Baba Mkwe wangu ananitishia NISHAURINI

Baba Mkwe wangu ananitishia NISHAURINI

Mkuu kwa sasa ni rahisi sana kusema chochote kwa kuwa kile unachofikiria kuwa unakihitaji kwa mwanamke unakipata wakati wowote unaotaka, Kiranga hujapata kibano cha maisha na ukaona kuwa hawa watu tunawahitaji kwa kiasi gani? kama wenza katika maisha.Mwanamke ni zaidi ya unavyofikiria. Sijui umezaliwa na kulelewa katika mazingira gani? Lakini embu fikiria kama baba yako angeishi kama wewe!! leo hii kiranga ungekuwa na Kiranga??
Kutofautiana katika maisha ya ndoa sio jambo geni ni kawaida tu kila binadamu ana mapungufu yake, pale mwenzanko anapoishia we anzia hapo! jazia mapungufu yake, na maisha husonga mbele

Kwa hiyo unaona ndoa ni nzuri kwa sababu ya kibano cha maisha? Na kama hakuna kibano cha maisha?
 
Mimi naona kama ulifanya kosa kumrudisha kwao kabla hujawaeleza wazazi wake tatizo ni nini. wao hawana taarifa za upande wako wana za mtoto wao tu. Isitoshe suala hili si la wazazi wake peke yao. Nadhani ungemshirikisha mshenga wako pamoja na wazee wa busara wakusaidie. Wazazi wake pia hawana busara walitakiwa wakuulize kulikoni, kabla hawaanza kukurushia maneno ya kipuuzi. Hii inaonyesha hukufanya homework yako vizuri kabla hukuoa. Uliangalia uzuri nini? Uzuri wa mtu si sura ila watu wengi hubabaika na jinsi mtu anavyoonekana. Ilibidi usome tabia ya mwenzio kabla hamjaoana. Tafuta wazee wa busara mkae wewe,wazee wako na wake muangalie jisi ya kulitatua. Pole.
Ni wiki imepita tangu nimrejeshe kwao wife kwa mara ya kwanza tangu tuoane miaka 10 iliyopita kutokana na kutozingatia makubaliano tunayowekeana kama couple na jeuri, ubabe pamoja na kiburi. Lengo la kumpeleka si kumfukuza bali ili wazazi wamhoji na kumshauri baada ya wazazi wangu kufanya kazi hiyo miaka zaidi ya 9. Wazazi wangu (mwanaume) wamekuwa kimbilio la mke wangu kwa zaidi ya miaka 9 hata pale mkosa anapokuwa ni yeye akiamini wao nitawasikiliza zaidi pale wanapoomba nimsamehe wife. Kwa upande mwingine hajawahi kimbilia kwao licha ya kuwa jirani na tunapoishi kwa kuona ndugu zake watamwona ameshindwa kuishi ktk ndoa. This time nimemwambia aende kwa wazazi wake na then tutaongea mambo yote pale baada ya wiki moja.

Siku mbili baada ya kufika kwao Mama yake kaanza kulaani mimi(mume) kumpa binti yao masharti ya kuishi ktk ndoa na kusema ni marufuku mimi kumpa masharti binti yao. Kwa tone hiyo hiyo siku nne baadaye baba mkwe kanipigia simu KUNITISHIA KWAMBA atamleta KWA NGUVU BINTI YAKE huku mama yake akisema nisipofungua nyumba wakati wa kumleta WATAVUNJA MLANGO WAMWINNGIZE NDANI.

Cha ajabu hawa wazazi wa binti hawajawahi niuliza tuna ugomvi gani, tometofautiana nini bali kunilaumu hata bila kunisikiliza. Hali hii inanifanya niamini kuwa ujeuri, ubabe na kiburi cha binti yao ambaye ni mke wangu kinakuzwa na hawa wazazi wake kwa kutokuwa rational.
Ndugu zangu wanachukulia huu kama udhalilishaji na vita isiyokuwa ya lazima ya ukoo na dharau kwa upande si wa ndugu zangu tu bali hata kwa mume wa binti yao.
NISAIDIENI BUSARA ZA KU REACT!!!!
 
Ni wiki imepita tangu nimrejeshe kwao wife kwa mara ya kwanza tangu tuoane miaka 10 iliyopita kutokana na kutozingatia makubaliano tunayowekeana kama couple na jeuri, ubabe pamoja na kiburi. Lengo la kumpeleka si kumfukuza bali ili wazazi wamhoji na kumshauri baada ya wazazi wangu kufanya kazi hiyo miaka zaidi ya 9. Wazazi wangu (mwanaume) wamekuwa kimbilio la mke wangu kwa zaidi ya miaka 9 hata pale mkosa anapokuwa ni yeye akiamini wao nitawasikiliza zaidi pale wanapoomba nimsamehe wife. Kwa upande mwingine hajawahi kimbilia kwao licha ya kuwa jirani na tunapoishi kwa kuona ndugu zake watamwona ameshindwa kuishi ktk ndoa. This time nimemwambia aende kwa wazazi wake na then tutaongea mambo yote pale baada ya wiki moja.

Siku mbili baada ya kufika kwao Mama yake kaanza kulaani mimi(mume) kumpa binti yao masharti ya kuishi ktk ndoa na kusema ni marufuku mimi kumpa masharti binti yao. Kwa tone hiyo hiyo siku nne baadaye baba mkwe kanipigia simu KUNITISHIA KWAMBA atamleta KWA NGUVU BINTI YAKE huku mama yake akisema nisipofungua nyumba wakati wa kumleta WATAVUNJA MLANGO WAMWINNGIZE NDANI.

Cha ajabu hawa wazazi wa binti hawajawahi niuliza tuna ugomvi gani, tometofautiana nini bali kunilaumu hata bila kunisikiliza. Hali hii inanifanya niamini kuwa ujeuri, ubabe na kiburi cha binti yao ambaye ni mke wangu kinakuzwa na hawa wazazi wake kwa kutokuwa rational.
Ndugu zangu wanachukulia huu kama udhalilishaji na vita isiyokuwa ya lazima ya ukoo na dharau kwa upande si wa ndugu zangu tu bali hata kwa mume wa binti yao.
NISAIDIENI BUSARA ZA KU REACT!!!!

Pole sana ndugu.
Kwenye ndoa huwa wanaume tunafanya makosa sana ndoa inapoanza, hatuweki misingi ya ndoa na kuisimamia pale ndoa inapoanza na kuchukua hatua sitahili misingi inapokiukwa. Moja ya makosa ni kuonesha ustaarabu pale misingi ya ndoa inapokiukwa. Uzoefu nilionao kwenye ndoa (7years) ni kwamba ninapochukua hatua ambayo inaonekana ni harsh kwa misingi ya ndoa yangu iliyokiukwa na wife kosa hilo halirudiwi tena. Nimeshafanya hivyo hadi ndugu wa wife wakanitishia kunitenga nikawaambia poa tu, nitabaki na ndoa yangu na lazima afuate misingi ya ndoa yangu na kama hataki atimue na sihitaji msaada wowote kutoka kwenu. Waliweka mgomo kutokuja kwangu for 6 months lakini sasa wanakuja na nina wasaidia! Weka msimamo bwana, wewe ni mwanaume!
 
Kwa hiyo unaona ndoa ni nzuri kwa sababu ya kibano cha maisha? Na kama hakuna kibano cha maisha?
Kiranga,
Ndoa ni nzuri kwa mambo mengi, mungu aliyemuumba mwanaume aliona ni vyema akawa na msaidizi kwa kuwa Alijua kuwa hatoweza kuface challenge za maisha akiwa peke yake,kwa hiyo sio kibano peke yake, mwanamke ni mwenza katika maisha, ni mwenza katika kila kitu na ni msaidizi wa kweli.Nilitoa mfano wa kibano angalau kukuonyesha ni namna gani unahitaji kuwa na mwenza.Maisha yana nyakati nyingi unahitaji mtu ambaye atakuwa na wewe katika steji zote za maisha wakati wa furaha mnafuraia mafanikio pamoja, wakati wa huzuni mnahuzunika pamoja, mnatofautiana kwa jambo moja au jingine lakini bado mnakuwa pamoja.
 
kama wazazi wa binti hawataki kukusikiliza kujua tatizo ni nini na wanalazimisha kumrudisha binti kwako basi acha wamrudishe lakini wewe ondoka mwachie binti yao nyumba wewe angalia utaratibu mwingine wa maisha
 
mkuu pole dah inaelekea hao wakwe zako wote walikuaga maaskari..utiii amri bila shurutii
 
Wazazi wengi uwasikiliza wakwe zao zaidi ya mabinti zao...unajua kwa nini?

Wewe utakuwa ulikuwa hupeleki misaada ukweni. Lol

Ila kwangu mimi kama mwanamke napenda sana wazazi wangu wa stand by me...ingawa si kwa staili hiyo...ila it feels good ndugu na jamaa zako wakikuamini
 
Watz wengi huwa tunakosea kutoa ushsuri mahali amabpo una mgogo baina ya pande mbili kwa kusikiliza madai ya upande mmoja,ni imani yangu kwamba huyo mkeo amewaambia maneno mazito na mabaya kuhusu wewe ndio maana wamereaact,kuna njia za kufuatwa kumaliza taizo hili sijui ndoa yako uliifinga kimisingi gani yaani serikalini,kanisani,msikitini aua wapi???
 
kama wazazi wa binti hawataki kukusikiliza kujua tatizo ni nini na wanalazimisha kumrudisha binti kwako basi acha wamrudishe lakini wewe ondoka mwachie binti yao nyumba wewe angalia utaratibu mwingine wa maisha
duh mgogoro hauwi solved hivyo naamini lengo la kumrudisha kwa wazazi wake sio kumkimbia ni ili apaeleke tarifa nini kinaendelea na wazazi wajue kwa busara zao nini wanaweza wakafanya kunusuru ndoa ajabu wazazi wenyewe hovyo wamekuruouka kwenye kufanya maamuzi
 
ww pia huna busara kwanini unarudisha mkeo nyumbani mara kwa mara?Miaka 10 adi leo hamjajuana tabia zenu?
Suluhisho la ndoa hufanya na wanandoa wenyewe na si wazazi wala majirani,Marafiki.

Mkishindwa kuelewana na mkeo hama chumba kwa mda adi hasira zikuishe na sio kumfukuza mwenzio na kwenda kujiongezea maneno na chuki kwa watu wa nje.Hayo mambo ya kufukuza wanafanya mwenye ndoa changa ikifika miaka 4 kuendelea mnakuwa mmeshajuana tabia.sio kwamba watu hawagombani wengi tunakwaruzana kwenye ndoa zetu lakini tunayamaliza mwenyewe kimya kimya na si kufukuza wala kwenda kushitakiana.
 
mwaga mboga kama hawajakuita wakawaulizeni tatizo ni nini?mwambie baba mkwe mwanawe analazimisha anipe tigo!!kwishney
 
Duh! kweli dunia hii ina mengi, Mkuu kelele za chura hazimzuii mtu kulala, na ukiona chura anakufanya ushindwe kulala ujue huna usingizi! Mi nadhani wanaelewa lililotokea ila wanafanya kusudi!

Muhimu ni kusolve hilo tatizo mojakwamoja, So jikaze na usubiri mpaka muyamalize ndio umrejeshe!
 
Nakushauri mtafutie bi mdogo kuongeza ushindani,mimi sasa hivi nimeamini kuwa ukitaka kujua tabia ya binti fuatilia tabia ya mama mzazi ama mlezi!

kaka umesema kweli,,, tabia huanzia nyumbani..... victim wa mianajike kama hiyo ni wengi mno........ afikirie maisha mengine hapo hamna kitu,,,,
 
Back
Top Bottom