Baada ya Bunge live kupigwa stop, Mawaziri wa Magufuli wahaha kutafuta Video zao na Audio

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
Ile kauli ya mtu kukata tawi alilokalia, imeanza kuwatokea Wabunge na Mawaziri wa CCM. Hali ya bunge kufanyikia backstage, imewafanya Mawaziri Waanze kuhaha kutafuta Video, Audio zao hasa zile walizoongea wakiwa ndani ya Bunge ili wazishee kwenye Mitandao ya Kijamii. Wapiga picha wa Bunge wamekuwa Wakisumbuliwa na Mawaziri ili wawape vipande vya sehemu walizoongea wao tu. Hii ni baada ya Mawaziri hao kukosa Mvuto kwa jamii, hivyo wanadhani Kuonekana kwao kwenye mitandao kutawarudishia hua kwenye jamii.

Ndo maana Sasa Mkitembelea kurasa za Mawaziri na manaibu waziri katika mitandao ya kijamii, mtakuta video, audio, maandishi ya kile walichokifanya bungeni tofauti na ilivyokuwa hapo mwanzo. Hii inadhihilisha waliunga mkono Bunge kufungiwa kuoneshwa bila kujua wafanyalo.

Hali hii imeongeza mwanya wa Rushwa Kwa Watendaji wa bunge kwa kile wanachosema nipe ile video yangu ntakupoza. Naomba TAKUKURU sasa mkunjue makucha. Kama mwataka muonekane na msikike, ruhusu live
 
Kwani mawaziri wameanza kuongea Bungeni?, mimi nilikuwa sijui, waziri mkuu naye ametoa bajeti yake?, mweeee tunapitwa na mengi jamani
 
Viva UKAWA.Hii ya kutokurusha Bunge live itaathiri sana wabunge na mawaziri wa CCM kwa sababu kuna Maneno mengi ya uongo watazushiwa na wenzao, na wananchi bila kujua wataamini kabisa Moja kwa moja kuwa hayo wanayoambiwa ni ya kweli 100%.CCM hili la bunge kutokuwa live ni hatari sana kwenu kuliko kwa wenzenu wa upinzani.
 
daah yan ccm wameharibu kweli sasa naona wataaandaa mswada wa censorship ya social medias
 
Kwani mawaziri wameanza kuongea Bungeni?, mimi nilikuwa sijui, waziri mkuu naye ametoa bajeti yake?, mweeee tunapitwa na mengi jamani
Ata sielewi jirani yangu labda tuwaulize makamanda uchwara Ritz, elizaboni,na stroke hawa ndio wanafiki na wachumia tumbo wa watala labda wanaweza kutujuza kinachoendelea.
 
YAANI MUDA HUO NIACHE YA ADAM NA EVA NIANGALIE UPUUZI NEVER !
 
Mwigulu.png
 
Back
Top Bottom