Babu wa Loliondo sasa yuko hatarini...

Wanaompigia kelele babu ni wezi kwa kutumia Biblia, janja yao kutokea nigeria na india, wanaombea matatizo miaka nenda rudi, sadaka mamiliöni. Lakini hakuna kitu. Babu ukimuona mara moja hutamuona tena. Wameambiwa usihukumu, wao wamepata wapi uwezo wa kuhukumu? PUMBA TUPU.
 
Nenda kwanza shule ya uandishi wa habari ndio utaweza kuchambua post zangu na vichwa vyake.

Wewe kwenye post hii umeandika Ndiyo Siyo Ndiyo Siyo - ongea pointi !

Kumbe ukiguswa kwenye ukweli unajua kukasirika. Hakuna mahali nimeandika ndiyo siyo. Kwa taarifa yako nimesomea uandishi wa kitaalamu. Hii ni pamoja na layout. Sina haja ya kuthibitisha hilo kwani mtu akisoma na kuangalia post yangu atathibitisha hayo. Na kama huoni pointi kwenye post yangu; basi unawathibitishia watu wote watakaosoma thread hii nani kati yetu hana point.

Umeshikilia ubatizo wa maji mengi, maji mengi! Kwa taarifa yako nimebatizwa kwa maji mengi. Ubatizo wa maji mengi siyo hoja ya msingi kwa suala la babu na huduma yake.
 
Unasubiri Revelation ndio ujue kuwa shetani yupo. Pole sana


Bado hapa umepoteza zaidi.....I think you are now beyond heaven

Kumbe kujua shetani yupo huhitaji revelation?

Basi kazi ipo maana naona pengo kubwa kati ya wahubiri injili wa aina yako na injili yenyewe
 
Bado hapa umepoteza zaidi.....I think you are now beyond heaven

Kumbe kujua shetani yupo huhitaji revelation?

Basi kazi ipo maana naona pengo kubwa kati ya wahubiri injili wa aina yako na injili yenyewe

What is revelation? It's a disclosing, discovering or making known of what was before secret, private or unknown.

The Bible has already disclosed Satan. Unataka revelation kutoka wapi tena?
 
Kumbe ukiguswa kwenye ukweli unajua kukasirika. Hakuna mahali nimeandika ndiyo siyo. Kwa taarifa yako nimesomea uandishi wa kitaalamu. Hii ni pamoja na layout. Sina haja ya kuthibitisha hilo kwani mtu akisoma na kuangalia post yangu atathibitisha hayo. Na kama huoni pointi kwenye post yangu; basi unawathibitishia watu wote watakaosoma thread hii nani kati yetu hana point.

Umeshikilia ubatizo wa maji mengi, maji mengi! Kwa taarifa yako nimebatizwa kwa maji mengi. Ubatizo wa maji mengi siyo hoja ya msingi kwa suala la babu na huduma yake.

Kwanini tuandikie mate na wino upo? Subiri baada ya siku chache zijazo utajua mkweli na mwongo ni nani.
 
Mediaman wewe ni Mwongo:
1. Wewe ndiye uliyeanzisha thread nyingine isemayo: Siri Imefichuka! Babu wa Loliondo ametumwa na shetani. Ukweli ni kuwa hakukuwa na siri yoyote isipokuwa mahubiri yako ukitumia maandiko kama unavyopenda yasupport hoja yako. Na hapa unakuja na thread nyingine eti Babu wa Loliondo yupo hatarini ... Hatari gani? Kichwa cha habari yako hakina tofauti na vichwa vya magazeti ya alasiri na dar leo au na magazeti ya udaku. Kichwa kingine habari nyingine.
2. Hapa unasema: Wachunguzi na wataalam wa masuala ya kiroho wamegundua kuwa ndoto hiyo ni ya uongo.Je, wewe ndiye mchunguzi huyo? Habari yako haina reference hata moja ya mchunguzi wa mambo ya kiroho na taarifa yake inasemaje? Ninachoona ni porojo zako zisizoenda shule na ambazo zina mwegemeo wa mafundisho ya Biblia yaliyo nusu nusu.
3. Kwa kutumia Yeremia 23:25-32, unajaribu kushawishi watu kuwa Mungu haoteshi watu ndoto kipindi hiki kwa vile ni makapi: Katika mistari hiyo, BWANA Mungu anazifananisha ndoto na makapi.Huu ni upotoshaji wa Biblia wa waziwazi. Petro katika Mdo 2:17 alimnukuu Nabii Yoeli na alisema : Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho wa yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. Je, andiko hili haliko kwenye Biblia yako? [Kwa bahati mbaya sana kama unaamini juu ya litera translation ... basi ni wazee ndo wanaota ndoto na hapo kwa babu ndo imefika].
4. Unasema: Vyanzo vingine vya habari kutoka nje ya nchi, vimethibitisha kuwa huyo babu wa Loliondo ni nabii wa uongo - Unaendeleza uongo wako kwa kusingizia vyanzo vingine kutoka nje ya nchi - vyanzo gani hivyo? Acha kutuzuga hapa? Kama una vyanzo sema nani na nani kasema nini kwa ushahidi upi?

Nasisitiza: Mediaman ni mwongo kwa vile anajitahidi kutafuta kuungwa mkono na watu ambao hawapo. Biblia inasema: Bali maneni yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu (Mat 5:37).
Na kwavile Mediaman umethubutu kusema uongo basi wewe ndiye mtumishi wa shetani. Yesu alisema: Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuuaji tangu mwanzo ; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo na baba wa huo. (Yon 8:44).
Nafurahia zaidi inavyosomeka kiingereza: (John 8:44) - You belong to your father, the devil, and you want to carry out your father's desire. He was a murderer from the beginning, not holding to the truth, for there is no truth in him. When he lies, he speaks his native language, for he is a liar and the father of lies.

Ukinywa au ukiwa na imani na kikombe cha babu huwezi kuona siri wala hatari. Giza la shetani linakufunika.
 
Kwanini tuandikie mate na wino upo? Subiri baada ya siku chache zijazo utajua mkweli na mwongo ni nani.

Nashukuru umeanza kuona hoja. Hatuna haja ya kuhukumu na kuwa wakali kama unavyofanya. Time will tell. There are so many things we do not know.

Ukinywa au ukiwa na imani na kikombe cha babu huwezi kuona siri wala hatari. Giza la shetani linakufunika.

Kwa taarifa yako sijaenda kwa babu. Hata hivyo siwabezi walioenda huko. I hava a very strong biblical background.
 
Hata Kakobe asilalamike, aliwahi kusema huwezi kuhoji nguvu za Kimungu. Kwa hiyo kama babu anatibu kwa nguvu za Kimungu hakuna kuhoji, au mapato yamepungua kanisani kwenu ndo maana mnamuonea gere babu aliyebarikiwa kweli na Mungu?
 
Unabii hupimwa na neno la Mungu kama yardstick/kioo. Hivyo kama unabii unapingana na neno la Mungu, unabii huo huwa wa uongo. Biblia inasema MTAWEKA MIKONO JUU YA WAGONJWA, NAO WATAPATA AFYA, sasa hii staili mpya ya kikombe imetoka wapi? Ama kwa kuwa kina Askofu Laizer wamekwenda, na kina Sumaye na Lowasa ndio iwe sababu ya kuamini ndoto zake? Kila jambo litawekwa wazi, punde mtagundua kuwa babu alipata ndoto ya kishetani...
 
Ukinywa au ukiwa na imani na kikombe cha babu huwezi kuona siri wala hatari. Giza la shetani linakufunika.

Nimekufuatilia sana kwa kuwa naamini una mafundisho ambayo siyo sahihi. Narudia kusema sijaenda kwa babu na hata hivyo siwabezi walioenda kwa sababu sina biblical basis ya kufanya hivyo.

Maandiko yote uliyokuwa unayachomoa kutoka kwa Yeremia yana historia yake kwa wakati ule. Ni vema ukaacha kupeleka maana kwenye maandiko. Acha andiko lijisemee lenyewe. Manabii wa wakati ule walizungumza na watu wale kwa wakati ule kwa mazingira na tatizo la wakati huo. Tunaposoma ni vizuri tukajua Mungu alikuwa anasema nao nini wakati ule huko. Na baada ya hapo, ndipo tuseme na sisi tunajifunza nini (au andiko hilo lina maana gani kwetu sisi sasa).

Sasa hivi tuko na hoja ya babu na tiba yake. Je maandiko yanakataza tiba ya miti shamba?

Nimesoma post zako na kuona umemtumia sana Yeremia. Naomba ufahamu Yeremia anataja habari ya dawa ya miti shamba (healing balm) walau mara tatu katika kitabu chake (Soma Yer 8:22; 46:11; 51:8). Gilead ilijulikana kwa kuwa na miti mingi ya tiba. Tunawaambiaje watu hao? Kuwa wayahudi wote hawakumjua Mungu? Tunasemaje pale Mungu anapowatuma wamisri waende Gilead kupata dawa?
Mwanzo 43:11 inasema: Hapo Israeli, baba yao, akawaambia, "Haya kwa kuwa ni lazima iwe hivyo basi, fanyeni hivi: chukueni katika mifuko yenu baadhi ya mazao bora ya nchi yetu, mkampelekee zawadi huyo mkuu. Mchukulieni mafuta kidogo ya mkwaju [healing balm], asali kidogo, ubani, manemane, kungu na lozi. Yakobo anawaambia watoto wake wampelekee Yusufu dawa ya miti shamba. Je, tumsemeje Yakobo hapa? Unahitaji kusoma maandiko zaidi.

Kwa taarifa yako vyakula vyote vya aina ya mbegu (matunda na mazao mengine) ni miti shamba. Kwa vile umeyazoea mahindi hayafanyi kuwa siyo mti shamba.
 
Kwa aliyeanzisha hii thread mimi nasema hivi......believe what you want to believe and let other people decide for themselves. Kila mtu atapima imani yake towards huyu Babu na ataamua kulingana na utashi wake! Going on and on about sijui mstari wa Bible unasema x, y and z isnt going to help much. If you think he is fake, ur point of view is noted and personally i respect ur views...but at the end of the day i will trust and believe what i want! Do i hear an AMEN?
 
Unabii hupimwa na neno la Mungu kama yardstick/kioo. Hivyo kama unabii unapingana na neno la Mungu, unabii huo huwa wa uongo. Biblia inasema MTAWEKA MIKONO JUU YA WAGONJWA, NAO WATAPATA AFYA, sasa hii staili mpya ya kikombe imetoka wapi? Ama kwa kuwa kina Askofu Laizer wamekwenda, na kina Sumaye na Lowasa ndio iwe sababu ya kuamini ndoto zake? Kila jambo litawekwa wazi, punde mtagundua kuwa babu alipata ndoto ya kishetani...

Wagonjwa wote makanisani na kwenye mikutano ya injili huwa wanawekewa mikono? Je, staili ya kuombea handkerchief imetoka wapi? Vipi staili ya kupiga power watu imetoka wapi?
 
Habari zilizoandikwa katika magazeti na kusikika katika redio na Televisheni siku kadhaa zilizopita zilieleza kwamba Babu wa Loliondo ameoteshwa na Mungu dawa ya kuwatibu watu magonjwa sugu.

Wachunguzi na wataalam wa masuala ya kiroho wamegundua kuwa ndoto hiyo ni ya uongo kulingana na Neno la Mungu katika kitabu cha Yeremia 23:25-32. Neno la Mungu (Biblia) katika mistari hiyo linasema hivi:
"Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto. Je, mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe? Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao...Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema BWANA...Basi kwa sababu hiyo...mimi [NIKO KINYUME]na manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema. Tazama, mimi [NIKO KINYUME] na hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA."

Katika mistari hiyo, BWANA Mungu anazifananisha ndoto na makapi. Hazina maana. Neno lake(ngano) ndilo lenye maana. Maandiko hayo yanaonyesha wazi kuwa Mungu hajamtuma babu kusema wala kufanya hayo anayoyafanya sasa na kwa sababu hiyo yuko matatani au hatarini maana Mungu yuko kinyume naye sasa.

Vyanzo vingine vya habari kutoka nje ya nchi, vimethibitisha kuwa huyo babu wa Loliondo ni nabii wa uongo. Vyanzo hivyo vinaeleza kuwa ukitaka kumtambua nabii wa uongo angalia mambo yafuatayo:

1. Mkazo wake hauko kwa Yesu, bali ni juu ya miujiza kama ambavyo babu asivyolitaja Jina la Yesu. Mkazo wa babu uko kwenye kikombe na huo mti. Watu wengi wanapoona miujiza (kama huo mti wenye sumu kutoweza kuua kama walivyozoea) wanakuwa wepesi kuamini kuwa Mungu ndiye anayefanya miujiza hiyo. Wanasahau kwamba hata waganga na wachawi wa Misri walitenda miujiza kama ile aliyotenda Mungu. Shetani anafanya miujiza na ataendelea kufanya hata zaidi ya huo wa kikombe. Soma 2 Wathesalonike 2:8-12.

2. Nabii wa uongo hufanya vitu ambavyo haviwezi kuthibitishwa na Neno la Mungu. Badala yake hutaja tu kwamba anafanya hivyo kwakuwa ameota ndoto au amefunuliwa. Katika Biblia tunaona kuwa Yesu alikuwa akiyathibitisha yale aliyokuwa akisema kwa kutaja neno "Imeandikwa". Babu hana ujasiri wa kusema "Imeandikwa, mtapona kwa mti wa mgariga" Hawezi, maana andiko hilo halipo.

3. Nabii wa uongo husema mambo yasiyotimia. "Atakaponena nabii kwa Jina la BWANA, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena BWANA; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope." Kum 18:22. Babu alisema wazi wazi kwamba dawa yake inaponya kabisa lakini baadhi ya wale waliokwenda kwake tayari wameishapoteza maisha yao baada ya kunywa dawa hiyo. Na wengine wanakiri kwamba hawajapona kabisa ila wanasikia nafuu tu!

4. Nabii wa uongo hawezi kuwahubiri watu kwa mkazo waache dhambi zao. "Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri. Lakini kama wangalisimama katika baraza yangu, ndipo wangaliwasikizisha watu wangu maneno yangu, na kuwageuza waziache njia zao mbaya, na uovu wa matendo yao(Yeremia 23:21-22). Babu wa Loliondo anakazana tu kugawa vikombe badala ya kuwahubiri mafisadi, makahaba, majambazi, watoaji wa mimba, wabakaji, wagomvi, wauache uovu wao. Manabii wa kweli wa Mungu(kama Eliya) pamoja na kutenda miujiza, walihubiri Neno la Mungu kwa ujasiri sana.

5. Nabii wa uongo hugeuza au kupinga baadhi ya Maneno ya Mungu. Babu wa Loliondo ni miongoni mwa wale wanaopinga ubatizo wa kibiblia wa maji mengi. Badala yake anatetea ubatizo wa watoto wadogo, jambo ambalo halimo katika Biblia. Yesu aliwabariki watoto, hakuwabatiza. Mtawatambua kwa matunda yao! Sio hilo tu anapinga pia agizo kuu la Yesu katika Marko 16:15-18. Katika mistari hiyo watumishi wa Mungu wameagizwa kwenda ulimwenguni mwote kuihubiri Injili na kuweka mikono juu ya wagonjwa ili wapate afya. Yeye babu kwa ukaidi alionao toka 1991, badala ya kutoka na kwenda katika miji na vijiji (kama Yesu alivyofanya - Mt 9:35) ili kuwahubiri wenye dhambi na kuwapoza wagonjwa (walioko Shinyanga, Kigoma, Rukwa, Namibia nk nk), eti ameamua kujenga makao ya kudumu huko huko porini. Hataki kutoka, halafu anasema Mungu amemtuma. Mungu hawezi kupingana na Neno lake.

6. Nabii wa uongo hunukuu pia maneno ya Mungu. Asilimia kama 95 yanakuwemo kwenye Biblia lakini asilimia kama 5 ni uongo. Shetani alipowadanganya Adam na Hawa alitumia pia maandiko . Hata alipomjaribu Yesu alisema imeandikwa. Mathayo 4:6-7. Yesu alijua lengo lake ni baya akampinga. Babu naye vivyo hivyo, akiwa kanisani Jumapili ananena maneno ya Mungu lakini asilimia kama 5 ya yale anayoyasema yako kinyume na Biblia. Yesu aliwapa wanafunzi wake amri ya kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Yeye babu anasema anatibu magonjwa sugu tu.

7. Nabii wa uongo hugeuza huduma kuwa biashara, ingawa hapendi ajulikane kuwa anafanya biashara. Miujiza na karama za Mungu hazitolewi kamwe kwa pesa. Yesu aliwaambia hivyo wanafunzi wake pale alipowapa uwezo wa kuponya. Katika Mathayo
10:8 anasema: "Pozeni(ponyeni) wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure." Hiyo sh 500 anayotoza babu kwa kila mgonjwa sio sadaka kama yeye anavyodai. Sadaka haina masharti. Sadaka hutolewa kwa hiari na kwa moyo wa kupenda (Kutoka 35:29). Si kwa kulazimishwa. Kwa babu usipotoa hiyo 500, kikombe hupati! Babu anadai kwamba maelfu ya watu wanaokwenda kwake sasa hivi ni sehemu ndogo tu maana watu watatoka pande zote za dunia. Dunia ina watu zaidi ya bilioni 6. Hebu sasa jaribu kuwaza, iwapo watu bilioni moja tu duniani kote wanaumwa magonjwa sugu, wakija Tanzania na babu akawatoza sh 500, mwisho wa siku atakuwa amepata sh ngapi? 500x1,000,000,000=??? Kama huo sio wizi wa mchana ni nini? Ndio maana ameibuka nabii mwingine wa uongo, Rombo, na yeye anadai ameoteshwa atoe dawa kwa kipimo cha vikombe viwili. Watanzania, tuamke! Tuwe macho! Hata wenye digrii moja, mbili, tatu, tunakubali kudanganyika kirahisi namna hiyo? Na usomi wetu?

Babu anasema watu wengi(+wazungu) watatoka nje ya nchi kuja kupata kikombe. Sidhani kama wazungu waliostaarabika wana muda wa kupanga foleni siku 7 wakingojea kwenda kwa babu. Sijui pia kama wazungu waliostaarabika watakuwa tayari kukaa mahali pasipo na vyoo au kwenda kujisaidia porini. Labda wazungu anaowasema ni wale watakaokuja kufanya utafiti kuhusu utendaji kazi wa waganga wa kienyeji na kwanini Watanzania tunaishi kwa dhiki kubwa huku tuna mlima mrefu kuliko yote Africa, madini ya Tanzanite,mbuga nzuri za wanyama, nk, nk, nk.

Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo [wanaonekana watulivu kama babu alivyo] lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali...Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako...kufanya miujiza...ndipo nitawaambia dhahiri, sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Kumbe miujiza peke yake sio ishara kuwa aitendaye ametumwa na Mungu.

Pinga, usipinge, babu wa Loliondo ametumwa na shetani, baba wa uongo na lengo lake ni kuwafanya watu walisahau Neno la Mungu, wasahau ahadi za Mungu, wadharau uponyaji wa kweli unaopatikana katika Yesu Kristo, waweke matumaini yao kwenye kikombe badala ya kumtumaini Mungu, hatimaye siku ile ya mwisho waangamie katika moto wa milele.

"AONYWAYE MARA NYINGI AKISHUPAZA SHINGO, ATAVUNJIKA GHAFLA..." Mithali 29:1.
Nawachia wadau ama kwa upande nilko mimi kwanza manabii wameshakwisha,pili dawa za mitishamba si miujiza bali ni dawa za kawaida na suwala la ndoto ni ndoto tu Mungu hana haja ya kumjia mtu hivi sasa kwani alishakamilisha maamrisho yake na hata hapo alipokuwa akileta basi alitumia malaika.
 
kama babu ni nabii wa uongo na anafuatwa na watu wengi namna hii wenye kuhitaji uponyaji wa magonjwa ya miili yao, basi ujue kwamba taifa hili halina nabii wa kweli hata mmoja kwa sasa. Kama wangilikuwepo na kupewa uwezo wa kuwaponya watu maradhi yao kwa neno la Yesu, hawa wanaomwendea babu wangetoka wapi?
Kwa habari ya babu kutoza 500, sijui kama hilo ni tatizo. Litakuwa tatizo ikiwa atajitokeza mtumishi mmoja tuu katika taifa letu mwenye kanisa na kwa uaminifu akanushe kwamba gherama za maisha yake hazina hata senti moja ya pesa zilizotoka kwa wafuasi wa kanisa.
Hapo babu atakuwa na hatia kumsemea mungu ambaye wale wanaompinga hawanae.
.
 
Sasa Babu si hataki jamani???? nenda ujaribu kumpa gari kama atakubali ...............amesema Mungu wake kamkataza!!!!!!!!!!! Mungu gani anayekukataza usifanikiwe????? Mungu wa Kweli anabariki na kuinua; anabadilisha maisha ....sasa anayemkataza Babu ni Mungu kweli au ni mungu yupi???? nauliza!!!

Kumbe hivi ndivyo mnavyoelezwa huko kanisani kwenu. 'Ole wenu maana ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuuona ufalme wa mbinguni''
 
Habari zilizoandikwa katika magazeti na kusikika katika redio na Televisheni siku kadhaa zilizopita zilieleza kwamba Babu wa Loliondo ameoteshwa na Mungu dawa ya kuwatibu watu magonjwa sugu.

Wachunguzi na wataalam wa masuala ya kiroho wamegundua kuwa ndoto hiyo ni ya uongo kulingana na Neno la Mungu katika kitabu cha Yeremia 23:25-32. Neno la Mungu (Biblia) katika mistari hiyo linasema hivi:
"Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto. Je, mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe? Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao...Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema BWANA...Basi kwa sababu hiyo...mimi [NIKO KINYUME]na manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema. Tazama, mimi [NIKO KINYUME] na hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA."

Katika mistari hiyo, BWANA Mungu anazifananisha ndoto na makapi. Hazina maana. Neno lake(ngano) ndilo lenye maana. Maandiko hayo yanaonyesha wazi kuwa Mungu hajamtuma babu kusema wala kufanya hayo anayoyafanya sasa na kwa sababu hiyo yuko matatani au hatarini maana Mungu yuko kinyume naye sasa.

Vyanzo vingine vya habari kutoka nje ya nchi, vimethibitisha kuwa huyo babu wa Loliondo ni nabii wa uongo. Vyanzo hivyo vinaeleza kuwa ukitaka kumtambua nabii wa uongo angalia mambo yafuatayo:

1. Mkazo wake hauko kwa Yesu, bali ni juu ya miujiza kama ambavyo babu asivyolitaja Jina la Yesu. Mkazo wa babu uko kwenye kikombe na huo mti. Watu wengi wanapoona miujiza (kama huo mti wenye sumu kutoweza kuua kama walivyozoea) wanakuwa wepesi kuamini kuwa Mungu ndiye anayefanya miujiza hiyo. Wanasahau kwamba hata waganga na wachawi wa Misri walitenda miujiza kama ile aliyotenda Mungu. Shetani anafanya miujiza na ataendelea kufanya hata zaidi ya huo wa kikombe. Soma 2 Wathesalonike 2:8-12.

2. Nabii wa uongo hufanya vitu ambavyo haviwezi kuthibitishwa na Neno la Mungu. Badala yake hutaja tu kwamba anafanya hivyo kwakuwa ameota ndoto au amefunuliwa. Katika Biblia tunaona kuwa Yesu alikuwa akiyathibitisha yale aliyokuwa akisema kwa kutaja neno "Imeandikwa". Babu hana ujasiri wa kusema "Imeandikwa, mtapona kwa mti wa mgariga" Hawezi, maana andiko hilo halipo.

3. Nabii wa uongo husema mambo yasiyotimia. "Atakaponena nabii kwa Jina la BWANA, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena BWANA; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope." Kum 18:22. Babu alisema wazi wazi kwamba dawa yake inaponya kabisa lakini baadhi ya wale waliokwenda kwake tayari wameishapoteza maisha yao baada ya kunywa dawa hiyo. Na wengine wanakiri kwamba hawajapona kabisa ila wanasikia nafuu tu!

4. Nabii wa uongo hawezi kuwahubiri watu kwa mkazo waache dhambi zao. "Mimi sikuwatuma manabii hao, lakini walikwenda mbio; sikusema nao, lakini walitabiri. Lakini kama wangalisimama katika baraza yangu, ndipo wangaliwasikizisha watu wangu maneno yangu, na kuwageuza waziache njia zao mbaya, na uovu wa matendo yao(Yeremia 23:21-22). Babu wa Loliondo anakazana tu kugawa vikombe badala ya kuwahubiri mafisadi, makahaba, majambazi, watoaji wa mimba, wabakaji, wagomvi, wauache uovu wao. Manabii wa kweli wa Mungu(kama Eliya) pamoja na kutenda miujiza, walihubiri Neno la Mungu kwa ujasiri sana.

5. Nabii wa uongo hugeuza au kupinga baadhi ya Maneno ya Mungu. Babu wa Loliondo ni miongoni mwa wale wanaopinga ubatizo wa kibiblia wa maji mengi. Badala yake anatetea ubatizo wa watoto wadogo, jambo ambalo halimo katika Biblia. Yesu aliwabariki watoto, hakuwabatiza. Mtawatambua kwa matunda yao! Sio hilo tu anapinga pia agizo kuu la Yesu katika Marko 16:15-18. Katika mistari hiyo watumishi wa Mungu wameagizwa kwenda ulimwenguni mwote kuihubiri Injili na kuweka mikono juu ya wagonjwa ili wapate afya. Yeye babu kwa ukaidi alionao toka 1991, badala ya kutoka na kwenda katika miji na vijiji (kama Yesu alivyofanya - Mt 9:35) ili kuwahubiri wenye dhambi na kuwapoza wagonjwa (walioko Shinyanga, Kigoma, Rukwa, Namibia nk nk), eti ameamua kujenga makao ya kudumu huko huko porini. Hataki kutoka, halafu anasema Mungu amemtuma. Mungu hawezi kupingana na Neno lake.

6. Nabii wa uongo hunukuu pia maneno ya Mungu. Asilimia kama 95 yanakuwemo kwenye Biblia lakini asilimia kama 5 ni uongo. Shetani alipowadanganya Adam na Hawa alitumia pia maandiko . Hata alipomjaribu Yesu alisema imeandikwa. Mathayo 4:6-7. Yesu alijua lengo lake ni baya akampinga. Babu naye vivyo hivyo, akiwa kanisani Jumapili ananena maneno ya Mungu lakini asilimia kama 5 ya yale anayoyasema yako kinyume na Biblia. Yesu aliwapa wanafunzi wake amri ya kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Yeye babu anasema anatibu magonjwa sugu tu.

7. Nabii wa uongo hugeuza huduma kuwa biashara, ingawa hapendi ajulikane kuwa anafanya biashara. Miujiza na karama za Mungu hazitolewi kamwe kwa pesa. Yesu aliwaambia hivyo wanafunzi wake pale alipowapa uwezo wa kuponya. Katika Mathayo
10:8 anasema: "Pozeni(ponyeni) wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure." Hiyo sh 500 anayotoza babu kwa kila mgonjwa sio sadaka kama yeye anavyodai. Sadaka haina masharti. Sadaka hutolewa kwa hiari na kwa moyo wa kupenda (Kutoka 35:29). Si kwa kulazimishwa. Kwa babu usipotoa hiyo 500, kikombe hupati! Babu anadai kwamba maelfu ya watu wanaokwenda kwake sasa hivi ni sehemu ndogo tu maana watu watatoka pande zote za dunia. Dunia ina watu zaidi ya bilioni 6. Hebu sasa jaribu kuwaza, iwapo watu bilioni moja tu duniani kote wanaumwa magonjwa sugu, wakija Tanzania na babu akawatoza sh 500, mwisho wa siku atakuwa amepata sh ngapi? 500x1,000,000,000=??? Kama huo sio wizi wa mchana ni nini? Ndio maana ameibuka nabii mwingine wa uongo, Rombo, na yeye anadai ameoteshwa atoe dawa kwa kipimo cha vikombe viwili. Watanzania, tuamke! Tuwe macho! Hata wenye digrii moja, mbili, tatu, tunakubali kudanganyika kirahisi namna hiyo? Na usomi wetu?

Babu anasema watu wengi(+wazungu) watatoka nje ya nchi kuja kupata kikombe. Sidhani kama wazungu waliostaarabika wana muda wa kupanga foleni siku 7 wakingojea kwenda kwa babu. Sijui pia kama wazungu waliostaarabika watakuwa tayari kukaa mahali pasipo na vyoo au kwenda kujisaidia porini. Labda wazungu anaowasema ni wale watakaokuja kufanya utafiti kuhusu utendaji kazi wa waganga wa kienyeji na kwanini Watanzania tunaishi kwa dhiki kubwa huku tuna mlima mrefu kuliko yote Africa, madini ya Tanzanite,mbuga nzuri za wanyama, nk, nk, nk.

Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo [wanaonekana watulivu kama babu alivyo] lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali...Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako...kufanya miujiza...ndipo nitawaambia dhahiri, sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Kumbe miujiza peke yake sio ishara kuwa aitendaye ametumwa na Mungu.

Pinga, usipinge, babu wa Loliondo ametumwa na shetani, baba wa uongo na lengo lake ni kuwafanya watu walisahau Neno la Mungu, wasahau ahadi za Mungu, wadharau uponyaji wa kweli unaopatikana katika Yesu Kristo, waweke matumaini yao kwenye kikombe badala ya kumtumaini Mungu, hatimaye siku ile ya mwisho waangamie katika moto wa milele.

"AONYWAYE MARA NYINGI AKISHUPAZA SHINGO, ATAVUNJIKA GHAFLA..." Mithali 29:1.


  • Manabii wa uwongo ni hawa wanaoanzisha makanisa yao katika hii karne ya 21. Babu hajaanzisha kanisa
  • Ninachoweza kuwashauri wamiliki wa makanisa ya maombezi/kiroho ni kuweka mkakati wa kuwavutia watu wasio na shida waje makanisani. Muache kupita mahospitalini na kuwarubuni wagonjwa, hamuwatendei haki. Wafateni watu wenye afya zao wajiunge na makanisa yenu, hapo hamtapata mtikisiko hata akitokea nani. Hii ndio sababu ya uimara au ukubwa wa makanisa kama ya KKKT, RC, Anglikana, Sabato nk.
 
kama babu ni nabii wa uongo na anafuatwa na watu wengi namna hii wenye kuhitaji uponyaji wa magonjwa ya miili yao, basi ujue kwamba taifa hili halina nabii wa kweli hata mmoja kwa sasa. Kama wangilikuwepo na kupewa uwezo wa kuwaponya watu maradhi yao kwa neno la Yesu, hawa wanaomwendea babu wangetoka wapi?
Kwa habari ya babu kutoza 500, sijui kama hilo ni tatizo. Litakuwa tatizo ikiwa atajitokeza mtumishi mmoja tuu katika taifa letu mwenye kanisa na kwa uaminifu akanushe kwamba gherama za maisha yake hazina hata senti moja ya pesa zilizotoka kwa wafuasi wa kanisa.
Hapo babu atakuwa na hatia kumsemea mungu ambaye wale wanaompinga hawanae.
.

Kuna better life in christ kuliko huko kuponywa na dawa ya Babu na kesho unaugua mafua, malaria, typhoid etc kweli ikiingia ndani yako basi ugonjwa ukigusa mwili wako wenyewe una surrender na kupiga magoti nimekoma sinta rudi tena. Kwanini ukapange foleni na wengine kufa kabla ya kupata kikombe cha Babu huku unaweza tu ukajiwekea mwenyewe maji free kutoka kwa Yesu just from the atmosphere? Its possible to live such kind of life thats the whole mission of why Christ came and died for us.

Pata shule hapa;

|| Pastor Chris Online - Channel ||


|| Pastor Chris Online - Channel ||

Do you want to live in the night of your life of day of your life?

I choosed to live in the day of my life and am preaching so that others may discover themselves and come out of their dark life to the greater life where they would enjoy life in sunshine.
 
Mada hii ni nzuri. Wewe ni jasiri najua hutaumia wala kukata tamaa kwa matusi yanayofuata. Umesema kweli unayoiamini bila kuogopa kwa sababu unajua unachokifanya.

Ninachoona mimi, watu hawana sababu ya kutetea kwamba Loliondo kuna Mungu. Hilo jambo ni gumu kulisema kwa kuimba kama kibwagizo kama kweli mtu unamaanisha. Ninaomba wapenzi wa babu wasitoe matusi. Mbona yeye hatukani? Ninachokijua mimi wengi wanakwenda kule kutafuta uponyaji wa mwili na wala siyo kumtafuta Mungu. Na hata babu mwenyewe sijasikia anahusisha dawa zake na msamaha wa dhambi wala utakatifu. Hivyo watu wanaenda kunywa dawa sawa kama wangeambiwa imegunduliwa katika kitengo cha tiba za asili muhimbili, au ni ya nchi fulani, ama dawa za wachina. Bahati mbaya sana tukienda huko tulikokuzoea kutibiwa hatuulizagi hayo madawa asili zake nini. Mimi binafsi sitaki kuoanisha madawa na uwepo wa Mungu.

ILA KWA HABARI YA IMANI, NAWAAMBIA BINADAMU WAACHE DHAMBI NA WALA WASIMTUMAINIE BABU WA LOLIONDO WALA MTU YEYOTE MAANA NI WANADAMU WAKUPITA NA WOTE WAKO CHINI YA SHERIA YA MUNGU.

HAIJALISHI WANAUMWA AMA NI WAZIMA. WAMETIBIWA LOLIONDO, HOSPITALINI AMA KWA WAGANGA WAKIENYEJI WANAPASWA KUMUISHIA MUNGU. KUFA KUPO TU NA NI MARA MOJA. BAADA YA KIFO NI HUKUMU. SASA HAITASAIDIA KAMA MTU UNAKUFA KATIKA DHAMBI KWA SABABU YA MAISHA HAYA MAFUPI HALAFU UNAPOTEZA UMILELE WAKO. NAOMBA WATU WOTE WAMPOKEE BWANA YESU KRISTO KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAO MAANA YEYE NDIYE NJIA KWELI NA UZIMA. NA MTU HAFIKI KWA MUNGU ILA KWA NJIA YA YESU KRISTO PEKE YAKE.
NAWASILISHA.
 
Back
Top Bottom