Man Mvua
JF-Expert Member
- Apr 12, 2016
- 2,184
- 3,517
Amani iwe nanyi.
Mnamo tarehe 30 July 2020 nilimkopesha L.S. pesa kiasi cha 1.5M kwa riba ya 25% kwa mwezi mmoja hadi tarehe 30 Agosti 2020.
Wakati wa kupeana pesa tuliandikishana mbele ya balozi na ndugu yake mmoja kama shahidi wake. Dhamana ya mkopo wake ilikuwa hati ya serikali ya mtaa ya nyumba yake ambayo haijakamilika iliyopo Tegeta Skanska.
Sharti lililokuwepo kwenye mkataba ni kwamba akishindwa kulipa ndani ya muda kutakuwa na penalty ya 25% kwa kila mwezi utakao ongezeka hivyo hadi kufika 30 December 2020 inakuwa miezi mitano hivyo kufanya penalty kuwa 75% hivyo ukijumlisha na ile riba inakuja kuwa 100%.
Wakati wa kuandikishana sikushikilia dhamana kwa kuwa anayeishi pale ni ndugu yake hivyo nikaondoka na hati na mkataba.
Mpaka naandika hapa Jamaa hajalipa hata senti tano na nilipoanza kumbana alinizungusha sana yaani mnoo na baadae nilipomwambia naenda kumtoa ndugu yake kwenye nyumba (nakumbuka ilikuwa 02 December 2020) jamaa aliongea na polisi ambao ni rafiki zake wanitumie barua ya kuitwa kituo za polisi Kunduchi Mtongani.
Wakati hayo yote yanatokea nilikuwa nimepata udhuru wa kikazi hivyo nilisafiri kwenda Simiyu kikazi. Hivyo nikawaambia ndugu zangu wasitishe kwenda kumtoa ndugu yake kwenye nyumba badala yake wakachukue ile barua.
Sasa sikwenda polisi na nilipokuwa Simiyu balozi alinipigia simu kuna barua yangu nyingine, nikamwambia aniambie niende kureport kituo chochote cha polisi mkoani Simiyu kusema hivyo mpaka sasa hivi kimyaa nami bado sijarudi Dar es Salaam.
Ninavyojua mimi polisi hawaruhusiwi kuingilia kesi za madai(sasa sijui jamaa alimwambia nini polisi hadi kutuma barua ya kuniita kituoni).
DAWA YA DENI NI KULIPA VYOVYOTE ITAKAVYOKUWA.
Ndugu zangu jamaa nilimsaidia akiwa ana shida mnoo tena sanaaa leo hii amefanya nijute sana kumsaidia. Swala la kwenda polisi kuzuia nisishikilie dhamana amenipa hasira zaidi.
KABLA SIJAFANYA MAAMUZI YANGU YA HASIRA NIMEONA NIJE KWENU MNISHAURI KWA LOLOTE HASA KISHERIA ZAIDI.
AHSANTE SANA.
Mnamo tarehe 30 July 2020 nilimkopesha L.S. pesa kiasi cha 1.5M kwa riba ya 25% kwa mwezi mmoja hadi tarehe 30 Agosti 2020.
Wakati wa kupeana pesa tuliandikishana mbele ya balozi na ndugu yake mmoja kama shahidi wake. Dhamana ya mkopo wake ilikuwa hati ya serikali ya mtaa ya nyumba yake ambayo haijakamilika iliyopo Tegeta Skanska.
Sharti lililokuwepo kwenye mkataba ni kwamba akishindwa kulipa ndani ya muda kutakuwa na penalty ya 25% kwa kila mwezi utakao ongezeka hivyo hadi kufika 30 December 2020 inakuwa miezi mitano hivyo kufanya penalty kuwa 75% hivyo ukijumlisha na ile riba inakuja kuwa 100%.
Wakati wa kuandikishana sikushikilia dhamana kwa kuwa anayeishi pale ni ndugu yake hivyo nikaondoka na hati na mkataba.
Mpaka naandika hapa Jamaa hajalipa hata senti tano na nilipoanza kumbana alinizungusha sana yaani mnoo na baadae nilipomwambia naenda kumtoa ndugu yake kwenye nyumba (nakumbuka ilikuwa 02 December 2020) jamaa aliongea na polisi ambao ni rafiki zake wanitumie barua ya kuitwa kituo za polisi Kunduchi Mtongani.
Wakati hayo yote yanatokea nilikuwa nimepata udhuru wa kikazi hivyo nilisafiri kwenda Simiyu kikazi. Hivyo nikawaambia ndugu zangu wasitishe kwenda kumtoa ndugu yake kwenye nyumba badala yake wakachukue ile barua.
Sasa sikwenda polisi na nilipokuwa Simiyu balozi alinipigia simu kuna barua yangu nyingine, nikamwambia aniambie niende kureport kituo chochote cha polisi mkoani Simiyu kusema hivyo mpaka sasa hivi kimyaa nami bado sijarudi Dar es Salaam.
Ninavyojua mimi polisi hawaruhusiwi kuingilia kesi za madai(sasa sijui jamaa alimwambia nini polisi hadi kutuma barua ya kuniita kituoni).
DAWA YA DENI NI KULIPA VYOVYOTE ITAKAVYOKUWA.
Ndugu zangu jamaa nilimsaidia akiwa ana shida mnoo tena sanaaa leo hii amefanya nijute sana kumsaidia. Swala la kwenda polisi kuzuia nisishikilie dhamana amenipa hasira zaidi.
KABLA SIJAFANYA MAAMUZI YANGU YA HASIRA NIMEONA NIJE KWENU MNISHAURI KWA LOLOTE HASA KISHERIA ZAIDI.
AHSANTE SANA.