baba yangu alivyomtesa mama yangu

baba yangu alivyomtesa mama yangu

Wanaume wengi wanachukulia vipigo kwa wake wazao kama ubabe hivi. Wanataka kutengeneza woga kwa wake zao ili wafanye mambo yao kwa uhuru. Wanasahau kuwa mke ni mtu mzima mwenzie hata kama kuna tatizo au kakukosea ni vema mkakaa na kujadili tatizo liko wapi. Nakupongeza sana kwa kuona tatizo la baba yako. Endelea kuwa na tabia njema.
 
Inasikitisha sana kuwa umesubiri baba yako kafa ndo umeleta hii habari. Ulipata kuongea na mama yako akapata kufahamu kuwa una post mgogoro huu hapa? Umepata kujua mama yako ametoa msamaha wa aina gani kwa baba?. Ingelikua wewe ndiyo mama, au ikiwa mama asingelikuwepo ungelimpokea na kumlea baba ktk hali yake ya kuumwa licha ya uovu wake kwa mama?
Ni vema na ingekuwa heri kwa kila mmoja ndani ya familia ungeliongea na baba akiwa hai, ungemuonyesha madhara ya matendo yake na kisha kutangaza kumsamehe.amekufa ndo unakuja kuiambia jamii forums tena na kuaidi wewe unajiandaa kuwa mume mwema, haisaidii kwani baba amekufa, chanzo cha magomvi yake na mama walijua wao, wewe unachojua ni effects za huo ugomvi. Hekima na busara zituongoze zaidi kuliko hisia. Amini nakwambia kwa kujua makosa ya hayat baba yako na kuya sema hapa jf haitoi tiket ya amani ktk ndoa yako, lakini kwa kujua makosa ya baba na kuchanganya na hekima ya mama yako ingekuwa si raisi kuandika hbr inayomsema mfu,
 
Wengi tumeathirka na mifumo ya maisha baba zetu(all things remaining constant)..
kuna mengi ambayo leo hii tunaogopa kufanya kisa tu ni memories za utotoni kuhusu mahusiano ya wazazi wetu
Nimeona watu wazima ambao wameweka chuki za ajabu towards their fathers(mostly) na kwakweli sio healthy..kuna mmoja amesema kutokuingilia mahusiano ya wazazi(wao ndo wanajua sabb) ila umeshindwa tu kutambua kama familia,mtoto huathirika zaidi ya mahusiano ya wazazi kuliko wazazi wenyewe..kumpiga mwanamke sio solution ya matatizo yenu,wote ni watu wazima(above 18yrs hopefully),ni kama kunywa pombe kwa mentality ya kuondoa mawazo while asubuhi matatizo yapo the same..
nje ya mada:without research wengi ya wananaume wanaopiga wenzi wao cant fight with wanaume wenzao,they are weaklings in a way
 
Back
Top Bottom