Poa poa kiongoziTuma ujumbe mfupi hapa 0758573660 au hapa 0624155629
Uliona mbali sana mkuu tayari mtunzi kashaanza kizingua.HATUTAKI RIWAYA ZENU MNAZOZIKATISHA KATIKAKATI. AMUENI MOJA KM MNAUZA AU MNATOA BURE
Sent using Jamii Forums mobile app
riwaya za magumashi mtu kama huwezi maliza hunahaja ya kuleta humuUliona mbali sana mkuu tayari mtunzi kashaanza kizingua.
MmhRIWAYA; BAHARIA
NAP; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA TANO
Mzee Mashimo alikodoa macho kwa kutoamini anachosikia kutoka kwa mkewe.
“Mke wangu unaanza kuchanganyikiwa kwa kifo hiki ngoja niite mchungaji ak..”
“Nipo mzima kabisa wala sijaugua na naomba tusitishe msiba huu Baba Msangu”
“Mama Msangu unakufuru sasa!” Mzee Mashimo aliwaka kwa hasira na kisha akatoka ndani na kuelekea nje bila kutia neno zaidi na aliona kama mkewe ameanza kuchanganyikiwa na msiba ule.
Maongezi yao yalikuwa yanasikiwa vyema na mdada aliekuwa amamekaa karibu kabisa na chumba walichokuwamo wazee wale alikuwa ameshika simu janja yake akionekana kuperuzi ila alikuwa anatuma ujumbe mahali na ujumbe ule uliibua jambo lingine tena katika familia ile ya mzee Mashimo.
Jambo ambalo kamwe hawatakaa walisahau katika maisha yao yote.
****
Wakati hayo yakiendelea nyumbani kwa kina Vedi; Vedi yeye alikuwa ndani ya daladala akielekea hospitali ya mwananyamala kulikokuwa kumehifadhiwa mwili wa mtu aliesemekana ni yeye.
Nae alitaka kujihakikishia mwenyewe mtu huyo ambae dada yake alithibitisha ni yeye hadi kupelekea kuwekwa msiba nyumbani kwao.
Mwanzo hakuwa ameona uzito wa jambo lile,ila muda ulivyozidi kusogea aliona ni jambo ambalo halijatokea bahati mbaya ni kama kuna mipango hivi inayoendelea juu yake.
Mipango ndio; lakini ni nani hasa yupo nyuma yake na kwanini?. Je ni kile kitabu cha marehemu Banzi au ni maiti ya Banzi ama shida ni nini hasa!.
Hakukuwa na wa kumjibu swali lake hilo,na wala hakuona kama ni jambo linaloweza kupelelekea taarifa za kifo chake ingali yu hai.
Safari iliendelea huku mawazo lukuki yakikipitia kichwa chake na kumbukumbu ya jinsi alivyoshuhudia watu wakipamiana baada ya kumuona wakihisi ni mzimu wa Vedi na si Vedi mwenyewe.
“Inamaana hata mama nae anajua nimekufa?” Alijiuliza huku taswira la ya mama yake ikijirudia kichwani, aliona upendo wa mama yake kwake tangu yu ngali mdogo hadi ukubwa wake huo.
Alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.
“Hata baba?” Alijiuliza tena na hapo akamkumbuka dada yake Msangu.
“Ooh shiit! Dada nae anahakikisha kaniona mochwari? I can’t believe this…” Alijiwazia kwa uchungu Vedi.
Kamasi na machozi yalitoka kwa pamoja na akatumia tena mgongo wa kiganja chake kujifuta.
Konda nae akatangaza kituo cha Mwananyamala hospitali na gari likasimama.
Wakashuka watu akiwemo na Vedi.
Vedi akavuka barabara na watu wengine waliokuwa wanaingia langoni mwa hospitali ile kwa shida mbali mbali.
Vedi akaingia na kuanza kupiga hatua kuelekea upande uliokuwa umeonyeshwa ni maalumu kwa wagonjwa mahututi.
Akavuka majengo kadhaa na kutafuta kibao kilichokuwa kimeandikwa “Mochwari”
Akakiona!
Ila wakati anapiga hatua ili akifuate na kufuata uelekeo kulipooneshwa;aliona mtu akiwa na watu wengine wawili na jumla akawa ameona watu watatu.
Wawili walikuwa wamevaa fulana nyeupe zenye rangi ya kufanana na suruali za jinzi zenye rangi tofauti.
Walionekana kuwa ni watu wenye mazoezi kwa jinsi miili yao ilivyoonekana imara.
Wawili wale hakuwafahamu kabisa na ndo mara ya kwanza kuwaona,ila mmoja kati yao alikuwa anamfahamu na alikuwa amevaa mavazi yale yale aliomuona nayo siku ya kwanza.
Koti jeusi na kichwani alivaa kofia ya pama na miwani usoni, viatu vyeusi vya buti na suruali ya Jinzi na mikononi aliziba viganja vyake kwa glavu nyeusi.
Alikuwa ni yule yule jamaa aliemuona ndani ya meli usiku wa ndoa ya rafiki yake kipenzi Nyamizi.
Ni yule yule bwana ambae alimuona akiingia na kutoka ndani ya kikontena kilichokuwa kwenye chumba cha ufundi ndani ya meli, alikuwa ni yule jamaa ambae walikutana mlangoni na kisha akamuona akiwa ukumbini akitafuta kitu ambacho yeye hakukijua.
Alikuwa ni yule mtu anaevaa miwani hata wakati wa giza nene.
Vedi alijikuta akihisi kama maji yanamwagika tumboni mwake kisha mwili ukaingiwa na ubaridi wa woga.
Hakujua ni kwa nini hali ile ilimkuta punde tu baada ya kumuona mtu yule.
Akajichanganya na watu wachache ambao walikuwa wanapishana huku na huko, ila macho yake bado yalikuwa kwa wale watu watatu ambao walikuwa wakijadili jambo huku wakiwa wameegemea nguzo ilioshika bati.
Vedi alijikuta anashawishika kutaka kujua watu wale walikuwa pale kwa dhumuni gani.
Akaangaza kidogo na kuona gari moja ikiwa imepaki sehemu ambayo yeye aliona itamfaa kujibanza na kushuhudia nyendo za watu wale.
Akajibanza!
Watu wale waliendelea kuongea na punde akatokea kijana mmoja aliekuwa amevaa mavazi ya kitabibu;koti jeupe na alizungusha shingoni kifaa cha kupima mienendo ya mapigo ya moyo.
Kijana yule akawasabahi watu wale na kisha akapeana nao mkono kila mmoja.
Walifahamiana bila shaka.
Walizungumza kidogo kisha tabibu yule akaanza kuondoka na wale watu nao walimfuata.
Vedi nae akafuata!
Walitembea kidogo na kuingia kwenye ofisi ambayo tofauti na ofisi zingine yenyewe iliandikwa jina la mwenye ofisi ile.
“Dr.Willy Masimba”.
Kwanini iliandikwa vile wakati ofisi zingine zote ziliandikwa majina ya vitengo wanavyohudumu matabibu wanaokuwa ndani yake?
Hilo hakujua.
Vedi akakumbuka kitu, akaingiza mkono kwenye mkoba wake na kutoa kalamu na kile kitabu alichokuwa amechukua ndani ya kontena na baadae aligundua kinamilikiwa na mtu alieitwa Banzi.
Akaandika jina la ofisi ile na pembeni yake akaandik pia jina lake ili yeyote atakaekuja kukutana na kitabu kile kitabu, basi aelewe kilitumiwa na watu wawili tofauti.
Akamalizia kwa kuandika tarehe ya siku hiyo.
Akasubiri kwa dakika ishirini zaidi ili aone watu wale kama watatoka, ila bado hakuwaona na wala hakuona dalili za kutoka kwao.
Akaelekea kule alikotaka kwenda mwanzo.
Akafuata uelekeo huo na hatimae alijikuta akiingia kwenye ofisi za wahifadhi maiti.
Akajitambulisha kwa jina bandia kisha akaomba kuutambua mwili wa rafiki yake alieitwa Vedi Mashimo.
Wahusika walimpa mtu wa kumpeleka kwenye hivyo vyumba vya kuhifadhia maiti.
Akapelekwa hadi kwenye jokofu lililokuwa limehifadhi maiti ya Vedi kulingana na maelezo yaliokuwa yamewekwa kwenye kitabu cha kumbukumbu.
Mlinzi akavuta.
Na hapo mlinzi akamkazia macho Vedi na kisha akarudisha macho kwenye jokofu, mara akaruka nyuma kwa nguvu huku akiachia ukelele wa woga.
Vedi nae akachungulia.
Lauhaula!!!
Alijiona yeye mwenyewe akiwa ametulia tuli ndani ya jokofu. Hata mavazi aliokuwa amevaa usiku wa sherehe ile, hadi mtindo wa nywele ulikuwa ni ule ule aliokuwa ameuweka siku ile.
Vedi akaruka nyuma huku vidole vyake vikiwa vimekimbilia kuziba mdomo ili asipige kelele.
Alijiona yeye mwenyewe akiwa ndani ya jokofu la kuhifadhia maiti.
Mlinzi nae alikuwa hoi akitetemeka.
Mara mlango ukasukumwa na wakaingia wale watu watatu aliowaona Vedi wakiwa wameongozana na Dr. Masimba.
Vedi akagwaya!!.
kaza mkono kakaRIWAYA; BAHARIA
NAP; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660 SEHEMU YA TANO
Mzee Mashimo alikodoa macho kwa kutoamini anachosikia kutoka kwa mkewe.
“Mke wangu unaanza kuchanganyikiwa kwa kifo hiki ngoja niite mchungaji ak..”
“Nipo mzima kabisa wala sijaugua na naomba tusitishe msiba huu Baba Msangu”
“Mama Msangu unakufuru sasa!” Mzee Mashimo aliwaka kwa hasira na kisha akatoka ndani na kuelekea nje bila kutia neno zaidi na aliona kama mkewe ameanza kuchanganyikiwa na msiba ule.
Maongezi yao yalikuwa yanasikiwa vyema na mdada aliekuwa amamekaa karibu kabisa na chumba walichokuwamo wazee wale alikuwa ameshika simu janja yake akionekana kuperuzi ila alikuwa anatuma ujumbe mahali na ujumbe ule uliibua jambo lingine tena katika familia ile ya mzee Mashimo.
Jambo ambalo kamwe hawatakaa walisahau katika maisha yao yote.
**** Wakati hayo yakiendelea nyumbani kwa kina Vedi; Vedi yeye alikuwa ndani ya daladala akielekea hospitali ya mwananyamala kulikokuwa kumehifadhiwa mwili wa mtu aliesemekana ni yeye.
Nae alitaka kujihakikishia mwenyewe mtu huyo ambae dada yake alithibitisha ni yeye hadi kupelekea kuwekwa msiba nyumbani kwao.
Mwanzo hakuwa ameona uzito wa jambo lile,ila muda ulivyozidi kusogea aliona ni jambo ambalo halijatokea bahati mbaya ni kama kuna mipango hivi inayoendelea juu yake.
Mipango ndio; lakini ni nani hasa yupo nyuma yake na kwanini?. Je ni kile kitabu cha marehemu Banzi au ni maiti ya Banzi ama shida ni nini hasa!.
Hakukuwa na wa kumjibu swali lake hilo,na wala hakuona kama ni jambo linaloweza kupelelekea taarifa za kifo chake ingali yu hai. Safari iliendelea huku mawazo lukuki yakikipitia kichwa chake na kumbukumbu ya jinsi alivyoshuhudia watu wakipamiana baada ya kumuona wakihisi ni mzimu wa Vedi na si Vedi mwenyewe.
“Inamaana hata mama nae anajua nimekufa?” Alijiuliza huku taswira la ya mama yake ikijirudia kichwani, aliona upendo wa mama yake kwake tangu yu ngali mdogo hadi ukubwa wake huo.
Alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.
“Hata baba?” Alijiuliza tena na hapo akamkumbuka dada yake Msangu.
“Ooh shiit! Dada nae anahakikisha kaniona mochwari? I can’t believe this…” Alijiwazia kwa uchungu Vedi.
Kamasi na machozi yalitoka kwa pamoja na akatumia tena mgongo wa kiganja chake kujifuta.
Konda nae akatangaza kituo cha Mwananyamala hospitali na gari likasimama.
Wakashuka watu akiwemo na Vedi.
Vedi akavuka barabara na watu wengine waliokuwa wanaingia langoni mwa hospitali ile kwa shida mbali mbali.
Vedi akaingia na kuanza kupiga hatua kuelekea upande uliokuwa umeonyeshwa ni maalumu kwa wagonjwa mahututi.
Akavuka majengo kadhaa na kutafuta kibao kilichokuwa kimeandikwa “Mochwari”
Akakiona!
Ila wakati anapiga hatua ili akifuate na kufuata uelekeo kulipooneshwa;aliona mtu akiwa na watu wengine wawili na jumla akawa ameona watu watatu.
Wawili walikuwa wamevaa fulana nyeupe zenye rangi ya kufanana na suruali za jinzi zenye rangi tofauti.
Walionekana kuwa ni watu wenye mazoezi kwa jinsi miili yao ilivyoonekana imara.
Wawili wale hakuwafahamu kabisa na ndo mara ya kwanza kuwaona,ila mmoja kati yao alikuwa anamfahamu na alikuwa amevaa mavazi yale yale aliomuona nayo siku ya kwanza.
Koti jeusi na kichwani alivaa kofia ya pama na miwani usoni, viatu vyeusi vya buti na suruali ya Jinzi na mikononi aliziba viganja vyake kwa glavu nyeusi. Alikuwa ni yule yule jamaa aliemuona ndani ya meli usiku wa ndoa ya rafiki yake kipenzi Nyamizi.
Ni yule yule bwana ambae alimuona akiingia na kutoka ndani ya kikontena kilichokuwa kwenye chumba cha ufundi ndani ya meli, alikuwa ni yule jamaa ambae walikutana mlangoni na kisha akamuona akiwa ukumbini akitafuta kitu ambacho yeye hakukijua.
Alikuwa ni yule mtu anaevaa miwani hata wakati wa giza nene. Vedi alijikuta akihisi kama maji yanamwagika tumboni mwake kisha mwili ukaingiwa na ubaridi wa woga.
Hakujua ni kwa nini hali ile ilimkuta punde tu baada ya kumuona mtu yule.
Akajichanganya na watu wachache ambao walikuwa wanapishana huku na huko, ila macho yake bado yalikuwa kwa wale watu watatu ambao walikuwa wakijadili jambo huku wakiwa wameegemea nguzo ilioshika bati.
Vedi alijikuta anashawishika kutaka kujua watu wale walikuwa pale kwa dhumuni gani.
Akaangaza kidogo na kuona gari moja ikiwa imepaki sehemu ambayo yeye aliona itamfaa kujibanza na kushuhudia nyendo za watu wale.
Akajibanza!
Watu wale waliendelea kuongea na punde akatokea kijana mmoja aliekuwa amevaa mavazi ya kitabibu;koti jeupe na alizungusha shingoni kifaa cha kupima mienendo ya mapigo ya moyo.
Kijana yule akawasabahi watu wale na kisha akapeana nao mkono kila mmoja.
Walifahamiana bila shaka.
Walizungumza kidogo kisha tabibu yule akaanza kuondoka na wale watu nao walimfuata. Vedi nae akafuata!
Walitembea kidogo na kuingia kwenye ofisi ambayo tofauti na ofisi zingine yenyewe iliandikwa jina la mwenye ofisi ile.
“Dr.Willy Masimba”.
Kwanini iliandikwa vile wakati ofisi zingine zote ziliandikwa majina ya vitengo wanavyohudumu matabibu wanaokuwa ndani yake?
Hilo hakujua.
Vedi akakumbuka kitu, akaingiza mkono kwenye mkoba wake na kutoa kalamu na kile kitabu alichokuwa amechukua ndani ya kontena na baadae aligundua kinamilikiwa na mtu alieitwa Banzi.
Akaandika jina la ofisi ile na pembeni yake akaandik pia jina lake ili yeyote atakaekuja kukutana na kitabu kile kitabu, basi aelewe kilitumiwa na watu wawili tofauti.
Akamalizia kwa kuandika tarehe ya siku hiyo. Akasubiri kwa dakika ishirini zaidi ili aone watu wale kama watatoka, ila bado hakuwaona na wala hakuona dalili za kutoka kwao. Akaelekea kule alikotaka kwenda mwanzo. Akafuata uelekeo huo na hatimae alijikuta akiingia kwenye ofisi za wahifadhi maiti.
Akajitambulisha kwa jina bandia kisha akaomba kuutambua mwili wa rafiki yake alieitwa Vedi Mashimo.
Wahusika walimpa mtu wa kumpeleka kwenye hivyo vyumba vya kuhifadhia maiti. Akapelekwa hadi kwenye jokofu lililokuwa limehifadhi maiti ya Vedi kulingana na maelezo yaliokuwa yamewekwa kwenye kitabu cha kumbukumbu.
Mlinzi akavuta.
Na hapo mlinzi akamkazia macho Vedi na kisha akarudisha macho kwenye jokofu, mara akaruka nyuma kwa nguvu huku akiachia ukelele wa woga.
Vedi nae akachungulia.
Lauhaula!!!
Alijiona yeye mwenyewe akiwa ametulia tuli ndani ya jokofu. Hata mavazi aliokuwa amevaa usiku wa sherehe ile, hadi mtindo wa nywele ulikuwa ni ule ule aliokuwa ameuweka siku ile.
Vedi akaruka nyuma huku vidole vyake vikiwa vimekimbilia kuziba mdomo ili asipige kelele.
Alijiona yeye mwenyewe akiwa ndani ya jokofu la kuhifadhia maiti.
Mlinzi nae alikuwa hoi akitetemeka.
Mara mlango ukasukumwa na wakaingia wale watu watatu aliowaona Vedi wakiwa wameongozana na Dr. Masimba.
Vedi akagwaya!!.
Mbona umeguna?
misukusuko anayopitia tu huyo dada,hasa hilo la maiti kufanana nae kila kitu hadi nguo alizovaaMbona umeguna?