Nimekulia malezi ya Dada yangu, Mama yetu alituzaa watoto 4, kaka zangu 2, dada yangu na mimi, mimi ni mtoto wa mwisho kwa wazazi wangu, Baba yetu baada ya kuamua kuoa mke mwingine mama alitulea kwa shida na taabu nyingi mno, Lakini nashukuru Mungu kwani tulikua vyema, Hata hivyo baada ya baba kuoa na mwanamke wake kutokuzaa baba aliamua kurudi kwa mamayangu, lakini mama hakuwa tayari kumpokewa baba kwa kile alichodai ni kuonewa, na hivyo baba aliamua kuondoka na kurudi kwa wakwe zake, yaani kwa wazazi wa mkewe, na huko aliteseka sana ba baadae alifariki dunia na hakuna aliyeweza kwenda kumuona baba licha ya kumzika.
Nimekulia malezi ya Dada yangu, Mama yetu alituzaa watoto 4, kaka zangu 2, dada yangu na mimi, mimi ni mtoto wa mwisho kwa wazazi wangu, Baba yetu baada ya kuamua kuoa mke mwingine mama alitulea kwa shida na taabu nyingi mno, Lakini nashukuru Mungu kwani tulikua vyema, Hata hivyo baada ya baba kuoa na mwanamke wake kutokuzaa baba aliamua kurudi kwa mamayangu, lakini mama hakuwa tayari kumpokewa baba kwa kile alichodai ni kuonewa, na hivyo baba aliamua kuondoka na kurudi kwa wakwe zake, yaani kwa wazazi wa mkewe, na huko aliteseka sana ba baadae alifariki dunia na hakuna aliyeweza kwenda kumuona baba licha ya kumzika.
Asubuhi ya siku hiyo nimechukliwa na dada, Nakumbuka tukiwa sebuleni, Dada yangu alimwambia mumewe, Mume wangu mpendwa, ninaomba Sheila aishi na sisi ili atusaieid kulea watoto na kunisaidia kazi za ndani na gharama za msichana zipungue kwani atafanya kazi zote za ndani kikubwa tu akae hapa... Shemeji yangu alinitazama kwa huruma mno kisha akanishika kichwa na kusema kaa hapa usijali wala hutakaa kama msichana wa kazi ila kama moto wetu. Dada yangu alilia kwa uchungu na machozi yakimtoka na kisha kumwambia mumewe, Mungu akubariki mno mume wangu na akufanikishe mno mume wangu mpenzi, asante sana Mume wangu.. Dada kwa shukrani hizo alinifanya na mimi machozi yanitoke.
Dada alinifuata akaniambia, Sheila mdogowangu, wewe ni kama mwanangu sasa naomba niheshimu kama mama yako na shemeji yako mheshimu kama baba yako, uwe na adabu unaona baba wa watu kaamu akukukubali naomba usiniangushe, uwe na heshima mdogo wangu ili ufanikiwe, Mume wangu atakusaidia sana nakuomba tafadhali,kila nitakachokueleza nisikilize, nikikukosea vumilia mdogo wangu ili upate maisha, sawa mama? Alinieleza kwa kunibembeleza maneno hayo,, Nilimtazama dada yangu na kumhurumia kwani alikuwa akitaka nipate maisha mazuri na alikuwa tayari mimi nifanye hata kazi za ndani ili mradi tu niishi naye kwani mateso kwa kaka zangu hakuyapenda hata kidogo.
Nikiwa na miaka 15 baada ya kumaliza darasa la saba, nilikuwa mchapa kazi, dada yangu anaishi mjini, kuna kila aina ya starehe, Mume wa dada anafanya kazi kwenye kampuni kubwa serikalini wana maisha mazuri mno, hivyo nilijua kuishi kwa adabu ndiko kutanifanikisha kimaisha. Na mimi niliamua kuvumilia na kuishi kwa adabu ili niweze kufanikiwa, Nilifanya kazi kwa bidii zote na wala sikujali kwani nilijua kufanya kazi kwangu ndiko kutanipa heshima na kupendwa zaidi. Asbh niliamka na kuwaandaa watoto 3 wa dada yangu kwa ajiali ya kwnda shule, nilifnaya usafi nyumba nzima na kufagia nje, na ilipofika saa 2 kamili asb nilikuwa nimemaliza kila kazi. Dada na shemeji walinipenda mno, wengi waliamini kwamba mimi ni msichana wa kazi hapo mtaani, lakini ukweli nilikuwa mdogo kabisa wa dada yangu.
Maisha yaliendelea hivyo na siku moja nikiwa sebuleni nawasimamia watoto wa dada yangu wale chakula Shemeji yangu alinitazama nilivyokuwa nawasimamia watoto kwa upendo, kisha alimuita dada yangu.. MAMA WATOTO,,, Dada yangu aliitika,, Abee mume wengu.. kisha akawa anakuja sebuleni akitokea chumbani huku anasuka mabutu nywele zake tayari kwa kulala kwani ilikuwa ni usiku.. na mara nyingi husuka nywele zake mabutu alalapo... Alifika alipokuwa shemeji na kisha akamwambia ona watoto wetu walivyo na furaha na mama yao mdogo! Dada aliwatazama kisha akatabasamu na kuniangalia na kusema Sheila anawapenda sana watoto.... Shemeji alimtazama dada na kusema je unaonaje kama tukimtafutia Sheila shule kwa kazi nzuri aliyoifanya? Dada yangu amejaliwa kushukuru,, alimtazama Mume wake na kumwambia,, Mume wangu,, nitakushukur zaidi ya kukushukuru asante kumsaidia Sheila ... Shemeji alinitazama kisha akaniambia utaweza kusoma? Nilimjibu ndio shemeji nitaweza kusoma... kisha Shemeji akamwambia dada kwamba kesho nikiwa ofcn usisahau kunipigia simu kunikumbusha juu ya swala hili ili nilishughulikie.
Wakati wote huo kaka zangu walijua naishi kwa dada yangu, na saa wakaanza kuingiwa na wivu kwa nini ninaishi kwa dada badala ya kwa kaka? awalianza maneno ya kichini chini na kuanza kumchukia dada yangu. Wifi yangu wa kaka mdogo alimueleza dada yangu maneno ya umbea na kumwambia kwamba huenda ninatembea na shemeji yangu ndi omaana shemeji yangu ananisomesha, maneno yalikuwa makubwa mno, lakini dada yangu aliniambia KAMA HUFANYI USIJALI, Na kweli sikuwa nafanya hivyo wala sikujali, na dada alinitia moyo sana, ,, Nilikuwa nina heshima mno, nilimpenda dada yangu sana, nilimheshimu mno, alinipenda na kunijali.... Nikiwa sekondari mwaka wa pili kidato cha pili wakati wa likizo niliporejea nyumbani, kaka zangu walikuja kwa dad ayangu na kunitaka kurudi nyumbani yaani kwa mmoja wa kakazangu, roho yangu iliniuma mno, na waliniambia kwamba watanisomesha wao na hivyo siruhusiwi kukaa kwa dada yangu, niliumia sana kwani pia walimurushia shemeji maneno ya kejeli na kumwambia kwamba mimi nina mahusiano ya mapenzi na shemeji yangu niliumia sana na sasa ilikuwa ni lazima niondoke. Usiku huo nilianza kufungasha nguo zangu na kuwaaga dada na shemeji na sasa nilikuwa naelekea kwa kaka yangu kuishi naye huko.
Maisha ya kwa kaka yalikuwa magumu, kaka alikuwa haeleweni na mkewe, hiivyo mudamwigni walikuwa hawana furaha wala maelewano, nilijiahidi kufanya kazi kwa kumaanisha lakin hawakuridhika,,, Kaka alinitafutia shule ambayo waliweza kumudu kulipa ada na ilikuwa ni shule ya day wkwani shule ambayo nilikuwa nasoma ambayo dada na shemeji walinilipia ilikuwa ya gharama kiasi kwamba kaka wasingeweza japo uwezo walikuwa nao. Nilikaa kwa wifi lakini kwa mateso makubwa mno, nilitukanwa, nilidharuliwa lakini sikuwa na laa kufanya. Wifi yangu alinichukia mno lakni hakuna kibaya nilichofanya. Mateso yalipozidi ikiwa ni pamoja na kufungiwa nje mara nichelewapo kurudi nyumbani kutokana na usafiri,, kwani kulala nje ilikuwa ni kawaida, mara nichelewapo hakuna aliyefungua mlango niingie ndani, sio kaka wala wifi, hivyo nilikuwa niliilala nje kila mara ,, Nilipoenda kumueleza dada dada aliumia sana na aliniahidi kwamba kama nina moyo wa kujitolea kutengwa na familia basi niondoke na nisijali kwani watakataa kulipa ada ya shule ... na dada alinaimbia kwamba mume wake aliogopa kueondelea kunisaidia kuotkana na kejeli za kaka zetu.. Niliwaza sana je niendelee na mateso ili nilipiewe ada ya shule ama nikose shule na kutafuta maisha mengine? nilikuwa kwenye wakati mgumu mno.
Mateso yaliendelea kwa kaka na mwisho wa siku wifi na kaka walienda kunishtaki shuleni wkwamba nina tabia ya kulala nje,, niliumia sana na waliniita malaya.... Nilimfuata mwalimu mkuu wa shule, na kumueleza kisa halisia, na kwamba hizo tabia sina, mwalimu aliniangalia na kusema anaamini kwamba sina hizo tabia lakini walezi wanalalamika juu ya tabia hizo na wamesema hawatanisomesha tena,,, niliumia mno, nilipenda shule, nilitamani kusoma ili niweze kufanikiwa maishani mwangu, niliamini elimu ni ufunguo wa maisha,,, Kaka na wifi waliapa kutonilipia ada na waliondoka,, mwalimu mkuu alinitazama na kunihurumia,, sana na akasema hana uwezo wa kunisaidia kwani ni lazima niwe na ada ndipo nipate Elimu. Wifi na kaka waliondoka na kuniacha shuleni nikiwa nalia.. Jioni nilielekea nyumbani, nilipofika kaka alinipokea kwa matusi na kuanza kunipiga sana kwa kudai kwamba nina wanaume, alinipiga mnonilimuomba msamaha lakini wifi alionekana kushinikiza nipigwe, niliumiamwilini kwani kaka alinichapa na mkanda,,, Baada ya kipigo hicho niliwaza nifanyeje? Niliondoka nakuelekea kwa dada yangu,, nilipofika nilimkuta amekaa sebuleni na mumewe na watoto na msichana wao wa kazi,, walinipokea na kuniuliza kulikoni? niliwaeleza hali halisi. Dada yangu aliumia sana na kujaribu kumuelewesha mumewe kwamba anisaidie tu kunilipia ada kwa siri mimi nikae shule ya boarding,, alimbembeleza mno. Usiku huo shemeji yangu alihofia mimi kulala ndani kwani nilikuwa nimepigwa mno na kuvimba na kuvilia damu, hivy alimshauri dada yagnu anipeleke hospitali. nilipelekwa hospitali na kutibiwa nakupewa dawa za kutuliza maumivu. kisha nikarudi kulala, nililala siku nne nikiwa hoi ndani naugulia maumivu. Kaka yangu hakunitafuta wala wifi , isipokuwa walimueleza kaka yangu mwingine kwamba nimetorokea kwa mwanaume.
Fuatana nami kibebi msimuliaji katika simulizi hii ya kusisismua
Nimekulia malezi ya Dada yangu, Mama yetu alituzaa watoto 4, kaka zangu 2, dada yangu na mimi, mimi ni mtoto wa mwisho kwa wazazi wangu, Baba yetu baada ya kuamua kuoa mke mwingine mama alitulea kwa shida na taabu nyingi mno, Lakini nashukuru Mungu kwani tulikua vyema, Hata hivyo baada ya baba kuoa na mwanamke wake kutokuzaa baba aliamua kurudi kwa mamayangu, lakini mama hakuwa tayari kumpokewa baba kwa kile alichodai ni kuonewa, na hivyo baba aliamua kuondoka na kurudi kwa wakwe zake, yaani kwa wazazi wa mkewe, na huko aliteseka sana ba baadae alifariki dunia na hakuna aliyeweza kwenda kumuona baba licha ya kumzika.
Asubuhi ya siku hiyo nimechukliwa na dada, Nakumbuka tukiwa sebuleni, Dada yangu alimwambia mumewe, Mume wangu mpendwa, ninaomba Sheila aishi na sisi ili atusaieid kulea watoto na kunisaidia kazi za ndani na gharama za msichana zipungue kwani atafanya kazi zote za ndani kikubwa tu akae hapa... Shemeji yangu alinitazama kwa huruma mno kisha akanishika kichwa na kusema kaa hapa usijali wala hutakaa kama msichana wa kazi ila kama moto wetu. Dada yangu alilia kwa uchungu na machozi yakimtoka na kisha kumwambia mumewe, Mungu akubariki mno mume wangu na akufanikishe mno mume wangu mpenzi, asante sana Mume wangu.. Dada kwa shukrani hizo alinifanya na mimi machozi yanitoke.
Dada alinifuata akaniambia, Sheila mdogowangu, wewe ni kama mwanangu sasa naomba niheshimu kama mama yako na shemeji yako mheshimu kama baba yako, uwe na adabu unaona baba wa watu kaamu akukukubali naomba usiniangushe, uwe na heshima mdogo wangu ili ufanikiwe, Mume wangu atakusaidia sana nakuomba tafadhali,kila nitakachokueleza nisikilize, nikikukosea vumilia mdogo wangu ili upate maisha, sawa mama? Alinieleza kwa kunibembeleza maneno hayo,, Nilimtazama dada yangu na kumhurumia kwani alikuwa akitaka nipate maisha mazuri na alikuwa tayari mimi nifanye hata kazi za ndani ili mradi tu niishi naye kwani mateso kwa kaka zangu hakuyapenda hata kidogo.
Nikiwa na miaka 15 baada ya kumaliza darasa la saba, nilikuwa mchapa kazi, dada yangu anaishi mjini, kuna kila aina ya starehe, Mume wa dada anafanya kazi kwenye kampuni kubwa serikalini wana maisha mazuri mno, hivyo nilijua kuishi kwa adabu ndiko kutanifanikisha kimaisha. Na mimi niliamua kuvumilia na kuishi kwa adabu ili niweze kufanikiwa, Nilifanya kazi kwa bidii zote na wala sikujali kwani nilijua kufanya kazi kwangu ndiko kutanipa heshima na kupendwa zaidi. Asbh niliamka na kuwaandaa watoto 3 wa dada yangu kwa ajiali ya kwnda shule, nilifnaya usafi nyumba nzima na kufagia nje, na ilipofika saa 2 kamili asb nilikuwa nimemaliza kila kazi. Dada na shemeji walinipenda mno, wengi waliamini kwamba mimi ni msichana wa kazi hapo mtaani, lakini ukweli nilikuwa mdogo kabisa wa dada yangu.
Maisha yaliendelea hivyo na siku moja nikiwa sebuleni nawasimamia watoto wa dada yangu wale chakula Shemeji yangu alinitazama nilivyokuwa nawasimamia watoto kwa upendo, kisha alimuita dada yangu.. MAMA WATOTO,,, Dada yangu aliitika,, Abee mume wengu.. kisha akawa anakuja sebuleni akitokea chumbani huku anasuka mabutu nywele zake tayari kwa kulala kwani ilikuwa ni usiku.. na mara nyingi husuka nywele zake mabutu alalapo... Alifika alipokuwa shemeji na kisha akamwambia ona watoto wetu walivyo na furaha na mama yao mdogo! Dada aliwatazama kisha akatabasamu na kuniangalia na kusema Sheila anawapenda sana watoto.... Shemeji alimtazama dada na kusema je unaonaje kama tukimtafutia Sheila shule kwa kazi nzuri aliyoifanya? Dada yangu amejaliwa kushukuru,, alimtazama Mume wake na kumwambia,, Mume wangu,, nitakushukur zaidi ya kukushukuru asante kumsaidia Sheila ... Shemeji alinitazama kisha akaniambia utaweza kusoma? Nilimjibu ndio shemeji nitaweza kusoma... kisha Shemeji akamwambia dada kwamba kesho nikiwa ofcn usisahau kunipigia simu kunikumbusha juu ya swala hili ili nilishughulikie.
Wakati wote huo kaka zangu walijua naishi kwa dada yangu, na saa wakaanza kuingiwa na wivu kwa nini ninaishi kwa dada badala ya kwa kaka? awalianza maneno ya kichini chini na kuanza kumchukia dada yangu. Wifi yangu wa kaka mdogo alimueleza dada yangu maneno ya umbea na kumwambia kwamba huenda ninatembea na shemeji yangu ndi omaana shemeji yangu ananisomesha, maneno yalikuwa makubwa mno, lakini dada yangu aliniambia KAMA HUFANYI USIJALI, Na kweli sikuwa nafanya hivyo wala sikujali, na dada alinitia moyo sana, ,, Nilikuwa nina heshima mno, nilimpenda dada yangu sana, nilimheshimu mno, alinipenda na kunijali.... Nikiwa sekondari mwaka wa pili kidato cha pili wakati wa likizo niliporejea nyumbani, kaka zangu walikuja kwa dad ayangu na kunitaka kurudi nyumbani yaani kwa mmoja wa kakazangu, roho yangu iliniuma mno, na waliniambia kwamba watanisomesha wao na hivyo siruhusiwi kukaa kwa dada yangu, niliumia sana kwani pia walimurushia shemeji maneno ya kejeli na kumwambia kwamba mimi nina mahusiano ya mapenzi na shemeji yangu niliumia sana na sasa ilikuwa ni lazima niondoke. Usiku huo nilianza kufungasha nguo zangu na kuwaaga dada na shemeji na sasa nilikuwa naelekea kwa kaka yangu kuishi naye huko.
Maisha ya kwa kaka yalikuwa magumu, kaka alikuwa haeleweni na mkewe, hiivyo mudamwigni walikuwa hawana furaha wala maelewano, nilijiahidi kufanya kazi kwa kumaanisha lakin hawakuridhika,,, Kaka alinitafutia shule ambayo waliweza kumudu kulipa ada na ilikuwa ni shule ya day wkwani shule ambayo nilikuwa nasoma ambayo dada na shemeji walinilipia ilikuwa ya gharama kiasi kwamba kaka wasingeweza japo uwezo walikuwa nao. Nilikaa kwa wifi lakini kwa mateso makubwa mno, nilitukanwa, nilidharuliwa lakini sikuwa na laa kufanya. Wifi yangu alinichukia mno lakni hakuna kibaya nilichofanya. Mateso yalipozidi ikiwa ni pamoja na kufungiwa nje mara nichelewapo kurudi nyumbani kutokana na usafiri,, kwani kulala nje ilikuwa ni kawaida, mara nichelewapo hakuna aliyefungua mlango niingie ndani, sio kaka wala wifi, hivyo nilikuwa niliilala nje kila mara ,, Nilipoenda kumueleza dada dada aliumia sana na aliniahidi kwamba kama nina moyo wa kujitolea kutengwa na familia basi niondoke na nisijali kwani watakataa kulipa ada ya shule ... na dada alinaimbia kwamba mume wake aliogopa kueondelea kunisaidia kuotkana na kejeli za kaka zetu.. Niliwaza sana je niendelee na mateso ili nilipiewe ada ya shule ama nikose shule na kutafuta maisha mengine? nilikuwa kwenye wakati mgumu mno.
Mateso yaliendelea kwa kaka na mwisho wa siku wifi na kaka walienda kunishtaki shuleni wkwamba nina tabia ya kulala nje,, niliumia sana na waliniita malaya.... Nilimfuata mwalimu mkuu wa shule, na kumueleza kisa halisia, na kwamba hizo tabia sina, mwalimu aliniangalia na kusema anaamini kwamba sina hizo tabia lakini walezi wanalalamika juu ya tabia hizo na wamesema hawatanisomesha tena,,, niliumia mno, nilipenda shule, nilitamani kusoma ili niweze kufanikiwa maishani mwangu, niliamini elimu ni ufunguo wa maisha,,, Kaka na wifi waliapa kutonilipia ada na waliondoka,, mwalimu mkuu alinitazama na kunihurumia,, sana na akasema hana uwezo wa kunisaidia kwani ni lazima niwe na ada ndipo nipate Elimu. Wifi na kaka waliondoka na kuniacha shuleni nikiwa nalia.. Jioni nilielekea nyumbani, nilipofika kaka alinipokea kwa matusi na kuanza kunipiga sana kwa kudai kwamba nina wanaume, alinipiga mnonilimuomba msamaha lakini wifi alionekana kushinikiza nipigwe, niliumiamwilini kwani kaka alinichapa na mkanda,,, Baada ya kipigo hicho niliwaza nifanyeje? Niliondoka nakuelekea kwa dada yangu,, nilipofika nilimkuta amekaa sebuleni na mumewe na watoto na msichana wao wa kazi,, walinipokea na kuniuliza kulikoni? niliwaeleza hali halisi. Dada yangu aliumia sana na kujaribu kumuelewesha mumewe kwamba anisaidie tu kunilipia ada kwa siri mimi nikae shule ya boarding,, alimbembeleza mno. Usiku huo shemeji yangu alihofia mimi kulala ndani kwani nilikuwa nimepigwa mno na kuvimba na kuvilia damu, hivy alimshauri dada yagnu anipeleke hospitali. nilipelekwa hospitali na kutibiwa nakupewa dawa za kutuliza maumivu. kisha nikarudi kulala, nililala siku nne nikiwa hoi ndani naugulia maumivu. Kaka yangu hakunitafuta wala wifi , isipokuwa walimueleza kaka yangu mwingine kwamba nimetorokea kwa mwanaume.
Fuatana nami kibebi msimuliaji katika simulizi hii ya kusisismua