ni usiku wa kama saa tano ivi namsikia mama akilia kwa uchungu wa kupigwa na kiatu cha baba.....mama anakimbilia kwa watoto baada ya kuona kipigo kimezidi,kwa wakati huo nilikua mdogo wa kama miaka 5 ivi na nililala na dada yetu wa kazi na mdogo wangu wa kike..[uhaba wa vyumba].....kama vile haitoshi baba alivamia chumbani na kuendelea kumpiga mama..nililia sana kwa wakati huo nilichoweza kukifanya ni kufungua mlango alioufunga baba na kuweka mazingira ya mama kutorokea nje mimi na yeye........nakumbuka siku hiyo nilikaa nje tangu saa sita hadi saa 8 huku mvua ikitunyeshea..........na mama alivimba mwili mzima..
baba alifunga milango yote akalala....baadae nilimwomba dada yetu afungue kwa taratibu maana baba alikua akikoroma hivyo kutosikia..nikaingia ndani na mama tukalala........tulijifungia mlango nakumbuka..
asubuh baba alikuja kugonga mlango,haukufunguliwa aliishia kuuvunja na kisha kumhoji mama kwa nini amelala kwa watoto.......akampiga makofi na kisha kwenda zake kazini........
nakumbuka nilikua kindergaten,na mama yangu ndie aliyenipeleka........
vipigo hivi viliendelea siku hadi siku pamoja na vikao kuwekwa mara kwa mara........ila tulikuja kugundua baadae alikua n amwanamke mwingine..na siku akienda huko akirudi ni lazima mama apigwe.Mama alikua mvumilivu sana,si kwa ajili yetu tu bali pia alikua ni mtu wa kusamehe haraka sana,alikua na moyo wa upendo wa hali ya juu
baba alitangulia mbele za haki mwaka 2011.........apumzike kwa amani,japo pengo lako bado lipo ila baba ulikua katili sana kwa mama.Mungu akusamehe kwa hilo...
Nimejifunza mengi sana kwa experience ile ya maisha,namshukuru Mungu kama mwanaume/kijana ninayejiamini na kujitambua..........nina familia [ndoa rasmi mwaka huu],elimu,kazi na kikubwa upendo na heshima si kwamke wangu tu bali pia kwa wanawake wote....nawapa pole wanawake wote wanaopitia magumu yasababishwayo na sisi wanaume......wazidi kumuomba Mungu wao nakuwa wavumilivu.......haya ni mapito tu,twautafuta mji udumuo!!
WANAUME TUBADILIKE TUACHE UNYANYASAJI WA NAMNA YEYOTE ILE.