Baada ya kumkataa Rais

Baada ya kumkataa Rais

kwanza kabla ya yote rais wa Tanzania siyo mbunge, kwa kenya sawa, pili ili kuthibitisha hilo rais ataruhusiwa kuingia bungeni pindi tu katiba au mwongozo wa bunge utakapo vunjwa na kuafikiwa na wabunge wote,
hoja yako ya pili ninadhani huelewi vizuri siasa nahujui kuhusu bunge na wabunge, nani anaruhusiwa kuunda kambi ya upinzani, jaribu kwanza kusoma katiba na miongozo yake ndio uwasilishe hoja. wabunge wa chadema hawajachaguliwa na kikwete, wamechaguliwa na wananchi na wapo pale kutetea maslahi ya wananchi,
Tatu nimetambua uwezowako ni mdogo kweli kama ulivyotangulia kusema wewe unadhani siasa ni uadui sisi kama CHADEMA hatuendeshi siasa za uhasama na kusalimiana kwa Dr Slaa na pinda ndo kielelezo tosha kwamba tupo katika kutetea maslahi ya nchi ukijumlisha na pinda kwani naye ni mwananchi.
ANGALIZO:
kama ubongo wako ni wa mgando kimawazo usitumie kuwadanganya hata wale walioelimika, kaa kimya tuachie sisi tunayohitaji mabadiliko na tutayapata yatakusaidia wewe na watoto wako.

Maumivu ya kichwa huanza taaratiibu! nipe paracetamol. hapo umemsizisha! twende kazi.
 
SERIKALI - Rais + Baraza la mawaziri nk.

BUNGE - Spika + Wabunge

MAHAKAMA - Jaji Mkuu + Majaji, Mahakimu, nk.



Sokomoko acha kuaibisha shule uliyosoma.
anaaibisha shule za kata lakini ndio product ya shule za kata hii na tutarajie mengi tu
 
Sokomoko na Ssizy,

Acheni hasira! Bubge ni Rais na wabunge, hiyo haina ubishi, nilisoma hivyo siku za nyuma shuleni, au imebadilishwa? Hata hivyo, wabunge wanawajibika kwa wananchi na ndiyo maana wana haki hata ya kumkataa Rais kwa kura ya turufu, wakiamua uchaguzi unarudiwa...nadhani kwa system ya TZ siyo rahisi.

Nadhani Dr. Slaa na Pinda kusalimiana ni jambo jema, kwani hawa ni wa Tanzania.
 
Angalizo:
Wananchi wazalendo na wapenda maendeleo fanyeni kazi kwa bidii kuinua tija ya maisha yetu wanasiasa wapo zaidi kimaslahi kuliko kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini. Hakuna atakae fanya saruji ishuke bei na hakuna atakae leta maisha bora kwa kila mtanzania bila ya mtanzania huyo kufanya kazi itakayomletea kipato na kujihakikishia maisha bora.
Nawakilisha.[/B]

Nadhani unajikoroga mwenyewe pia. Kwakuwa chadema wanapenda maendeleo ya watu na sio kuchumia tumbo na shikwambi tu kama ccm, ndio maana wakawasihi wabunge wake kuwafanyia kazi kwa dhati wananchi ili waweze kuiona tofauti kati yao na ccm. Kushusha bei ya sementi au mambo mengine naona kwa sasa haliwezekani, ila kinachowezekana ni kuipandisha kutoka 13000 za sasa na kufikia 20,000 kama kawa, kwani hata alipoingia kwa mara ya kwanza sukari ilikuwa 600, na akaipandisha kwa kasi hadi 1800, achilia nyama iliyofika 4000 kwa sasa. Sijui kwa hoja zako unataka tukusaidie je? Ulitaka waseme kuwa hawaendi kuwasemea wananchi na kutetea maslahi yao ili mpate yale mliyoyataka baada ya kuwaziba midomo waliodiriki kusema kweli kama kina 6?

Mbinu za mapambano zipo nyingi, bila shaka na hii ni ya aina yake!
 
kaaaazi kwelikweli.
taratibu jamani kuwaelimisha hawa watu wanajamii wenzetu Sokomoko na Marshal.
wengine wameshasema ufahamu wao ni pungufu ya kizima kwa hiyo let us take these two as a sample to train them for the benefit of the others.and not just to abuse them without a fair final solution,they real need ufahamu na wameshakiri hawafamu kitu.
 
Heshima zenu wanaJF,

Nimesoma habari iliyotolewa na Chadema ya kutomtambua Rais na matokeo ya Urais kwa ujumla. Kitu ambacho kimenistaajabisha au sijakielewa nahitaji kueleweshwa pengine uwezo wangu wa kuchanganua mambo ni mdogo ni kuwa Rais ni sehemu ya Bunge na Wabunge hawawezi kufanya kazi bila kumshirikisha Rais. Unapopitshwa mswada na Bunge Rais anausaini na unakuwa sheria.

Kwa jinsi nionavyo mimi kitendo cha kumkataa Rais na kuendelea kufanya kazi nae kina walakini unless kuna interest ndani yake na hilo nadhani maslahi ndio yanayowafanya Chadema wawe watumwa wa kauli yao. Wanaogopa wakifreez hawatapata ruzuku hawata pata posho za ubunge na za KUB.

Nimefikiria sana na kujiuliza mbona Chadema walikuwa na mchecheto wa kukimbilia kuongoza kambi ya upinzani bungeni na Rais ni sehemu ya bunge na Rais huyo huyo wanadai leo hii hawamtambui? hivi mwenye akili timamu na mwenye ku reason out haoni kuna namna hapo? Mimi ndio maana nimeamua kuachana na sihasa za kibongo kwani zimejaa unafiki mwingi na unaweza kuumia kichwa kwa kufikiria mambo yanvyoenda. Kule visiwani vyama vimeungana hujui nani mshindi nani kashindwa tunaambiwa wote wameshinda. Huku Bara kuna chama kinakataa kumtambua Rais lakini wapo tayari kufanya kazi chini yake! Kuna wengine wanasema eti kile chama cha upinzani kule visiwani ni CCM B kwahili mie nataka nifikiri na hiki kinachofanya mambo kinafki ni CCM C !

Kule visiwani kuna kipindi kama sikosei mwaka 1995 chama kikuu cha upinzani kilisusia matokeo ya uchaguzi na shughuli zote za baraza la uwakilishi na wakatamka bayana hawamtambui Rais tena kwa vitendo sio kwa maneno. Sisemi na Chadema wafanye hivyo laaa maana adhari zake zilikuwa kubwa na zilizopelekea uhasama mkubwa baina ya wananchi huku viongozi wakikuta wanagonga tano refer to Slaa na Pinda nje ya viwanja vya bunge dodoma juzi!

Angalizo:

Wananchi wazalendo na wapenda maendeleo fanyeni kazi kwa bidii kuinua tija ya maisha yetu wanasiasa wapo zaidi kimaslahi kuliko kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini. Hakuna atakae fanya saruji ishuke bei na hakuna atakae leta maisha bora kwa kila mtanzania bila ya mtanzania huyo kufanya kazi itakayomletea kipato na kujihakikishia maisha bora.

Nawakilisha.

Kweli na mimi naamini wewe una upeo mdogo wa kufikiri, kama wewe mwenyewe ulivyosema!Kwa taarifa yako CHADEMA kuunda kambi ya upinzani ni haki yao kwa kuwa hichi ndicho chama kikuu cha upinzani!Kuna mihimili mitatu ya dola,nayo ni parliament,judiciary na excutive.Vyombo hivi hufanya kazi kwa kushirikiana, lakini kila kimoja kina mamlaka na mipaka yake ya kufanya kazi!hivyo kutomtambua rais haina maana ni kutolitambua bunge!!
 
nisaidieni kidogo wana jamii, Hivi huwa wabunge husimama wakati Raisi anapoingia bungeni? Kama ni hivyo nahisi huwa ni ishara ya kumheshimu vile! Je kutokana na hili kambi ya Chadema itasimama au la? Na iwapo watasimama si itakuwa ishara ya kumkubali na kumheshimu kama Raisi? Naomba msaada kwa hili may be!
 
SERIKALI - Rais + Baraza la mawaziri nk.

BUNGE - Spika + Wabunge

MAHAKAMA - Jaji Mkuu + Majaji, Mahakimu, nk.



Sokomoko acha kuaibisha shule uliyosoma.

Sikubaliani na wewe kuhusu bunge.
Nanukuu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Sura ya tatu, sehemu ya kwanza, 62 (1) "Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge."
 
Hivi siku hizi hawafundishi tena somo la siasa au ndo mambo ya shule za kata? eehe Sokomoko!
 
hawawezi kugomea bunge watashindwa kulipa mishahara na gharama za uendeshaji
 
Heshima zenu wanaJF,

Nimesoma habari iliyotolewa na Chadema ya kutomtambua Rais na matokeo ya Urais kwa ujumla. .....

Angalizo:

Wananchi wazalendo na wapenda maendeleo fanyeni kazi kwa bidii kuinua tija ya maisha yetu wanasiasa wapo zaidi kimaslahi kuliko kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini. Hakuna atakae fanya saruji ishuke bei na hakuna atakae leta maisha bora kwa kila mtanzania bila ya mtanzania huyo kufanya kazi itakayomletea kipato na kujihakikishia maisha bora.

Nawakilisha.

Hapo ndipo dhumuni la hoja yako linapoingia shaka. Unajaribu kuwaambia Watanzania wapuuze michakato ya kisiasa ambayo ni muhimu katika kujenga mifumo bora ya uongozi nchini na hapohapo unategemea wafanye kazi yenye tija? Ndugu yangu, ukiwaachia wahuni wachukue hatamu za uongozi wa nchi, hata ufanye kazi kwa bidii, maarifa na nguvu zote, hufiki popote. Utabakia kuwa masikini wa kutupwa huku jasho lako likineemesha hao wahuni wachache. Tena basi, ufanisi ndio sahau kabisa.

Labda unachojaribu kufanya hapa ndio mkakati wa chama tawala kuwaaminisha watanzania kwamba wasijisumbue; hawawezi kubadili chochote kwani wanaochaguliwa kuongoza ni kwa manufaa yao tu hivyo nyie wengine (wapiga kura) mkazanie angalau kushikishwa kitu kidogo (tusenti, kapelo, fulana, kanga na mitandio) wakati wa uchaguzi na kuachia "wanasihasa" waendelee kutumbua nchi bila kuwajibika. Hatuwezi kukubaliana na hoja muflisi kiasi hicho.
 
Haya mambo ya katibe mbovu yanatia kichefuchefu. Hivi mtu akikuibia mali yako na uhakika upo, ushahidi upo halafu unalazimishwa kukubali kuwa hiyo mali aliyoiba kwako ni ya kwake kihalali wakati ushahidi upo utasemaje?
Uhakika wa wizi wa kura upo, sasa tunalazimishwa tumkubali huyo aliyeiba hizo kura. Upupu mtupu jamani wadanganyoka mpaka lini mtazinduka kutoka usingizini?
 
SERIKALI - Rais + Baraza la mawaziri nk.

BUNGE - Spika + Wabunge

MAHAKAMA - Jaji Mkuu + Majaji, Mahakimu, nk.



Sokomoko acha kuaibisha shule uliyosoma.

Kwenye red: nini tofauti kati ya National Assembly na Parliament? Tuwe tunasoma na kuelewa kwanza kabla ya kukosoa hoja ya mtu. Parliament kikao akiwemo na Rais na national assembly kikao bila Rais. Soma ibara ya 62 (1) na 63 (1) ya katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania (toleo la 2005).
 

jamani,
ni kweli hili tangazo la chadema kuwa hawamtambui rais, ambaye amechaguliwa na ametangazwa kikatiba, ni kichekesho cha mwaka na ni jambo la kitoto! Wabunge wenyewe wa chadema wameapa kulinda katiba ya nchi, kama alivyoapa rais ambaye chadema wanasema hawamtambui. Je, wakati rais msiyemmtambua anapokuja bungeni, kikatiba, kuhutubia, chadema mtakuwepo au mtatoka nje? Rais akileta jina la waziri mkuu ili athibitishwe na wabunge, chadema, watatambua kitendo hicho cha rais wasiyemtambua anayetaka apate msaidizi wake, ambaye ni waziri mkuu? Waziri mkuu mwenyewe, aliyeteuliwa na rais (ambaye chadema hawamtambui) na kuthibitishwa na bunge, ndiye atakayekuwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, je chadema watamtambua? Watamuuliza maswali ya papo kwa papo? Mimi nadhani chadema wangefanya vema kutomtambua rais na kutotambua matokeo ya kura za ubunge pia na wakatoka bungeni! Humtambui rais, lakini unatambua bunge, ambalo sehemu yake, kikatiba, ni rais. Acheni danganya toto! Na hawa waaandishi wetu wa habari, akina saed kubenea, wameshindwa hata kumuuliza mbowe na slaa, “the legal implications and interpretation of this move”. Wanaandika tu na kutuletea, kama kasuku! Slaa akisema, wanatuandikia tu, mbowe akisema, wanatuaandikia tu, mtikila akisema, wanatuandikia tu! Hamuulizi hata maswali? Jamani?
bwassa

pole kwa kushindwa kuelewa dhamira nje ya chadema,
1. Katiba na sheria za nchi hii, baadhi ni za kidhalimu, ikiwamo hii ya kutoruhusu mtu au taasisi yoyote kupinga matokeo ya urahisi katika chombo chochote kile. Hii tafsiri yake ni nini? Hata kama una ushahidi wote wa kutosha kuthibitisha aliyeshinda aliiba kura, lkn huwezi kushtaki, kupinga wala kuzuia huyo mwizi wa kura kutangazwa kuwa rais, kuapishwa na kufanya kazi zake kama rais wa nchi. Kwa jinsi hiyo, chadema hata wangetoa machozi ya damu, kikwete pamoja na kuchakachua na hakuna asiyejua hili, bado angetangazwa na kuwa rais. Na ndio maana kwa kujua hilo, wanachofanya ni ku create awareness inside and outside the country kwamba hatukuwa na uchaguzi huru, ili kushinikiza kuundwa kwa katiba mpya na tume huru. Vinginevyo ulitaka watu wabebe mapanga waingie mtaani kupinga matokeo??? Mi nadhani wametumia busara ya hali ya juu. Pia wamesema wabunge, madiwani watafanya kazi zao kama kawaida kwakuwa wamechaguliwa na wananchi, na kazi si tu kujadili miswada na kutunga sheria, pia ni kukemea ufisadi, kuwakilisha matatizo ya wananchi na mengineyo mengi. Naomba uone na uelewe kuwa chama kinapotawala kwa muda mwingi, kitafanya kila liwezekanalo kubaki madarakani, yanahitajika mapinduzi ya kweli ili kuleta mabadiliko. Na huu niliouona ni mwanzo mzuri, ukisema eti na wabunge tuliowapata pia wasishiriki kwenye kazi zao ni sawa na kuwaruhusu hawa watu wafanye wanavyotaka. Hatuwezi kamwe kufanya hivyo, tutawatumia hawa hawa kueneza chama zaidi na kuzidi kuleta elimu na ufahamu mkubwa kwa wale ambao bado hajaelimika.na bado tutaendelea kusema kuwa hatuheshimu wala kutambua mkuu wa nchi aliyejiweka pale kinyume na matakwa ya wananchi. Maana hasa ya kusema hatutambui urais wa kikwete ni kuwa, ukweli unabaki kuwa ameshatangazwa kuwa rais lkn hatumheshimu kama rais aliyestahili kuwa madarakani, sheria ingeruhusu tungemshtaki mahakamani na tungefanya uchaguzi huru. Lkn kwa kuwa hayo yote hayawezekani, that's the best we can do. Katiba mpya, tume huru ya uchaguzi ndivyo tutakavyopigania kwa kuwatumia wawakilishi wetu, wabunge namadiwani.
 
kwanza kabla ya yote rais wa Tanzania siyo mbunge, kwa kenya sawa, pili ili kuthibitisha hilo rais ataruhusiwa kuingia bungeni pindi tu katiba au mwongozo wa bunge utakapo vunjwa na kuafikiwa na wabunge wote,
hoja yako ya pili ninadhani huelewi vizuri siasa nahujui kuhusu bunge na wabunge, nani anaruhusiwa kuunda kambi ya upinzani, jaribu kwanza kusoma katiba na miongozo yake ndio uwasilishe hoja. wabunge wa chadema hawajachaguliwa na kikwete, wamechaguliwa na wananchi na wapo pale kutetea maslahi ya wananchi,
Tatu nimetambua uwezowako ni mdogo kweli kama ulivyotangulia kusema wewe unadhani siasa ni uadui sisi kama CHADEMA hatuendeshi siasa za uhasama na kusalimiana kwa Dr Slaa na pinda ndo kielelezo tosha kwamba tupo katika kutetea maslahi ya nchi ukijumlisha na pinda kwani naye ni mwananchi.
ANGALIZO:
kama ubongo wako ni wa mgando kimawazo usitumie kuwadanganya hata wale walioelimika, kaa kimya tuachie sisi tunayohitaji mabadiliko na tutayapata yatakusaidia wewe na watoto wako.

Unaonaje Sizy ukasoma vizuri katiba toleo la 2005 kabla ya kutoa hoja zako za kumpinga Sokomoko - kwani kwa sehemu kubwa angalizo lako linakuhusu wewe mwenyewe!!!!!!!!!! Sielewi kwa nini wengine wamekushukuru kwa post yako.
 

Jamani,
Ni kweli hili tangazo la Chadema kuwa hawamtambui Rais, ambaye amechaguliwa na ametangazwa kikatiba, ni kichekesho cha mwaka na ni jambo la kitoto! Wabunge wenyewe wa Chadema wameapa kulinda Katiba ya Nchi, kama alivyoapa Rais ambaye Chadema wanasema hawamtambui. Je, wakati Rais msiyemmtambua anapokuja Bungeni, kikatiba, kuhutubia, Chadema mtakuwepo au mtatoka nje? Rais akileta jina la Waziri Mkuu ili athibitishwe na Wabunge, Chadema, watatambua kitendo hicho cha Rais wasiyemtambua anayetaka apate msaidizi wake, ambaye ni Waziri Mkuu? Waziri Mkuu mwenyewe, aliyeteuliwa na Rais (ambaye Chadema hawamtambui) na kuthibitishwa na Bunge, ndiye atakayekuwa kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni, je Chadema watamtambua? Watamuuliza maswali ya Papo kwa Papo? Mimi nadhani Chadema wangefanya vema kutomtambua Rais na kutotambua matokeo ya kura za Ubunge pia na wakatoka Bungeni! Humtambui Rais, lakini unatambua Bunge, ambalo sehemu yake, kikatiba, ni Rais. Acheni danganya toto! Na hawa waaandishi wetu wa Habari, akina Saed Kubenea, wameshindwa hata kumuuliza Mbowe na Slaa, “the legal implications and interpretation of this move”. Wanaandika tu na kutuletea, kama kasuku! Slaa akisema, wanatuandikia tu, Mbowe akisema, wanatuaandikia tu, Mtikila akisema, wanatuandikia tu! Hamuulizi hata maswali? Jamani?
Bwassa

Lenin once said, we have to take one step back in order to take two steps forward. Alisema haya akimaanisha ni lazima waingie kwenye ubepari ili kujenga msingi wa taifa lenye viwanda na kisha kutimkia kwenye ukomunist ambao kaulimbiu yake ni each according to his needs. Hivyo usione chadema wako bungeni na wakati huo hawamtambui rais. Wako kwenye mkakati wa kupigania katiba mpya na hilo litafanyika ndani ya bunge!
 
Hebu fikiria kama Kikwete na CCM wameweza kuiba kura na kufanya udanganyifu mkubwa ili kulinda maslahi yao, Je,hawatashindwa kufanya maamuzi mengine kuwakandamiza wananchi? Ndio maana pamoja na kutomtambua rais na serikali, CHADEMA lazima wabaki bungeni kuwawakilisha wananchi na kuwatetea dhidi ya udhalimu mwingine wa serikali.
Ulitaka wasusie bunge ili wananchi tubaki defenseless?
 

Jamani,

Mnapotoa michango humu, muwe mnaelewa mambo, siyo mnapiga porojo tu! Kuna mtu humu amesema Bunge ni Bunge na Rais ni Rais. Angalieni Katiba ya Jamhuri ya Muungano inavyosema:-

Ibara 62.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ambalo litakuwa na sehemu mbili, yaani Rais na Wabunge;
Ibara 63. – (1) Rais kama sehemu moja ya Bunge, atatekeleza madaraka aliyokabidhiwa na Katiba hii kwa ajili hiyo.

Je, haya Dk. Slaa, ambaye aligombea Urais, hayajui? Je, aliyejipachika Mkuu wa Upinzani katika Bunge, Freeman Mbowe, kwa uroho na uchoyo wa madaraka bila ya kuvishirikisha vyama vingine mashuhuri kama CUF, hayajui haya? Unamkataaje Rais, lakini unakubali kuwa Mbunge? Na hawa ndiyo watu waliotaka waongoze Dola! Wanaapa kwa Katiba ambayo hawaijui? Bora wameshindwa! Tungepta taabu sana nchi hii!
Suala Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya, halihusiki sasa hivi hivi baada ya matokeo! Dk. Slaa na Chadema, walitakiwa wakatae tangu mapema kushiriki uchaguzi kwa kuwa “Tume siyo huru” na “Katiba haifai”. Mnaingia mashindanoni, mnashinda Viti vya Ubunge ili kuogeza ruzuku, mnakubali matokeo na kuapa kuilinda Katiba mkiwa Wabunge (Tume ni ile ile na Katiba ni ile ile); mnashindwa Urais mnasema: “Tume mbovu…Katiba haifai… kura zimechakachuliwa…! Ni sawa na mechi ya mpira, unafungwa mabao, unasema Sheria 17 za FIFA hazifai tena; Refa ametuuma! Tena anayeyasema hayo siyo Kamisaa wa Mchezo bali Kapteni wa Timu iliyoshindwa! Jamani!

Bwassa
 

Jamani,
Ni kweli hili tangazo la Chadema kuwa hawamtambui Rais, ambaye amechaguliwa na ametangazwa kikatiba, ni kichekesho cha mwaka na ni jambo la kitoto! Wabunge wenyewe wa Chadema wameapa kulinda Katiba ya Nchi, kama alivyoapa Rais ambaye Chadema wanasema hawamtambui. Je, wakati Rais msiyemmtambua anapokuja Bungeni, kikatiba, kuhutubia, Chadema mtakuwepo au mtatoka nje? Rais akileta jina la Waziri Mkuu ili athibitishwe na Wabunge, Chadema, watatambua kitendo hicho cha Rais wasiyemtambua anayetaka apate























msaidizi wake, ambaye ni Waziri Mkuu? Waziri Mkuu mwenyewe, aliyeteuliwa na Rais (ambaye Chadema hawamtambui) na kuthibitishwa na



















Bunge, ndiye atakayekuwa kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni, je Chadema watamtambua? Watamuuliza maswali ya Papo kwa Papo? Mimi nadhani Chadema wangefanya vema kutomtambua Rais na kutotambua matokeo ya kura za Ubunge pia na wakatoka Bungeni! Humtambui Rais, lakini unatambua Bunge, ambalo sehemu yake, kikatiba, ni Rais. Acheni danganya toto! Na hawa waaandishi wetu wa Habari, akina Saed Kubenea, wameshindwa hata kumuuliza Mbowe na Slaa, “the legal implications and interpretation of this move”. Wanaandika tu na kutuletea, kama kasuku! Slaa akisema, wanatuandikia tu, Mbowe akisema, wanatuaandikia tu, Mtikila akisema, wanatuandikia tu! Hamuulizi hata maswali? Jamani?

Bwassa




Bado una akili zile zile haujabadilika tu Bwassa...

Angalia Kikwete alimsimamisha Mramba kuwa wananchi wampigie kura wananchi wakakataa wakachagua Mzee sela....

Maana yake kuna vitu viwili hapa na ndio maana mijitu ya CCM na lichama lao zinashindwa kutofautisha....
Ngoja nijaribu kutumia mfano wa darasa la kwanza........
Bunge na Rais ni watoto wa Nyumba moja.... nyumba hiyo ni WANANCHI... means wabunge wamechaguliwa na wananchi na rais amechaguliwa na wananchi....
Bunge linauwezo wa kupiga kura ya kutokuwa na Imani na rais ... Lakini Rais hana mamlaka juu ya Mbunge aliyechaguliwa na wananchi...

sasa basi Chadema hawezi kususia kazi aliyotumwa na wananchi kwa sababu ya Rais ambaye nae amechaguliwa na wananchi...
Yeye ameeleza Boss wao kwa vitendo ambaye ni wananchi kwamba huyu mtoto wako ni Mwizi....aliiba baraka za mtu mwingine na sio vingine....
wabunge wataendelea kuwepo ila hawamtambui rais, watafanya walichotumwa na wananchi basi.................

Yani Ukiwa CCM hata kama una akili kiasi gani unakuwa Bumunda sijui kuna laana imepita huko..................
Hawa watu wa CCM makao makuu Dodoma wanakimbizana Halimashauri kuomba hela ya Mafuta ya gari ni ugonjwa au ndo ufisadi uliokidhiri??:A S angry:
 
quote_icon.png
Originally Posted by Sokomoko
Heshima zenu wanaJF,

Nimesoma habari iliyotolewa na Chadema ya kutomtambua Rais na matokeo ya Urais kwa ujumla. Kitu ambacho kimenistaajabisha au sijakielewa nahitaji kueleweshwa pengine uwezo wangu wa kuchanganua mambo ni mdogo ni kuwa Rais ni sehemu ya Bunge na Wabunge hawawezi kufanya kazi bila kumshirikisha Rais. Unapopitshwa mswada na Bunge Rais anausaini na unakuwa sheria.

Kwa jinsi nionavyo mimi kitendo cha kumkataa Rais na kuendelea kufanya kazi nae kina walakini unless kuna interest ndani yake na hilo nadhani maslahi ndio yanayowafanya Chadema wawe watumwa wa kauli yao. Wanaogopa wakifreez hawatapata ruzuku hawata pata posho za ubunge na za KUB.

Nimefikiria sana na kujiuliza mbona Chadema walikuwa na mchecheto wa kukimbilia kuongoza kambi ya upinzani bungeni na Rais ni sehemu ya bunge na Rais huyo huyo wanadai leo hii hawamtambui? hivi mwenye akili timamu na mwenye ku reason out haoni kuna namna hapo? Mimi ndio maana nimeamua kuachana na sihasa za kibongo kwani zimejaa unafiki mwingi na unaweza kuumia kichwa kwa kufikiria mambo yanvyoenda. Kule visiwani vyama vimeungana hujui nani mshindi nani kashindwa tunaambiwa wote wameshinda. Huku Bara kuna chama kinakataa kumtambua Rais lakini wapo tayari kufanya kazi chini yake! Kuna wengine wanasema eti kile chama cha upinzani kule visiwani ni CCM B kwahili mie nataka nifikiri na hiki kinachofanya mambo kinafki ni CCM C !

Kule visiwani kuna kipindi kama sikosei mwaka 1995 chama kikuu cha upinzani kilisusia matokeo ya uchaguzi na shughuli zote za baraza la uwakilishi na wakatamka bayana hawamtambui Rais tena kwa vitendo sio kwa maneno. Sisemi na Chadema wafanye hivyo laaa maana adhari zake zilikuwa kubwa na zilizopelekea uhasama mkubwa baina ya wananchi huku viongozi wakikuta wanagonga tano refer to Slaa na Pinda nje ya viwanja vya bunge dodoma juzi!

Angalizo:

Wananchi wazalendo na wapenda maendeleo fanyeni kazi kwa bidii kuinua tija ya maisha yetu wanasiasa wapo zaidi kimaslahi kuliko kuwakwamua wananchi kwenye lindi la umasikini. Hakuna atakae fanya saruji ishuke bei na hakuna atakae leta maisha bora kwa kila mtanzania bila ya mtanzania huyo kufanya kazi itakayomletea kipato na kujihakikishia maisha bora.

Nawakilisha.

Salute Sokomoko!
Kwanza nimefurahi kuona Avatar yako,may be kuna ukweli fulani katika hiyo Avatar!Guess what??Chura wako Kastarehe anakuna kitambi,hiyo inamaanisha karidhika na hawezi fikiria kitu kingine zaidi ya Tumbo.

Pili,hizi title labda zibadilishwe na kuwa wanajamvi wote kuwa na Title moja,Maana JF senior Expert Member haiendani ni kiwango chako cha uchambuzi uliofanya!
Tuzungumzie mfano mdogo:Binti yako akiwa na mahusiano na mtu ambae wewe humtambui/ama humtaki au humkubali kwa sababu yoyote ile(hii hutokea mara nyingi) ,Je kwa bahati mbaya ama nzuri binti kapata mimba mtoto atakae zaliwa utamtambua kama mjukuu ama la,Je kuzaliwa kwa huyo mtoto kutakufanya ubadilishe msimamo kwa sababu yule bwana ambae wewe humkubali kazaa na binti yako,utakuwa tayari kumwita mkwe??
Refer Hoja ya mwanzo kabisa ambayo Slaa (Phd) alizungumza,Yeye hana shida na Kikwete kuwa Rais ila hawezi kuyatambua Matokeo ambayo ni ya Kupikwa na NEC na hivyo hawezi kumtambua kikwete kama Rais kwa sababu rahisi,hakushinda kwa matokeo halali ya wapiga kura!
Kwa Hiyo ulitaka Slaa aite nguvu ya umma kuingia barabarani kupinga Matokeo kama ilivyokuwa Kenya na Sehemu zingine walizomwaga damu??Kuwa mwana siasa ni pamoja na kutambua na kuweka Maslahi ya nchi mbele zaidi kuliko maslahi binafsi.Kwa Taarifa yako kama CHADEMA wangesimama na kuita nguvu ya umma kuhoji uhalali wa matokeo,na uhakika usingekuwa na amani uliyonayo wewe leo!Kuliko Kubeza Maamuzi nafikiri ungekuwa muungwana sana kuwapongeza CHADEMA kwa Ustahimilivu wa Kisiasa na Kuweka Maslahi ya nchi mbele Kuliko hata NEC and Co. ambao waliweka maslahi biafsimbele kuliko maslahi ya taifa.

Kikwete ataendelea kuwa Rais kwa Mujibu wa katiba mbovu tuliyonayo ambayo Raisi anajitangazia ushindi kwa sababu NEC ni chombo kilicho chini yake na wakuu wake wote ni wateule wa Rais unategemea watamtosa??Kumtambua Rais aliyeko madarakani ni sawa nakukubaliana na matokeo ya kupikwa na ya kishabiki ambayo NEC kwa sababu wanazojua wao wameamua kuyabadili yaendane na vile wanavyojua wao( mimi na wewe hatujui). Hata kama Slaa(Phd),angesmshinda 'Dr' kikwete kwa matokeo ya staili ile,bado watu tungepinga kwa sababu tunachohitaji ni Haki. Mbona CCM wameshinda Zanzibar kwn umesikia kuna mtu anasema hamtambua Shein??Kama kikwete 'dr' angeshinda bila zengwe wala kura zenye utata watu wangeheshim na kumtambua kama Rais wao!CHADEMA walikubali kushindwa mwaka 2005 na walikubali na kumtambua Rais na kumheshimu,je ulihoji kwa nini walimtambua??Don't look suprised if people can stand and raise up their Voices to fight for their constitutional rights!
Tambua Bunge na Rais ni systemy 2 tofauti so,Rais sio mkuu wa Bunge wala si mmbunge na anaingia Bungeni kwa ruhusa maalum!


Kama dhamira ya sokomoko ni kuelimishwa basi atakuwa amepata elimu kubwa isiyo na malipo, na kama hii siyo dhamira yake basi huna budi kumuelisha kiasi hiki. big up Mbalinga
 
Back
Top Bottom