Frustration
JF-Expert Member
- Jan 30, 2018
- 3,095
- 4,059
Hapo zamani nilikuwa na mchumba ambae hadi kuachana kwetu tayari alikuwa na mimba changa. Nlijua ila baada ya kuvurugwa kwa kutengana kule nilimkatalia kwa kumwambia sina mwanamke mwenye mimba kama wewe.
Yule binti akapata mtu mwingine ambae alidumu naye hadi kajifungua. Sijui walikubaliana nini ila mtoto aliandika jina lake kama baba mzazi.
Baada ya miezi kadhaa R.I.P. kijana kafariki na baada ya muda mwanamke kaolewa na mwanaume mwingine.
Leo tarehe 22/01/2020 mwanamke aliniita na akawa amenambia kuwa mtoto huyu japo unamtenga na haumhudumii ila ni wako. Alienda mbali na kunambia kuwa Ndugu wa marehemu walimjia kumwambia kuwa marehemu aliwaambia mtoto ni wake.
Yeye aliwakatilia kwa kuwaambia kuwa mtoto huyu ana baba ila sio mtoto kwenu. Ndugu wa marehemu wamegoma na wanaendelea kumtambua kama mtoto wa mtoto wao.
Naomba msaada kama inawezekana Kumpata mtoto kisheria na kubadili jina la baba ili liwe langu.
Yule binti akapata mtu mwingine ambae alidumu naye hadi kajifungua. Sijui walikubaliana nini ila mtoto aliandika jina lake kama baba mzazi.
Baada ya miezi kadhaa R.I.P. kijana kafariki na baada ya muda mwanamke kaolewa na mwanaume mwingine.
Leo tarehe 22/01/2020 mwanamke aliniita na akawa amenambia kuwa mtoto huyu japo unamtenga na haumhudumii ila ni wako. Alienda mbali na kunambia kuwa Ndugu wa marehemu walimjia kumwambia kuwa marehemu aliwaambia mtoto ni wake.
Yeye aliwakatilia kwa kuwaambia kuwa mtoto huyu ana baba ila sio mtoto kwenu. Ndugu wa marehemu wamegoma na wanaendelea kumtambua kama mtoto wa mtoto wao.
Naomba msaada kama inawezekana Kumpata mtoto kisheria na kubadili jina la baba ili liwe langu.