Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Huyu binti wa rafiki yangu anaitwa Shangwe. Shangwe ni binti anaevutia sana. Amemaliza kidato cha sita ingawa matokeo yake hayakuwa mazuri sana. Wakati wazazi wanafikiria cha kufamfanyia binti yao kwa maisha yake Shangwe alikutana na Dickson wakiwa kanisani. Dickson alimuelewa sana Shangwe.
Dickson alipata nafasi ya kwenda kusoma South Africa, akisomeshwa na kampuni. Baada ya kukaa miezi miwili huko Sauzi alimtumia Shangwe ticket apande pipa kwenda kuvinjari.
Shangwe alipotapa ticket alimuuliza Dickson nitawaaga wazazi wangu kuwa ninakwenda wapi na kwa nani? Mimi ninakuja kukutembelea kama nani?
Dickson alimuuliza nikituma ndugu walete barua ya posa kwenu itakuwaje?
Hivi ndivyo Shangwe alivyopata mume.
Dickson alipata nafasi ya kwenda kusoma South Africa, akisomeshwa na kampuni. Baada ya kukaa miezi miwili huko Sauzi alimtumia Shangwe ticket apande pipa kwenda kuvinjari.
Shangwe alipotapa ticket alimuuliza Dickson nitawaaga wazazi wangu kuwa ninakwenda wapi na kwa nani? Mimi ninakuja kukutembelea kama nani?
Dickson alimuuliza nikituma ndugu walete barua ya posa kwenu itakuwaje?
Hivi ndivyo Shangwe alivyopata mume.