Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Ndugu wana MMU,
Hivi majuzi nilipata nafasi ya kutembelea mitaa ya watu wa kawaida na kukutana na maisha halisi ya Watanzania. Nilijihisi na kukubali kuwa nimetengwa (detached) na maisha ya kawaida ya ndugu na jamaa zangu...Baadhi ya mambo niliyoshuhudia ni ngumu kuamini!
1. Kuna jamaa yangu ndiye mwenye simu katika kimtaa chake..kwa hiyo inaazimwa na kuzunguka karibia usawa wa mabalozi 2 wa nyumba kumi kumi. Watu wanafanya kubadilisha chips...Kwa hiyo alinambia nisipompata nijue simu iko kwa majirani!
2. Mwingine alinambia kuwa redio yake ikiharibika basi unakuwa mwisho wa kupata chakula cha usiku. Anasema kwa jinsi vyumba vilivyobanana na kwa vile hakuna ceilings...redio ndiye mkombozi wao...Hii ilitokana na mshangao wangu wa kwa nini redio zinapigwa karibia 24hrs
3. Kuna wengine hawana vyoo...kwa hiyo wanapata hifadhi kwa majirani...Hapa nikamkubuka Ex-GF wangu ambaye aliwahi kunambia kuwa hajawahi kuchimba dawa (kubwa) porini!!
4. Watu wengine walishasahau sura za noti..ukimpa noti ya shs 500 au 1000 anafunga novena kukuombea!!
5. Jamaa niliosoma nao miaka ile wanaonekana kama babu zangu...wamechoka na tayari wengine tumeagana...very sad in deed
6. Pamoja na matatizo niliyoona,....bado watu wametinga T-shirt za kijani za kuanzia Mkapa 1995 hadi JK 2010 na mabango yao. Pia bendera za kijana ndio zimepamba mitaa yao utadhani wanaandaa dhifa ya Taifa kwa Mgeni maarufu wa Ikulu..
7. Pamoja na kutambua kuwa sumu inayowaua ni umaskini...hawataki kusikia sauti nyingine zaidi ya kuwaeleza kuwa walinde amani yao!!
Hivi majuzi nilipata nafasi ya kutembelea mitaa ya watu wa kawaida na kukutana na maisha halisi ya Watanzania. Nilijihisi na kukubali kuwa nimetengwa (detached) na maisha ya kawaida ya ndugu na jamaa zangu...Baadhi ya mambo niliyoshuhudia ni ngumu kuamini!
1. Kuna jamaa yangu ndiye mwenye simu katika kimtaa chake..kwa hiyo inaazimwa na kuzunguka karibia usawa wa mabalozi 2 wa nyumba kumi kumi. Watu wanafanya kubadilisha chips...Kwa hiyo alinambia nisipompata nijue simu iko kwa majirani!
2. Mwingine alinambia kuwa redio yake ikiharibika basi unakuwa mwisho wa kupata chakula cha usiku. Anasema kwa jinsi vyumba vilivyobanana na kwa vile hakuna ceilings...redio ndiye mkombozi wao...Hii ilitokana na mshangao wangu wa kwa nini redio zinapigwa karibia 24hrs
3. Kuna wengine hawana vyoo...kwa hiyo wanapata hifadhi kwa majirani...Hapa nikamkubuka Ex-GF wangu ambaye aliwahi kunambia kuwa hajawahi kuchimba dawa (kubwa) porini!!
4. Watu wengine walishasahau sura za noti..ukimpa noti ya shs 500 au 1000 anafunga novena kukuombea!!
5. Jamaa niliosoma nao miaka ile wanaonekana kama babu zangu...wamechoka na tayari wengine tumeagana...very sad in deed
6. Pamoja na matatizo niliyoona,....bado watu wametinga T-shirt za kijani za kuanzia Mkapa 1995 hadi JK 2010 na mabango yao. Pia bendera za kijana ndio zimepamba mitaa yao utadhani wanaandaa dhifa ya Taifa kwa Mgeni maarufu wa Ikulu..
7. Pamoja na kutambua kuwa sumu inayowaua ni umaskini...hawataki kusikia sauti nyingine zaidi ya kuwaeleza kuwa walinde amani yao!!