RC Aboubakar Kunenge amefika katika Shule ya Msingi King'ongo wilayani Ubungo, Dar es Salaam baada ya Rais Magufuli kueleza kukerwa na wanafunzi shuleni hapo kukaa chini. Rais ameagiza atakaporejea Dar es Salaam madarasa shuleni hapo yawe yamekamilika na wanafunzi hawakai chini.
===
Akiwa mkoani Kagera, rais Magufuli alisema“Kuna maeneo hata Dar es salaam kuna mapungufu, kuna Shule moja ipo Ubungo, ina Wanafunzi wengi tu, Wanafunzi wapo Dar es salaam Ubungo bado wanakaa chini, madarasa yamebomoka, madawati yamevunjika, DC, DED na RC wapo na Mbunge yupo na ni Prof. tena wa Elimu”
“Namshukuru Mwandishi ameitoa kwenye mitandao kuwa Wanafunzi wanakaa chini, Viongozi wa kule wakaanza kusema ni masuala ya kisiasa, hayo sio masuala ya kisiasa, hayo Mimi ndio napenda kuyajua” aliongeza rais Magufuli.
“Ninazungumza nikiwa Kagera lakini nikienda Dar es salaam niyakute madarasa ya Shule ya Barango yamekamilika na Wanafunzi hawakai tena chini, nitaenda kuitembelea Mimi hiyo Shule, alibainisha rais Magufuli wakati akizungumza mkoani Kagera leo.
View attachment 1680653View attachment 1680654View attachment 1680655View attachment 1680656
RAIS MAGUFULI ATAKA VIONGOZI KUSHUGHULIKIA MAPUNGUFU
View attachment 1680666
- Asema, kuna Shule ya Msingi Ubungo, Dar iitwayo Barango bado Wanafunzi wanakaa chini huku madarasa mengine yakiwa yamebomoka
- Amesema atakapoenda anataka kukuta madarasa yamekamilika
Soma >
Rais Magufuli awataka Viongozi kushughulikia mapungufu akisema kuna wengine bado wamelala
#JFLeo
https://t.co/vC948tBDdi