hii ndo ile ukiona neno gumu unadhani kwamba ni bonge la kozi!!Kama uhijuh kwanini uliomba?!
Siku 14 baada ya official date ya kufungua Chuo kuna nafasi ya kuhama. Ila inategemea na uhitaji wa unapoenda na kama hakuna madhara unapotoka. Pia kigezo cha ufaulu kinachohitajik ktk kozi husika, unaandika barua kuonesha uhutaji wako na kwanini that's all.Kubadilisha mkuu ni sawa ila sijajua unabadilisha kwa mtindo wa upi ninavojua labda kuomba tena lakini apo nielezee kuhusu apo
Kuna vitu vya ajabu sana mtu anachagua course hajui inahusu nn.Ingekua zaman sawa coz wasomi walikua wachache,lkn saiz wasomi ni wengi mno cha ajabu dogo sijui ujuaji au ndo ubishi anajichagulia micourse ya ajabu ajabu mwisho anaanza kulialia. We nenda tu chuo kakarr mistori ya mijitu ya zaman. Ukirudi kitaa uje usugue vizur
Dah man uliomba course kisa jina limekaa kiinteresting au.. yani apo utazingua baba,, hizo zinalipa mambele sio kibongo bongo shughuli za iyo anthrropology azina soko sana,,anywats anthropology ni ile act mtu unaenda ishi kwenye jamii flani kwa lengo la kupata certain stuff iliyokupeleka hapo..utaishi nao na pia kujifunza lugha zao na kuadapt maisha yao...etc.... Ila hujalost sana ukifika chuo week mbili za mwanzo fanya mchakato uamie course nyingine inafaa fanya utafiti kwanza usije jutia
Anthropology ya UDSM wanafunzi huchagua kuanzia mwaka wa pili mkondo mmoja wapo: Medical anthropology (Afya), Political anthropology (Siasa) au Society and Environment (Jamii na Mazingira). Soma prospectus ya UDSM utaona mtiririko na mpangilio wa course zake. Nafikiri inauhusiano fulani na sociology (ziko idara moja), na wengi wanavyo fikiria humu sivyo wanamawazo yale ya anthropologist wanaosomea makabila fulani ambao hutoka ulaya na kuzamia huko vijijini. Hiyo bado ni anthropology lakini anthropology ni pana. Anthropologist ni wazuri kwenye qualitative research na ni vizuri upende utafiti. Chuo cha UDSM ndo chuo cha kwanza kuanzisha hiyo program hata kama kuna degree nyingine zenye elements ya anthropology. Kwa upya wake ni vigumu kwa wengi kujua inahusu nini na ajira zake zikoje. Kule Kenya kuna vyuo zaidi ya 5 hutoa degree za Anthropology (BA na MSc hata PhD). Kwa upya wake inakuwa ni risk kiasi kuisoma lakini wengine kwenye risk ndo huona opportunities.
Usiende chuo na wazo la kubadilisha kwani sio rahisi kama wengine wanavyo fikiria. Uwe tayari kuisoma hiyo program inayokupeleka chuo pale maombi yako ya kubadilisha yatakapo kwama ukiwa na bahati waweza badilisha. Fanya maamuzi.
Nani kakushauri kusoma vijikozi vya kiswahili namna hii? Yani umekubali kwenda kusomea mali kale, uwe msimulizi kwenye makumbusho ya kihistoria kule bagamoyo namna waarabu walivyowatesa babu zetu kwa biashara ya utumwa?
Kama hauna passion na hii kozi, it's better uipige chini tu.