Habari zenu members
Nina rafiki yangu ana mke mmoja. Hii ndoa imekuwa na misukosuko kutokana na tabia ya rafiki yangu kumpiga mkewe karibia Kila wiki pamoja na kupenda michepuko lakini pia rafiki yangu amekuwa haachi matumizi badala yake inaenda kwa michepuko
Nakumbuka siku moja mkewe alinifuata Mimi Kama rafiki wa mumewe na kutaka niongee naye alinieleza mambo yote anayokutana nayo kwenye ndoa yake na kuniomba nimsaidie Jambo moja.
Tutengeneze Jambo la uongo Mimi nijifanye daktari halafu yeye amekuja hospital kwetu akiwa na mimba yenye miezi minne bahati mbaya ionekane mimba yake imeharibika na amekuja bila hela yoyote alafu akaniambia mumewe akituma hela atanitoa 50k ikiwa tayali alishafoji cheti Cha kliniki kinaonesha ana mimba .
Kiukwel ilikuwa ngumu kukubali kirahisi kwasababu sikuwahi kufanya Jambo Kama hili hapo kabla lakini kutokana na mapito anayopitia ninayoiona na mengine alivyonieleza nikabidi nimfanyie hili jambo
Tulifanikiwa na chakushangaza matibabu yote tuliitaji laki 3 lakini rafiki yangu alimtumia mkwewe laki 5 ni zaidi ya kile kiasi ambacho mkwewe alichoomba.
Ikabidi anipe 50k baada ya kazi alioniomba kuisha ila me nilimwambia asinipe ujue hakuna mtu asiyependa hela lakini sometime utangulize huruma na utu na usipende Sana hela mbele kwenye Kila Jambo ingawa nilikuwa Nina shida na hela ila matatizo aliyonayo huyu dada ni makubwa Sana so why nikaona nisichue hiyo hela.
Ingawa nilikuwa najua mchepuko wa rafiki yangu sikuweza kumwambia mkewe ila nilichofanya ni kumsaidia ndoa yao isitetereke.
Me binafsi ninajiuliza kiukwel mke wa rafiki yangu ni mzuri Sana kuliko hata mchepuko wa rafiki yangu na ni mwanamke anajitambua lakini pia anampenda Sana rafiki yangu kwa changamoto anayopitia ni wanawake wachache sana wanaweza kuvumilia unajiuliza kitu gani unakikosa kwa mkwewe mpaka uwende kwa michepuko?
Me nilichofanya nikabidi nichukue number ya mchepuko wa rafiki yangu na kweli nikafanikiwa sura ninaijua ila number ndo nilikuwa Sina nikampigia yule mchepuko wa rafiki yangu na tukapanga tukutane na tuliweza kukutana na nikabidi nimwambie ukweli kwamba rafiki yangu ana mke kitu ambacho niligundua hajui na nikamweleza yote.
Na ni kweli baada ya muda mfupi rafiki yangu akaachwa na yule mchepuko lakini pia sikuishia hapo nikabidi nikae na rafiki yangu pamoja na mkewe ili ni tatua tatizo la na kweli mazungumzo yaliendelea vizuri na kiasi Fulani yalimsaidia kumbadilisha tabia rafiki yangu.
NB: Wanaume hebu tujitahidi tuache tabia ya kupiga wake vibaya au kusahau kutimiza majukumu yetu Kama wanaume.
Nina rafiki yangu ana mke mmoja. Hii ndoa imekuwa na misukosuko kutokana na tabia ya rafiki yangu kumpiga mkewe karibia Kila wiki pamoja na kupenda michepuko lakini pia rafiki yangu amekuwa haachi matumizi badala yake inaenda kwa michepuko
Nakumbuka siku moja mkewe alinifuata Mimi Kama rafiki wa mumewe na kutaka niongee naye alinieleza mambo yote anayokutana nayo kwenye ndoa yake na kuniomba nimsaidie Jambo moja.
Tutengeneze Jambo la uongo Mimi nijifanye daktari halafu yeye amekuja hospital kwetu akiwa na mimba yenye miezi minne bahati mbaya ionekane mimba yake imeharibika na amekuja bila hela yoyote alafu akaniambia mumewe akituma hela atanitoa 50k ikiwa tayali alishafoji cheti Cha kliniki kinaonesha ana mimba .
Kiukwel ilikuwa ngumu kukubali kirahisi kwasababu sikuwahi kufanya Jambo Kama hili hapo kabla lakini kutokana na mapito anayopitia ninayoiona na mengine alivyonieleza nikabidi nimfanyie hili jambo
Tulifanikiwa na chakushangaza matibabu yote tuliitaji laki 3 lakini rafiki yangu alimtumia mkwewe laki 5 ni zaidi ya kile kiasi ambacho mkwewe alichoomba.
Ikabidi anipe 50k baada ya kazi alioniomba kuisha ila me nilimwambia asinipe ujue hakuna mtu asiyependa hela lakini sometime utangulize huruma na utu na usipende Sana hela mbele kwenye Kila Jambo ingawa nilikuwa Nina shida na hela ila matatizo aliyonayo huyu dada ni makubwa Sana so why nikaona nisichue hiyo hela.
Ingawa nilikuwa najua mchepuko wa rafiki yangu sikuweza kumwambia mkewe ila nilichofanya ni kumsaidia ndoa yao isitetereke.
Me binafsi ninajiuliza kiukwel mke wa rafiki yangu ni mzuri Sana kuliko hata mchepuko wa rafiki yangu na ni mwanamke anajitambua lakini pia anampenda Sana rafiki yangu kwa changamoto anayopitia ni wanawake wachache sana wanaweza kuvumilia unajiuliza kitu gani unakikosa kwa mkwewe mpaka uwende kwa michepuko?
Me nilichofanya nikabidi nichukue number ya mchepuko wa rafiki yangu na kweli nikafanikiwa sura ninaijua ila number ndo nilikuwa Sina nikampigia yule mchepuko wa rafiki yangu na tukapanga tukutane na tuliweza kukutana na nikabidi nimwambie ukweli kwamba rafiki yangu ana mke kitu ambacho niligundua hajui na nikamweleza yote.
Na ni kweli baada ya muda mfupi rafiki yangu akaachwa na yule mchepuko lakini pia sikuishia hapo nikabidi nikae na rafiki yangu pamoja na mkewe ili ni tatua tatizo la na kweli mazungumzo yaliendelea vizuri na kiasi Fulani yalimsaidia kumbadilisha tabia rafiki yangu.
NB: Wanaume hebu tujitahidi tuache tabia ya kupiga wake vibaya au kusahau kutimiza majukumu yetu Kama wanaume.