Badala ya kubariki watoto na kizazi chako unabariki Israel usiyoijua wala isiyokujua; Acheni uchizi

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,553
52,288
BADALA YA KUBARIKI WATOTO NA KIZAZI CHAKO UNABARIKI ISRAEL USIYOIJUA WALA ISIYOKUJUA; ACHENI UCHIZI.

Anàandika, Robert Heriel

Mtibeli

Yesu kama Watibeli wengine alishawahi kuwatolea maneno mbaya mbovu Wafuasi wake akiwaambia;

Lk 23:28

Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.


Kitabu cha biblia hasa vitabu alivyoandika Musa vimeandikwa kwa namna Mbili. Mosi, vimeandikwa kwa maelekezo ya Mungu mwenyewe, lakini pili, vimeandikwa kisiasa na Musa mwenyewe ambaye ndiye Legend namba moja wa Uyahudi.

Jua kuwa Musa alikuwa Msomi wa kiyahudi aliyekulia katika jumba la kifalme la Farao. Hivyo elimu za wakati huo za kisiasa alikuwa nazo mbali na elimu ya dini kutoka kwa Mama yake.

Maneno ya kuwa ukiibariki Israel unabarikiwa na ukiilani Israel unalaaniwa yameasisiwa na yeye mwenyewe Musa ikiwa kama Propaganda za kisiasa katika kutetea maslahi ya Waisrael kwa wakati huo. Zingatia kwa zama walizokuwa kina Musa ilikuwa Zama za Vita ya miungu. Na kila jamii ilikuwa inapambana kugombea maeneo nyeti ya huu ulimwengu.

Hivyo katika namna ya kukabiliana na maadui zao hasa wale maadui waoga walitumia zaidi propaganda za Imani kuwadhibiti adui zao. Moja ya maneno na misemo waliyoitumia ilikuwa huo msemo wa "kuibariki Israel ni kutafuta baraka, na kuilaani ni kujitafutia Laana"

Kauli hiyo kwa mara ya kwanza aliiandika Musa Kwa mhusika Ibrahim akipewa maneno hayo na Yahweh.

Propaganda hizo za kidini hazikuishia kutumika katika zama hizo za vita ya miungu. Bali zimetumika mpaka kipindi cha juzi cha Ukoloni ambapo Ukristo ulitumika kusambaza propaganda za kulainisha nyoyo za Waafrika ili wakoloniwe( watawaliwe).

Sio hivyo tuu, hata hivi leo tumeona viongozi wengi wa dini wakitumia maneno na misemo ya kiiimani kama propaganda ya kutawala na kuwaburuza Watu vile wanavyotaka. Mfano, msemo wa kutomnyooshea Mtumishi wa Mungu kidole au kutomkosoa ni msemo wa propaganda wa kijinga mno ambao hutumika kudhibiti Watu walioamua kutotumia akili zao.

Yaani ni wanadamu fulani waliojitia cheo au hadhi fulani ambao wanatumia kisingizio cha imani kuwatumia wanadamu wenzao vibaya.

Israel ni moja ya mataifa yaliyoburuzwa na kupigwa sana katika Historia ya dunia. Kama yalivyo mataifa mengine, Israel imeshatawaliwa mara kibao na kupelekwa utumwani mara kibao.

Israel ni Watu kama Watu wengine ndio maana wanapitia mambo yote wanadamu wengine wanayopitia.

Kuiombea Israel badala ya kuombea nchi yako na familia yako ni uleule ujinga wa kumchangia mchungaji gari wakati wewe huna hata baiskeli. Au kumjengea nyumba mchungaji wakati waumini mnaishi maisha ya kindezi. Ni upumbavu tuu.

Propaganda ni upepo ambao hubeba Watu wenye upeo mdogo na kuwaburuza vile watakavyo.

Leo sina mengi ya kusema. Acha nipumzike tuu.

Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.

Robert Heriel

Taikon wa Fasihi

Kwa sasa Dar es salaam
 
mapalestina ni watu waliolaaniwaa walee yaani basii...kuna video kulee telegram yakiwaingilia kinyume wale vijana wakitanganyika akina molel pale gazaa mazee dah...
FB_IMG_1699422527907.jpg
 
N
BADALA YA KUBARIKI WATOTO NA KIZAZI CHAKO UNABARIKI ISRAEL USIYOIJUA WALA ISIYOKUJUA; ACHENI UCHIZI.

Anàandika, Robert Heriel

Mtibeli

Yesu kama Watibeli wengine alishawahi kuwatolea maneno mbaya mbovu Wafuasi wake akiwaambia;

Lk 23:28

Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.


Kitabu cha biblia hasa vitabu alivyoandika Musa vimeandikwa kwa namna Mbili. Mosi, vimeandikwa kwa maelekezo ya Mungu mwenyewe, lakini pili, vimeandikwa kisiasa na Musa mwenyewe ambaye ndiye Legend namba moja wa Uyahudi.

Jua kuwa Musa alikuwa Msomi wa kiyahudi aliyekulia katika jumba la kifalme la Farao. Hivyo elimu za wakati huo za kisiasa alikuwa nazo mbali na elimu ya dini kutoka kwa Mama yake.

Maneno ya kuwa ukiibariki Israel unabarikiwa na ukiilani Israel unalaaniwa yameasisiwa na yeye mwenyewe Musa ikiwa kama Propaganda za kisiasa katika kutetea maslahi ya Waisrael kwa wakati huo. Zingatia kwa zama walizokuwa kina Musa ilikuwa Zama za Vita ya miungu. Na kila jamii ilikuwa inapambana kugombea maeneo nyeti ya huu ulimwengu.

Hivyo katika namna ya kukabiliana na maadui zao hasa wale maadui waoga walitumia zaidi propaganda za Imani kuwadhibiti adui zao. Moja ya maneno na misemo waliyoitumia ilikuwa huo msemo wa "kuibariki Israel ni kutafuta baraka, na kuilaani ni kujitafutia Laana"

Kauli hiyo kwa mara ya kwanza aliiandika Musa Kwa mhusika Ibrahim akipewa maneno hayo na Yahweh.

Propaganda hizo za kidini hazikuishia kutumika katika zama hizo za vita ya miungu. Bali zimetumika mpaka kipindi cha juzi cha Ukoloni ambapo Ukristo ulitumika kusambaza propaganda za kulainisha nyoyo za Waafrika ili wakoloniwe( watawaliwe).

Sio hivyo tuu, hata hivi leo tumeona viongozi wengi wa dini wakitumia maneno na misemo ya kiiimani kama propaganda ya kutawala na kuwaburuza Watu vile wanavyotaka. Mfano, msemo wa kutomnyooshea Mtumishi wa Mungu kidole au kutomkosoa ni msemo wa propaganda wa kijinga mno ambao hutumika kudhibiti Watu walioamua kutotumia akili zao.

Yaani ni wanadamu fulani waliojitia cheo au hadhi fulani ambao wanatumia kisingizio cha imani kuwatumia wanadamu wenzao vibaya.

Israel ni moja ya mataifa yaliyoburuzwa na kupigwa sana katika Historia ya dunia. Kama yalivyo mataifa mengine, Israel imeshatawaliwa mara kibao na kupelekwa utumwani mara kibao.

Israel ni Watu kama Watu wengine ndio maana wanapitia mambo yote wanadamu wengine wanayopitia.

Kuiombea Israel badala ya kuombea nchi yako na familia yako ni uleule ujinga wa kumchangia mchungaji gari wakati wewe huna hata baiskeli. Au kumjengea nyumba mchungaji wakati waumini mnaishi maisha ya kindezi. Ni upumbavu tuu.

Propaganda ni upepo ambao hubeba Watu wenye upeo mdogo na kuwaburuza vile watakavyo.

Leo sina mengi ya kusema. Acha nipumzike tuu.

Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.

Robert Heriel

Taikon wa Fasihi

Kwa sasa Dar es salaam
i SAWA nawewe unayeshangilia tiny ya manchesta huku ukiwa huijui wala hawakujuiupo hapo?
 
Nakuunga mkono katika hili.
Tunachopaswa kuomba ni amani na utulivu kwa Taifa letu na mataifa yote! Neno la Mungu linahimiza hivyo, (1Timotheo2:1-2)
Lakini zaidi sana ni kuomba kwa ajili yako binafsi na familia yako!
(Mathayo6:9-14)
 
Nakuunga mkono katika hili.
Tunachopaswa kuomba ni amani na utulivu kwa Taifa letu na mataifa yote! Neno la Mungu linahimiza hivyo, (1Timotheo2:1-2)
Lakini zaidi sana ni kuomba kwa ajili yako binafsi na familia yako!
(Mathayo6:9-14)

Ni kweli kabisa
 
Vipi ile kauli ya Kiongozi anachaguliwa na Mungu

Yoshua 24:15 NEN​

Lakini msipoona vyema kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia, kama ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ngʼambo Frati, au miungu ya Waamori, ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia BWANA.”

1 Samwel 8
4Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samweli huko Rama; 5wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote. 6Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA. 7BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao. 8Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumikia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe. 9Basi sasa, isikilize sauti yao; walakini, uwaonye sana, na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki.
 
Kutokujua nafasi ya Israel katika mambo ya kiroho, siasa za dunia, na uchumi ni shida kwako na hao una waona wewe mazwazwa. Lakini kutokujua hakuondoi ukweli, kwamba Israel itabaki kitovu cha mambo ya kiroho, kisiasa na kiuchumi ya dunia. Na hii ikawe ishara kwamba yupo Mastermind nyuma kila linatokea... Unaweza kumuita Mungu.
Kifupi Israel ni kama saa ya kuonyesha muda wa mabadiliko muhimu kiroho, kisiasa na kiuchumi. Sasa ni wewe kujifunza jinsi ya kuisoma saa hiyo.
 
Back
Top Bottom