Baada ya huu mshikemshike, watakutana kweli?

Ufisadi wa Chadema umewaathiri vipi Watanzania? Na hii Serikali haramu iliyojaa magaidi inashindwa vipi kuwakamata majambazi ndani ya Chadema na kuwafungulia kesi za ujambazi badala yake inaishia kuwabambikia kesi FEKI!? Acha kuonyesha ujuha wako hadharani.

Ni wapi hamna ufisadi TZ hii? Huko kwenye vyama vyenu ndiyo majambazi yamejificha. Kama siyo mzee wa kiumri basi ni mzee wa jf (ref lini ulijiunga)
 
Binafsi nilihisi CDM walitaka kumpima huyu mama kama ana ubavu, yule kijana Mdude aliyeachiwa kutoka gerezani kauli yake binafsi ilinikera sana, nilianza kuhisi harufu ya kutaka kumjaribu mama, yanayoendelea kwa sasa tuliyatarajia baada ya kuona kasi ile.....la kustaajabisha huyu mama alionekana muungwana sana ila wanaume wakataka kumshika makalio....sasa nadhani tunakoelekea si penyewe yetu macho.....
 
Akilihutubia bunge, Rais Samia aliahidi kukutana na vyama vya siasa, si chama kimoja au kiongozi wa chama fulani. Katika hivyo vyama kuna CCM, CHADEMA, CUF, SAU, ADC, nk.; na hakutaja siku, tarehe, mwezi wala mwaka wa kukutana.

Atakapoitisha kukutana na vyama hivyo, yeyote atawakilisha, si lazima awe kiongozi wa chama ngazi ya juu.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Rais alianza kazi kwa kuonesha upendo na uungwana wa hali ya juu. Kitendo hili likatafsiriwa na chadema kama unyonge na wakaanza kumtolea lugha ya dharau. Alianza Mdude, akaja Mbowe kwa kumpangia Rais akutane nao haraka! . Choko mchokoe pweza
 
Hoja yako, Nyani, unataka wasikutane au unashangilia kwamba mkutano huo hautakuwepo?! Ni sawa kwa wapigania legacy mkutano ule ungepunguza punguza! Usicheke mapema lakini, kesho tu wanasiasa wanaweza kukushangaza!
 
Tatizo Mbowe alikuwa na haraka sana ya kukutana naye..."mama" alivyoanza kuupiga mwingi akaona yeye na wenzake wanapoteza relevancy wakabadili gia angani na kuanza kudai katiba mpya kwa ubabe huku akijua kabisa matokeo yake.
CHADEMA wanamdharau sana Rais SSH kwa kuwa ni mpole, wanataka afuate matakwa yao. Hapana akifanya hivyo atakuwa siyo Rais wa Tanzania. Freeman Mbowe yeye mwenyewe hachezewi hivi akiwa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Tumemuona alivyolinda kiti chake cha UENYEKITI mpaka kwa kumwaga damu. Kwa nini wasimsikilize Rais SSH aliposema Katiba isubiri kwanza ajenge uchumi?

Mbona waliufyata kwa Mwendazake ambaye alikuwa katili kupitiliza? Wananchi watawachoka kwa kuwa chama cha harakati na matukio. Kajipangeni namna ya ku-deal na Rais SSH. Wananchi wanamkubali anavyochukua hatua kupanga uchumi.

Na Katiba hajakataa, kasema nipeni muda.

Lakini akina Mbowe wanataka wamuendeshe kama gari bovu? Anadhani Rais SSH ni kama akina Catherine Ruge wa BAWACHA?? HAPANA huyu ni Rais wa Tanzania na anayoyafanya tunayaona
 
Hahahahahajaha si mbowe alivyotoka msiban Moshi akaelekea Mwanza moja kwa moja akasema akamatwe yeye sasa 😂😂😂😂😂😂 mtoto akililia wembe mpe umkate

Angetulia tu kwanza maana nchi ina pitia mengi magumu yy kazi yake kutupigia kelele tu
 
Ulitaka Chadema wasikemee uvunjifu wa sheria kwasababu palikuwa na miadi ya kukutana na Rais?

Wacha ushamba.
Hivi mbowe na sabaya kwa sasa wana tofauti?
Mbona mmemsahau sabay na kesi inaendelea?
 
Buddah kenya kuna katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ila what is always happening kwenye kila uchaguzi?
 
USIKURUPUKE kuja kuonyesha ujuha wako hadharani. Kama hujui kitu ULIZA!!!
Buddah kenya kuna katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ila what is always happening kwenye kila uchaguzi?
 
Kashapoteza akili huyu bibi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…