DOKEZO Responded Baadhi ya Majengo ya Shule ya Sekondari ya Jenista Mhagama yawaka moto, inadaiwa kuna hujuma

DOKEZO Responded Baadhi ya Majengo ya Shule ya Sekondari ya Jenista Mhagama yawaka moto, inadaiwa kuna hujuma

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
427
Reaction score
666
Baadhi ya mabweni ya Wanafunzi wa kike pamoja na stoo ya Shule ya Sekondari ya Jenista Mhagama iliyoko Halmashauri ya Songea Mkoani Ruvuma yameharibika kwa kuwaka moto siku chache zilizopita na kusababisha hasara ya mali.

Baadhi ya vitu vilivyoharibika ni matranka na vifaa vya Wanafunzi, huku kukiwa hakuna Mwanafunzi aliyejeruhiwa katika tukio hilo.
IMG_20250609_120429_334.jpg
Inadaiwa moto huo ulitokea Usiku wa Saa Nane ambapo sauti za Wanafunzi waliokuwa wakipiga kelele zilisikika wakisema "moto, moto” na waliotoka nje wakashuhudia moto huo hali iliyozua taharuki miongoni mwa Wanafunzi.

Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika rasmi, lakini inadaiwa kuna Mtu alihusika kwa makusudi kuchoma majengo hayo.

Inadaiwa kuwa mtu anayedhaniwa kuhusika na tukio hilo alikuwa akivizia nyakati ambazo Wanafunzi hawapo bwenini ndipo alipotekeleza kitendo hicho cha kuchoma majengo.
IMG_20250609_120429_795.jpg
Shule hiyo ina majengo mbalimbali takribani 126
WhatsApp Image 2025-06-07 at 20.52.54_8295a6b0.jpg

WhatsApp Image 2025-06-07 at 20.52.52_c4cec323.jpg

Majibu ya Mkuu wa Wilaya ~ DC Songea: Mwanafunzi amechoma moto shule ili ifungwe apate nafasi ya kupumzika
 
Dah nikikumbuka shuleni alikamatwa dogo alidanganywa na watu na wakampa pesa ili achome shule ila haikuwezekana
 
Back
Top Bottom