Baada ya kujitenga na mirathi ndugu zangu wamenitenga

Baada ya kujitenga na mirathi ndugu zangu wamenitenga

Vikao vyenyewe siku hizi hata sishirikishwi na vile vya kila mwaka ambavyo tuliviweka ambapo ndugu wote tunakuwepo hata aliembali lazima aje havikaliwi cha mwaka huu naona kimepita kimyakimya
Sasa ndio unatakiwa u-initiate kikao mkutane uwaweke wazi ili waelewe na waanze kukuelewa vizuri sababu ukiendelea kukaa kimya na wao hawajui ukweli halisi inakua inakua haileti picha nzuri.

Unatakiwa kusema mbele ya hao wahusika ukweli ulivyo na wao wajibu kwamba unasema ukweli au sio ukweli, shida inaonekana ni kwamba wewe unawaogopa hao kaka zako wapigaji au unawatunzia siri na huku wao wanakuangalia na kukutangaza wewe km mbaya na haufai. Njia pekee ni kuyasema hayo kwenye kikao cha wote sio kumwambia mtu mmoja mmoja hayo yasemwe mkiwa wote mmekusanyika kwenye kikao ili muanze kuelewana na kuacha kutengana.
 
Habari wakuu,

Huwa napenda kutoa baadhi ya matukio ya maisha yangu ili kupata ushauri na pia kama rejea au funzo kwa watu wengine katika jamii au jf

Kuna kipindi nilikuja humu kuomba ushauri wa namna ya kuifanya familia yangu kuwa familia kubwa yenye kuigwa, nashukuru nilipata ushauri na mwingine niliufanyia kazi miongoni mwao ni kuwa nilifanikisha kukaa na wanafamilia tukatengeneza katiba na kuchaguana viongozi ili kuendesha mirathi kimfumo wa utawala na demokrasia

Hivyo tulianza utekelezaji ambapo mwenyekiti ndio mtu mkubwa katika kutekeleza majukumu ya kifamilia endapo alichaguliwa kwa kura ya siri na pia alikuwa sio mkubwa wetu kwa kuzaliwa pamoja na viongozi wengine tukapeana majukumu mbalimbali katika kusimamia mirathi na kuanzisha miradi mingine kutokana na ukusanyaji wa mapato

Mimi nilikuwa miongoni mwa viongozi pia kwani katika kuchaguana hakuna aliyeachwa bila cheo chochote yani wote tulichaguana kulingana na nafasi za uongozi na majukumu, kwa upande wangu nilikuwa mkusanyaji wa pesa ambapo nipo na dada yangu ambae yeye ndio mkusanyaji mkuu mimi ni msaidizi wake

Sasa kilichofanya nijitoe katika uongozi ni baada ya kuona kaka zetu wakubwa kiumri na sio kivyeo (japo mmoja ndio mwenyekiti yani anaefuatia kwa ukubwa) wanahujumu jitihada za ukusanyaji ambapo ili wewe mkusanyaji uipate hiyo pesa iingie kwenye mfuko wa familia mpaka ugombane nao maana wanataka kuimanupulate ili kuzurumu au kuchakachua kabla haijaingia kwenye mfuko wa familia

Kumbuka katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi tumefanikiwa kupata wawekezaji wa eneo letu na walijenga flemu za biashara kwa mikataba na pia kuna maeneo mengi tulipangisha kwa wafanyabiashara hivyo mapato yameongezeka tofauti na kipindi cha nyuma kabla ya uongozi

Sasa baada ya kujiuzulu au kujitoa katika uongozi kwa sababu nilizotaja hapo juu ndugu zangu hawanishirikishi chochote kinachohusu familia hata kama hakigusi mirathi moja kwa moja mfano matukio ya kifamilia kama harusi, ugonjwa na hata au baadhi ya misiba. Yani kujitoa kwenye uongozi ni kana kwamba nimejivua undugu hizi jamii zetu shida sana

Nini maoni yako mdau mimi ndio mwenye shida au ndugu wa familia karibu kwa ushauri
Watakapoanza kugombanaia mali waakuita. Nawe, uwatenge ili usijichafue.
 
Sasa ndio unatakiwa u-initiate kikao mkutane uwaweke wazi ili waelewe na waanze kukuelewa vizuri sababu ukiendelea kukaa kimya na wao hawajui ukweli halisi inakua inakua haileti picha nzuri.

Unatakiwa kusema mbele ya hao wahusika ukweli ulivyo na wao wajibu kwamba unasema ukweli au sio ukweli, shida inaonekana ni kwamba wewe unawaogopa hao kaka zako wapigaji au unawatunzia siri na huku wao wanakuangalia na kukutangaza wewe km mbaya na haufai. Njia pekee ni kuyasema hayo kwenye kikao cha wote sio kumwambia mtu mmoja mmoja hayo yasemwe mkiwa wote mmekusanyika kwenye kikao ili muanze kuelewana na kuacha kutengana.
Sawa mkuu nitaufanyia kazi ushauri wako
 
Watakapoanza kugombanaia mali waakuita. Nawe, uwatenge ili usijichafue.
Sio muda tu maana mpaka tunashiriki kuweka uongozi kaka wakubwa walitaka kuweka rehani nyumba kwa ajili ya tamaa zao dada wakashituka ndio kuanza kutushawishi sisi wengine ambao hata hatukuwa na shobo na mambo za mirathi
 
Nimekuelewa we hujanielewa mimi.

Waambie nduguzo mgawane, mirathi inapendeza igawiwe pale pale.. huko mbele ya safari tatizo litakuwa kubwa kwa watoto wenu na wajukuu
Nimeamua kukaa mbali nayo najua mishe zangu cha kushangaza bado natengwa
 
Back
Top Bottom