mij
JF-Expert Member
- Mar 22, 2013
- 1,993
- 2,106
WanaJF,
Hivi ni kweli anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga? Kama maneno haya ni kweli basi namwomba mwenyezi Mungu yatimie kwa wale wote wanaolihujumu taifa hili kwa kuwakandamiza wanyonge na kutumia mamlaka waliyonayo kupindisha sheria,kusingizia watu na kutengeneza matukio au kesi zisizo za kweli ili wapate kufungwa magerezani!
Wanamuziki ambao ni baba na mwana,Nguza Viking na Papii Kocha mpaka sasa wanatumikia vifungo vya maisha baada ya kusingiziwa kuwalawiti watoto wanafunzi wa shule ya msingi huko Sinza! Katika kesi ambayo kwa sasa inaonekana kusahaulika taratibu kama ilivyo kawaida yetu, mwanasheria maarufu nchini Mabere Marando aliweza kuwatoa katika kifungo cha maisha watoto wawili wa Nguza Viking waliokuwa wamefungwa gerezani pamoja na baba yao!
Mpaka sasa haijulikani ni nani aliyeshinikiza na kuitengeza kesi iliyopelekea familia ya Nguza Viking kupatwa na masaibu haya ya kufungwa maisha gerezani! Ni nani mtu huyu aliyefanya yote haya? Bila shaka atakuwa ni mtu asiye na huruma na hatari sana! Kuna utata mkubwa katika kesi hii kwani mwalimu aliyesemekana kuwa ndiye aliyekuwa akiwapeleka watoto wanafunzi kulawitiwa nyumbani kwa Nguza Viking aliachiwa huru kisha baadaye alihama shule na kwenda kusikojulikana!
YULE MWALIMU YUPO MAENEO YA KIMARA/MBEZI ANAKULA KUKU.
"hii avatar yako mbona inatisha sana"