe orodha ya hilo kundi LA walipa kodi wakubwa. Kama huna hiyo orodha basi haya yatakua majungu

Weka ushahidi wa ukwepaji kodi isije ikawa ni lako jambo! Mtu kuwa na biashara nyingi si kiashirizi za kukwepa kodi..
 
Last edited by a moderator:
Jackbauer naye alishawahi post hili.

 
Last edited by a moderator:
Walipa Kodi 15 Wakubwa Tanzania (Tanzania Top 15 Tax payers) & the missing household names
Posted by zittokabwe
Kutoka Hotuba ya Waziri Mkuu 26.08.2011 ? Makampuni yanayoogoza kwa kulipa kodi
Note: (Highlights)
Only one Mining company (the smallest ie Resolute Mining), only one telecom company(Airtel Tanzania).
Household names like MeTL, Bakhresa/Azam, IPP, VodaCom, Coca cola, Pepsi(SABCO), Serengeti Breweries, Barrick Gold, AngloGold Ashanti not seen. No oil marketing companies pia.
One can conclude that, TBL is the most profitable company in Tanzania, NMB is the most profitable Bank.
A public debate is needed.
Here under is the an extract from the Prime Minister speech;
Mheshimiwa Spika,
1. Nitumie nafasi hii kuwapongeza baadhi ya Walipakodi Wakubwa kwa Serikali na ambao wamefanya vizuri kati ya kipindi cha mwaka 2005 na 2011. Kwa kipindi hicho, Makampuni yaliyoongoza kwa kulipa kodi ni pamoja na:
i. Tanzania Breweries Ltd. (Shilingi Bilioni 165.4 );
ii. National Microfinance Bank (Shilingi Bilioni 108.6 );
iii. Tanzania Cigarette Company (Shilingi Bilioni 92.1 );
iv. National Bank of Commerce (Shilingi Bilioni 89.9 );
v. CRDB Bank Ltd. (Shilingi Bilioni 79.2 );
vi. Tanzania Ports Authority (Shilingi Bilioni 76.8 );
vii. Tanzania Portland Cement (Shilingi Bilioni 73.4 );
viii. Airtel (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 63.6 );
ix. Tanga Cement Company Ltd. (Shilingi Bilioni 43.6 );
x. Standard Chartered Bank Ltd. (Shilingi Bilioni 40.0 );
xi. Citibank (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 35.7 );
xii. Resolute (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 32.1 );
xiii. Tanzania International Container Terminal Services (Shilingi Bilioni 25.9 );
xiv. Tanzania Distillers Ltd. (Shilingi Bilioni 13.4 ); na
xv. Group Five International (PTY) Ltd. (Shilingi Bilioni 9.5 ).
2. Napenda kutoa rai kwa Makampuni yote Nchini kuiga mfano huu mzuri. Wito wangu kwa Makampuni, Wafanyabiashara Wakubwa kwa Wadogo na Wananchi wote ni kuongeza juhudi katika kufanya biashara zao ili zizalishe kwa wingi na kupata faida kubwa zaidi. Faida kubwa itachangia katika kuongeza Mapato ya Serikali kwa njia ya Kodi na hivyo kusaidia kukuza uchumi, kuongeza Pato la Taifa na la Mwananchi mmoja mmoja na kuondoa Umaskini. Niwadhihirishieni kwamba, Serikali inatambua umuhimu wao kwa maendeleo ya Nchi yetu na itahakikisha inaongeza juhudi zake za kuweka Mazingira Wezeshi kwa Makampuni hayo kufanya shughuli zao vizuri ili kuwezesha kulipa Kodi kwa mujibu wa Sheria.
Loading...
 
Jibu ni rahisi,tuache kutumia bidhaa za wakwepa kodi. Mimi naanza kwa baadhi ya bidhaa ya huyu Bakhresa
 
Weka ushahidi wa ukwepaji kodi isije ikawa ni lako jambo! Mtu kuwa na biashara nyingi si kiashirizi za kukwepa kodi..

TRA hutoa orodha ya walipa kodi wakubwa na kuwatunuku vyeti. Katika orodha ya makampuni 10 hakuna hata moja linalomilikiwa na Bakharesa!
Ajabu yeye yupo kwenye orodha ya matajiri wakubwa Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika!
Mbona Reginald Mengi anaezidiwa utajiri na huyu bwana yeye yupo kwenye orodha ya walipa kodi wakubwa???
(orodha ya walipa kodi mwaka juzi)
Kuna haja ya kumchunguza Bakhresa!
 
Bora useme achunguzwe kuliko kusema alipi kodi..
 
Kama hawalipi kodi nani analipa kodi ? wewe unalipa ngapi ?
Kulipa kodi sawa lakini kama ukomoe watu kwa kodi za TRA za kubambikiza kuna athari katika uzalishaji na bei ya bidhaa zitapanda na watu hawatakua na uwezo wa kununua hatimae viwanda vitakufa na kazi nazo zitakwenda arijojo.

kila mtu ana andika pumba zake humu kwa chuki za kijinga . serikali haina njia ya mapato zaidi ya kodi za wafanya biashara.Na cha kustajaabisha ni kuwa hizi choko choko zinaelekezwa kwa makampuni ya ndani ambayo yanalipa hio kodi ambayo serikali inajidai nayo. HAKUNA HATA MMOJA AMBAYE ANO ONGELEA SUALA MADINI NA KODI ZAKE.HAWA HAWALIPI kodi na wanasafirisha madini bila ya kufanyiwa audit. miaka 20 sasa na nchi haijafaidika chochote na secta ya madini.

kufukuza watu makini kama kina Rished Babde wa TRA kwa sababu za hisia wakati TRA imekusanya 97% ya malengo yake mpaka sasa hivi ni kukurupuka.
hayo makontena 300 yallopotea ni katika ripoti ya uchunguzi ya Barde na tayari alishachukua hatua za kuwafata wahusika. alishawaandikia barua ya kulipa kodi kwa macontena yao.
wengine waliyatoa kwa mashinikizo na maagizo lakini yeye kama kuchukua tahadhari aliweka rekodi na kuwaaindikia.

discpline ni muhimi katika sehemu za kazi pamoja na uadilifu lakini maamuzi ya pupa bila ya taarifa za uhakika juu ya chanzo cha haya ..sasa tuchukulie mfano yale makontena yalitoka kwa ajili ya kusaidia kampeni za ccm ? watu wataumbuana katika hili jambo.

tunahitaji sera ya uchumi , sera ya kuongeza uzalishaji na sera ya ajira. kuwabana wafanya biashara kwa makodi makubwa ndio chanzo cha kukwepa kodi ..kodi ni kubwa mno kiasi hata TRA wenyewe hawaelewi namna ya kuzitoza . Leo ukiagiza nondo basi mpaka imfikie mlaji itakua imetozwa kodi ya asilimia zaidi 60% ..TRA wanapata faida zaidi ya huyo muagiziaji na hata mwenye kiwanda huko uturuki.. biashara haziwezi kwenda namna hio....
 
kibaya zaidi huyu jamaa anauza mpaka maandazi na chapati zilizokua ziuzwe na mama ntilie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…