Baba Mkwe wangu ananitishia NISHAURINI


Tunaishi as brother and sister na hataki yuko busy na kazi za ofisini hadi nyumbani, kachoka kila wakati. amepoteza sifa za kuwa mke na ana qualify kuwa mama ama dada yangu why should we stay in the same bedroom.
 
Pole sana,inaelekea hao wazazi wake wanafanana tabia na mtoto,toto limeshindikana kwao sasa wanataka kukusukumizia,hapo we ongea na wazazi wako kuhusu hivyo vitisho then kuwa mwanaume hata wao wako kwenye familia yao hakuna aliewavunjia mlango,weka msimamo kama hawataki amani peleka polisi na uyo wife fukuza kuna kitu kinampa kiburi,miaka tisa mkuu si bora ukae alone bhana kamtu kamoja kanakuzingua,mpeleke somewhere akaone wadada asifikiri yupo mwenyewe...
 
Tunaishi as brother and sister na hataki yuko busy na kazi za ofisini hadi nyumbani, kachoka kila wakati. amepoteza sifa za kuwa mke na ana qualify kuwa mama ama dada yangu why should we stay in the same bedroom.
Labda ana jini mahaba,ungejaribu kumpeleka kwenye maombi,ina maana hakutamani kabisa,hata ukimchokoza hataki,BIBLIA inasema msinyimane,pole sana kwa kweli
 
Pole sana kweli ndoa ni wakati mgumu, ila naona wewe pia ulikosea miaka 9 kukaa na kasoro usizoziripoti kwao, hivyo wameona kama ndoa ilikuwa ya heri ila ghafla umeamua kumfukuza..... Pili ulipaswa kumpigia mzazi hasa mama kumweleza matatizo yenu na kuwa unaomba huyo arudi hadi mje mjieleze wote wawili maana wazee wa watu kukuta binti kajaa nyumbani kisa kafukuzwa kwa mume wa ndoa njema ya miaka 10 si haba....Tatu ndugu yangu kuwa mpole na kama unaitaka ndo ana familia yako itabidi unyenyekee tu maana inaonekana ukoo uliooa ndo ulivyo hivyo uombe tu Mungu mkeo awe na afadhali mbeleni. Kutunza hasira na kinyongo miaka 9 naona umekwenda kuimwaga kwa wazazi ambao hukuwahi kuwashirikisha tatizo toka mwanzo, ndio reaction yao hiyo, hivyo kwa unyenyekevu nenda kakae usuluhishwe.
 
Kosa ulilolifanya ni moja tu ungeenda kwanza kwa wakwe zako na ukaongea nao kwa kirefu na ukawaelezea matatizo ya mtoto wao kisha wao wangemuita mke wako wangemueleza yale uliyowaambia na yeye angeeleza yake ya moyoni
wazazi wangejua kabisa kwamba nani ana makosa na nani yupo sahihi kumbuka kuwa wale ni wazazi wenu wapo kwenye ndoa muda mrefu wamepitia mengi
lakini kitendo cha kumrudisha kwao bila taarifa yoyote sio kizuri hebu chukulia kwamfano wewe una mtoto wa kike ameolewa zaidi ya miaka 9 alafu gafla upo nyumbani unamuona anarudi na mabegi unamuuliza vp anakuambia nimeambiwa nirudi nyumbani, kama ni wewe ungejisikiaje na ungechukua maamuzi gani jaribu kufikiri tu

chunga sana ushauri utakaopewa kwa kipindi hiki na usifanye maamuzi yoyote magumu ukiwa na hasira mwisho wake ni majuto
Kwenye RED nafikiri ingekuwa solution na hata mimi nilitaka ikiwa vipi niwe free ili wife awe huru ku exercise tabia zake hizo kwa uhuru bila kuingiliwa. Iweje wang'ang'anize kurudi kama vile nao hawamhitaji?
 
Maandiko yanasema tuishi na wanawake kwa akili Ephesians 5:25
Nlivosoma ulichoandika nimekuelewa wewe ni wale wanaotaka kunyenyekewa na mke kama mfalme na hutaki hata kujisaidia mwenyewe.
wewe unataka mke akufanyie kila kitu hutaki kutoa mkono wako kusaidia shughuli za ndani...
Jiulize haya
Unasubiri mkeo akupikie kila siku akuwekee mezani akupakulie?
unasubiri kuwekewa maji bafuni kila siku na ikiwezekana uogoshwe
unataka mkeo ahangaike na watoto kila siku hutaki hata kuogesha mwanao na hata asbh kusaidiana pia.
Unataka kunyooshewa nguo kila siku, kufuliwa hutii mkono kusaidia..
Kama una tabia kama hizi utamwona mkeo ana kiburi dharau na jeuri..
saidiana na mkeo katika shughuli zote za ndani
.
Mfumo dume umeshapitwa na wakati na sidhani kama una mamlaka ya kumfukuza mke kinyemelea arudi kwao
wakwezo wana haki ya kukukoromea kwa jeuri na ubabe wako.
labda niseme nimeishi na jamii ambazo mwanaume ndie anamtumikia mwanamke kwa upendo, kupika kupakua,kuandaa nguo ni shughuli ya kila mmoja kivyake.
hakuna kumtegemea mwenza akufanyie kila kitu na kama wote mnafanya kazi hiyo kejeli au kiburi hutaiona kwa mwenzako kwani kila mmoja atawajibika kwa mwezio inapowezekana na sio kunyenyekewa kama mfalme
 
ameshndwa masharti??? Kwani we mganga ndugu? Hayo masharti yanawabana wote au upande mmoja, yaani mke peke yake. Kwani maana ya "kuoana" ni nin? Wazazi wake kama ni kukaa na mtoto wao na kumfunza walishafanya miaka kibao iliyopta kabla hujafungua mikono yako kumpokonya toka kwa wazazi. Sahv yeye ni mzgo wako na wewe ni mzgo wake. Umemshndwa kabisa mpe talaka ya moja kwa moja ijulikane, sio eti akafundshwe na wazazi. Kwani ungewaita wazazi wake kwako na kuwaeleza matatzo yenu wakawashauri ingekuwaje?
 
Kama umehamia kwake mlivyofunga ndoa,mkahitilafiana akakufukuza utang'ang'ania(sio lazima akurudishe kwa wazazi)
 
Last edited by a moderator:
Inawezekana mwenye tatizo ni mkeo;
Lakini hata wewe baba unalo tatizo;

Mke amekusumbua muda mrefu ....pole
Kwao ni jirani sana na hapo kwako;
Kwanini usichukue ujasiri wa kumtuma kwanza
mshenga au mzee yeyote mtu mzima ili akaongee na
wazazi wa mkeo huku mkitaka kuonana na wazazi kwa ajili ya suluhu ya masuala
yenu ya ndoa.

Wazazi wa mke wanaona kwamba umewadharau kwa kuwa hawajawahi
kusikia malalamiko yanayohusu binti yao na kama yapo hawajapelekewa
rasmi.

Hata hivyo walikustahi sana ilitakiwa siku ile ile huyo mkeo arudishwe
kwako akiwa amesindikizwa na mtu ili muyasuluhishe.

Baba mkwe anaona umemtukana kumrudishia binti yake;
ili akalala kwake wakati ni mke wa mtu.
 
Tunaishi as brother and sister na hataki yuko busy na kazi za ofisini hadi nyumbani, kachoka kila wakati. amepoteza sifa za kuwa mke na ana qualify kuwa mama ama dada yangu why should we stay in the same bedroom.
Kweli huo mpingo,pole sana...
 
mmh km anakunyma unyumba na bado anakiburi huyo atakua na mtu anayempa kiburi na alikubali kuolewa na ww with a reason out of love kitu ambacho nikibaya sana kwa mustakbali wa ustawi wafamilia yenu na afya yako kipsychology na maradh mengneyo so fikiri na uchukue hatua za kiujasiri. Pia toka awali alijua tabia za wazaz wake na ndo mana alikuwa anaenda kwa wazaz wko
 
Uvumilivu ukizidi sana (miaka 9?) unageuka kuwa -----...Kwenye scenario yako wewe ni -----!!

Pia kuna wakati lazima itifaki na taratibu zivunjwe ili usonge mbele...fanya hivyo kwani unazo sababu makusudi.

Kuwa na msimamo...wakivunja mlango,watie lupango wakwe na binti yao.

Swali...je mmezaa nae watoto?
 
Anakwambia wanaishi as brother and sister "NO GAME"teh teh teh,anaquality zote za dada au mama ake,maisha gani ayo
 

Umenikumbusha kisa cha jamaa mmoja alimchapa makofi baba mkwe, Baba mkwe akapiga marufuku bintiye kurudi kwa mmewe vinginevyo ana mlaani. Baadae mme na nduguze walikuja omba msamaha yakaisha.
 
 
Yaani umeandika nilichokuwa niandike baada ya kusoma sababu ya kufukuzwa, pamoja na kusaidiana unataka mfumo dume wakati wewe mwenyewe unahitaji mchango wake ktk pato? inaonyesha anafanyakazi na bado nyumbani kuna kazi nawe wataka kutumikiwa labda ndio maana ulikuwa na kigugumizi kupeleka mashtaka kwao toka mwanzo? Pamoja na ubabe wao lakini unapaswa kujua hata kisheria huyo hapo ni kwake sasaivi 10 years unasema unamrudisha kwao? ingekuwa 1 year sawa tungesema habebeki ila kuwa mkweli ndani ya moyo wako. Na ujue utakaowapata wanaweza wasikae hata mwaka. Chunga sana ndoa sio ya ukoo kaa angalia mapungufu yako na si baba, dada au mama wanasema nini.
 
Hizi ndoa hizi,,,,,! Asprin kwa hisani ya al-shabaab, kuja pande hizi mume wa ujana wangu japo niku-hug tu!
 
Last edited by a moderator:
 
Kama umehamia kwake mlivyofunga ndoa,mkahitilafiana akakufukuza utang'ang'ania(sio lazima akurudishe kwa wazazi)

mimi kwanza sijawahi hamia kwa mme wangu,nimemkuta kapanga,tukajenga wote na tukahamia kwenye nyumba yetu wote,eti anifukuze,labda yeye ndo aondoke,siwezi ondoka kwenye mjengo ambao na mimi nimeshiriki kujenga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…