Baba hataki nibadilishe dini ili niolewe

Baba hataki nibadilishe dini ili niolewe

makofia360

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2015
Posts
776
Reaction score
2,405
Kijana amekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu sasa ndoto zao ni ndoa.

Tatizo lipo kwenye Dini msichana yeye yupo tayari kubadili na kuwa Muislam na hata mama yake msichana anamuunga mkono mwanae kwani hata yeye alibadilishwa na mumewe, Tatizo baba na ni muhudumu mkubwa wa Kanisa.

Wapi huyu kijana anzie anahofia hata kulifikisha kwa baba mkwe wake kwa alivyo mkali na misimamo. Tumsaidieni kwa mawazo chanya nini akifanye kwani wanapendana sana.

Karibuni waungwana
 
kijana amekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu sasa ndoto zao ni ndoa. Tatizo lipo kwenye dini msichana yeye yupo tayari kubadili na kuwa muislam na hata mama yake msichana anamuunga mkono mwanae kwani hata yeye alibadilishwa na mumewe, tatizo baba na ni muhudumu mkubwa wa kanisa. Wapi huyu kijana anzie anahofia hata kulifikisha kwa baba mkwe wake kwa alivyo mkali na misimamo. Tumsaidieni kwa mawazo chanya nini akifanye kwani wanapendana sana, karibuni waungwana
mm namuombea huyo msichana kuwe na pingamizi kubwa ashindwe kuolewa na huyo muislam,na huyo baba awe ma msimamo sana na hiyo ndoa isiwepo,nmemaliza
 
Kama wanapendana wakafunge ndoa kwa mkuu wa wilaya...then kila mmoja ashike dini yake.
 
Bora nionekane ninachuki hata vilevile nao wana chuki na mm,kama ni ww mdada nenda kaolewe huko utarudi tena hapa baada ya mwaka mmoja kuomba msaada kimbia haraka kama mwizi huyo hakufai kabisa
 
nabii mweusi acha ubaguzi wa dini kwa haina nafasi katika mapenzi.
 
Bora nionekane ninachuki hata vilevile nao wana chuki na mm,kama ni ww mdada nenda kaolewe huko utarudi tena hapa baada ya mwaka mmoja kuomba msaada kimbia haraka kama mwizi huyo hakufai kabisa

usimuhukumu mtu kwa dini yake.mtoto mwenyewe amekubali wamwache asilimu.
 
unachotaka kufanya ni hatari sana ndugu.Nimeona ndoa kama hizo nyingi tu mwisho wake si mzuri,yaani hazidumu hata kidogo.pia utakosa amani moyoni na furaha katika ndoa.kumbuka biblia inasema waheshimu baba yako na mama yako ili siku zako zipate kuongezeka.ndugu hakun faida yeyote ya kupata MALI na kukosa ufalme wa Mungu.
 
Wanawake wanadanganywa mno, eti mwanamke hana dini, anabadili dini mambo yakiwa magumu hajui pa kuanzia. Mtu anatakiwa aijue na kuiamini hiyo dini kwanza mambo yakiharibika ajue atawasiliana vipi na Mungu wake ampitishe katika magumu yanayomsibu.

Hivi mtu anabadilisha dini ili aoe /aolewe

Au anabadilisha dini baada ya kuisoma, kuijua, kuielewa na kuiamini????
 
Kijana amekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu sasa ndoto zao ni ndoa.

Tatizo lipo kwenye Dini msichana yeye yupo tayari kubadili na kuwa Muislam na hata mama yake msichana anamuunga mkono mwanae kwani hata yeye alibadilishwa na mumewe, Tatizo baba na ni muhudumu mkubwa wa Kanisa.

Wapi huyu kijana anzie anahofia hata kulifikisha kwa baba mkwe wake kwa alivyo mkali na misimamo. Tumsaidieni kwa mawazo chanya nini akifanye kwani wanapendana sana.

Karibuni waungwana
Usibadili dini yako wanaume ni matapeli sana utakujajuta kwa kosa hilo, anakutamani tu hakupendi. Je uko tayari kuwa na wanawake wenzio 2?
 
Hapo amtafute babu wa msichana
aliemruhusu mama yake kubadili dini ili kuolewa ndo atamdhibiti baba wa msichana
 
Hakuna mapenzi wala nn ni tapeli tu huyo kijana hujui kitu ww ndo maana unabisha wao lengo lao waongezeke ukifika huko jamaa anatafuta mwanamke mwingine na sio hivyo tu ni mengi yanakera,sasa ww dada nenda kaolewe ukapate chungu ya mapenzi,ningekuwa karibu yako ningezabua na vibao ,nyau kabisa ww,utakuwa sio ww sasa naanza kukemea hilo pepo lilililokuingia lishindwe katika jina lipitalo majina yote
 
Hapo amtafute babu wa msichana
aliemruhusu mama yake kubadili dini ili kuolewa ndo atamdhibiti baba wa msichana

Well Said! Yaaani your the big thinker,,,And The Boss ushauri mzuri sana ndugu yangu
 
Hivi mtu anabadilisha dini ili aoe /aolewe

Au anabadilisha dini baada ya kuisoma, kuijua, kuielewa na kuiamini????

Hapa ndio kwenye utata BADILI TABIA.. Ila mie nitamuheshimu sana yule ambae amelisikiliza neno na likamuingia na akaliamini na kubadilisha imani yake, kuliko yule aliebadili dini kwa sababu ya kuoa/kuolewa..

Maana kwa mwanaume aliebadilisha dini kwa ajili ya mwanamke, aelewe dini yake itakuwa ni kifanywa cha mwanamke.. Na mwanamke ambae amebadilisha dini kwa ajili ya mwanaume aelewe dini yake itakuwa ni kifanyio cha mwanaume..
 
Last edited by a moderator:
Hakuna mapenzi wala nn ni tapeli tu huyo kijana hujui kitu ww ndo maana unabisha wao lengo lao waongezeke ukifika huko jamaa anatafuta mwanamke mwingine na sio hivyo tu ni mengi yanakera,sasa ww dada nenda kaolewe ukapate chungu ya mapenzi,ningekuwa karibu yako ningezabua na vibao ,nyau kabisa ww,utakuwa sio ww sasa naanza kukemea hilo pepo lilililokuingia lishindwe katika jina lipitalo majina yote

We nawe nini unàkomaa !yeye kwani uislam haujui!ameishi na waislamu siku zote za maisha anajua kuna kuoa zaidi ya mwanamke mmoja nakila kitu,acha wivu na chuki.wangapi wamebadili dini na maisha yao yanakwenda vizuri acha upotoshaji!
 
Back
Top Bottom