popo1986
JF-Expert Member
- Jul 30, 2014
- 1,120
- 373
Mkuu mm nikutoe wasiwasi hamna mazingira magumu unayoyawaza, hii ni hali ya kawaida sana kimsingi nimuonavyo mm huyu Rais anahanu na shaiku ya kuinyoosha Tanzania ilifika kipindi Tanzania hii ilikuwa ni Shamba la bibi kila Mkuu anachuma anavyotaka yaani ilikuwa ni nchi ya familia Fulani zilizo kwenye system,sasa mambo hayo yabakie hukohuko kwenye vyama na sio katika Taifa.Tangu Rais Magufuli aanze kutoa matamko yamekua ni mengi na inaonekana hataki utani wala kuchezewa.
Kama alivyojipambanua kwenye hotuba zake za hivi karibuni, sasa katika mtiririko wa matamko na ilani zake amebakisha amri mbili tu.
Amri ya kwanza ni wananchi wavamie kila fisadi wanaemjua amepata pesa kwa njia zisizo halali na mali wajichukulie vyao,maana inaonekana rais ana hasira sana na hao watu.
Amri ya pili ni wananchi kutembea mwisho saa kumi na mbili kila mmoja awe nyumbani kwake.
Nchi inavyokwenda tunatakiwa kuomba Mungu sababu watu wamewasha moto halafu mmoja ameshika jinga la moto kuelekea kwenye mapipa ya petroli na hakuna wa kumzuia kasi ni kubwa!
Mungu ibariki Tanzania inapita kwenye majaribu makubwa.
Mungu ibariki Tanzania ,Mungu mbariki Rais wetu.