Bado ananipenda kweli?

Bado ananipenda kweli?

Kaazi kweli kweli...

Huyo hana lolote nae anakuzimia lakini ana mambo ya kitoto na inaonekana hujajua hili bado..

Cha kufanya mwache na fanya mambo yako bila kinyongo nae,onesha una furaha na usimtafute subiri mpaka yeye aanze kukutafuta...

Atakurudia tu na akifanya hivyo jiangalie kama bado wakati huo utakuwa unamhitaji,kama utakuwa unamhitaji mwambie wazi kuwa unahitaji msimamo na akikuelewa endeleeni kula raha ya dunia

Asipokurudia shukuru Mungu endelea na maisha yako...

Ukiwa unafanya zoezi hili utapata upinzani wa hisia,usirudi nyuma na usizisikilize hisia zako maana hutakufa kwa kukosa raha kwa muda,hii ndio njia ya kukua,endelea tu na utaweza....

Kila la kheri...
 
Haaaa dada pole wanaokushauri wengi ni ME,wanajua walivyowenyewe,nakushauri ufuate wanayosema jamaa amekuwa mkweli
 
We ushaambiwa kila kitu sijui bado unang'ang'ania nn..Endelea na maisha yako huyo jamaa achana nae..Na nakushauri kaa nae mbali..Mana kadri unavyozidi kuwasiliana nae we ndo unazidi kudevelop feelings kwake wakati ye hana habari..
 
Ushaachwa ila hujaridhika nankiasi cha maumivu ukichopata



Kukujibu


Hapana...hakupendi
 
We ushaambiwa kila kitu sijui bado unang'ang'ania nn..Endelea na maisha yako huyo jamaa achana nae..Na nakushauri kaa nae mbali..Mana kadri unavyozidi kuwasiliana nae we ndo unazidi kudevelop feelings kwake wakati ye hana habari..

Watu wengine sijui waambiwe kichina......
 
Wasalaam wanajamii forum wote.

Leo ni mara yangu ya kwanza kuleta mada hapa na ninakiri kuwa nilikuwa msomaji tu wa kawaida.

Nina tatizo kubwa linalonisumbua kwa sasa. Mimi ni mwanamke. Nilikuwa na mpenzi tuliedumu nae mwaka mmoja na nusu, mimi nikimpenda kweli ila sijui kwa mwenzangu ingawa naye nilizoea kusikia akiniambia hivyo. Miezi miwili iliyopita tuligombana.

Chanzo ikiwa ni yeye. Akidai kuwa anahitaji kuwa huru tu ingawa hana msichana mwingine. Niliomba msamaha kwa yote niliyomfnyia mpaka kufikia huko lakini hakuridhia. Tukaachana ila tukiendelea kuwasiliana na kusaidiana kama zamani. Ukaribu bado ulikuwepo ila haukua ule wa kimapenzi.

Mwenzangu aliendelea kuwa na furaha na hata mara nyingine aliongea vitu ambavyo nilihisi alitaka nimwonee wivu. Hali hiyo ikanikera na tukagombana tena na kumtukana juu. Ukaribu wetu ukapungua kwa kiwango kikubwa na hata simu hatukupigiana kwa muda wa mwezi mmoja.

Kiukweli nilimmisi muda huo nikatamani tena niwe karibu nae. Jana usiku nimempigia simu na kumuomba samahani, cha ajabu ananiambia yeye hana shida kabisa na mimi na bado anapenda kuwa karibu yangu. Usiku mzima ananitumia message kunitania hili na lile ingawa si za kimapenzi.
Hivi huyu mtu bado ananipenda kweli?

Msaada tafadhali.

huyu hakupendi ila wewe unaonekana unampenda sana hadi ukawa kipofu wa kuliona hili, nakushauri jikaze baada ya muda utamsahau na utaendelea kufurahia maisha
 
Wasalaam wanajamii forum wote.

Leo ni mara yangu ya kwanza kuleta mada hapa na ninakiri kuwa nilikuwa msomaji tu wa kawaida.

Nina tatizo kubwa linalonisumbua kwa sasa. Mimi ni mwanamke. Nilikuwa na mpenzi tuliedumu nae mwaka mmoja na nusu, mimi nikimpenda kweli ila sijui kwa mwenzangu ingawa naye nilizoea kusikia akiniambia hivyo. Miezi miwili iliyopita tuligombana.

Chanzo ikiwa ni yeye. Akidai kuwa anahitaji kuwa huru tu ingawa hana msichana mwingine. Niliomba msamaha kwa yote niliyomfnyia mpaka kufikia huko lakini hakuridhia. Tukaachana ila tukiendelea kuwasiliana na kusaidiana kama zamani. Ukaribu bado ulikuwepo ila haukua ule wa kimapenzi.

Mwenzangu aliendelea kuwa na furaha na hata mara nyingine aliongea vitu ambavyo nilihisi alitaka nimwonee wivu. Hali hiyo ikanikera na tukagombana tena na kumtukana juu. Ukaribu wetu ukapungua kwa kiwango kikubwa na hata simu hatukupigiana kwa muda wa mwezi mmoja.

Kiukweli nilimmisi muda huo nikatamani tena niwe karibu nae. Jana usiku nimempigia simu na kumuomba samahani, cha ajabu ananiambia yeye hana shida kabisa na mimi na bado anapenda kuwa karibu yangu. Usiku mzima ananitumia message kunitania hili na lile ingawa si za kimapenzi.
Hivi huyu mtu bado ananipenda kweli?

Msaada tafadhali.

Nyie bado mnapendana ila jamaa anakupima wewe na binti mwingine na hajaamua bado awe na yupi hasa.

Halafu Acha Matusi yanakupunguzia kama sio kukuondolea heshima.
 
Mpendwa father superior, waswahili wanasema ukweli wa mtu upo moyoni mwa mtu. Nadhani hilo swali lako ungemuuliza huyo mpenzi wako Yeye pekee ndieye anayeweza kukuambia ukweli kama bado anakupenda au la endapo ataamua kukueleza ukweli.
 
Anaona furaha ma amani mkiwa kama marafaki. Anakupenda kama rafiki na siyo vinginevyo. Keshoaona akuachie mapema kabla hamjaanza kusema mmepotezeana muda.
 
Wasalaam wanajamii forum wote.

Leo ni mara yangu ya kwanza kuleta mada hapa na ninakiri kuwa nilikuwa msomaji tu wa kawaida.

Nina tatizo kubwa linalonisumbua kwa sasa. Mimi ni mwanamke. Nilikuwa na mpenzi tuliedumu nae mwaka mmoja na nusu, mimi nikimpenda kweli ila sijui kwa mwenzangu ingawa naye nilizoea kusikia akiniambia hivyo. Miezi miwili iliyopita tuligombana.

Chanzo ikiwa ni yeye. Akidai kuwa anahitaji kuwa huru tu ingawa hana msichana mwingine. Niliomba msamaha kwa yote niliyomfnyia mpaka kufikia huko lakini hakuridhia. Tukaachana ila tukiendelea kuwasiliana na kusaidiana kama zamani. Ukaribu bado ulikuwepo ila haukua ule wa kimapenzi.

Mwenzangu aliendelea kuwa na furaha na hata mara nyingine aliongea vitu ambavyo nilihisi alitaka nimwonee wivu. Hali hiyo ikanikera na tukagombana tena na kumtukana juu. Ukaribu wetu ukapungua kwa kiwango kikubwa na hata simu hatukupigiana kwa muda wa mwezi mmoja.

Kiukweli nilimmisi muda huo nikatamani tena niwe karibu nae. Jana usiku nimempigia simu na kumuomba samahani, cha ajabu ananiambia yeye hana shida kabisa na mimi na bado anapenda kuwa karibu yangu. Usiku mzima ananitumia message kunitania hili na lile ingawa si za kimapenzi.
Hivi huyu mtu bado ananipenda kweli?

Msaada tafadhali.

Kukupenda huyu bado anakupenda sio kimapenzi ila kama kirafiki tu, Kwanza nampa pongezi huyu jamaa kuwa open kwako kuliko kukupotezea muda ukadhania una nafasi kumbe laa. Jamaa ana tabia kama zangu kuachana na mtu kwa matusi kwangu no amekuja kuomba penzi kistaarabu na amekuwacha kistaarabu. ukiwa na rafiki kama huyu utajifunza mengi kwenye maisha ya mapenzi na ya kawaida. kuna story nimemaliza kuisoma alieposti anaitwa Natafuta yaani huyu mtu nimemuona wa maajabu sana.
 
Haya ndo madhara ya kuwa kwa mahusiano mda mrefu eti wanasomana, kama anataka kusoma si aende shule? Bi zeya weitingi utapoteza bahati kwa wanaokulilia.
 
Mpendwa father superior, waswahili wanasema ukweli wa mtu upo moyoni mwa mtu. Nadhani hilo swali lako ungemuuliza huyo mpenzi wako Yeye pekee ndieye anayeweza kukuambia ukweli kama bado anakupenda au la endapo ataamua kukueleza ukweli.

Ninapomuuliza jibu analonipa ni kwamba bado ananipenda sana. Hata kuna muda anakuja akiwa amelewa na anadai ananipenda lakini matendo yake siyaelewi.
 
Watu ambao kweli walikuwa katika mahusiano hawawezi tena kuwa marafiki, hii nilijionea hata kwangu. Huyo mtu wako bado anakupenda ila inawezekana sasa hivi anahitaji nafasi ya kufanya jambo fulani ama anakupima nini tu kutaka kukujua vema. Vumilia tu, anaweza kurudi endapo utafaulu mtihani wake. Mpe nafasi, acha kumtafuta wala kumtukana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom