Azimio la Arusha: Kuzaliwa upya?

Tatizo kubwa liko kwenye kipengele (d) Ujamaa ni Imani:
Kinasema: “Lakini Ujamaa hauwezi kujijenga wenyewe. Kwani Ujamaa ni imani. Hauna budi kujengwa na watu wanaoamini na kufuata kanuni zake….. Wajibu wa kwanza wa mwana-TANU na hasa kiongozi wa TANU ni kutii kanuni hizi za Ujamaa hasa katika maisha yake mwenyewe. Na hasa mwana-TANU kiongozi hataishi kwa jasho la mtu mwingine au kufanya jambo lolote ambalo ni la kibepari au kikabaila

Kipengele hicho kinamalizia na: “Utimizaji wa shabaha hizo na nyinginezo zinazofuatana na siasa ya Ujamaa unategemea sana viongozi kwa sababu Ujamaa ni imani na ni vigumu kwa viongozi kujenga siasa ya Ujamaa ikiwa hawaikubali imani hiyo

Viongozi wengi hawakuwa waumini wa dhati ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Walikuwa wanafiki na wabinafsi. Hawakulipenda Azimio la Arusha tangu mwanzo kwa sababu waliona linawabana. Pia wapo wengine ambao walikuwa ni bendera tu yafuata upepo. Hao ndio wale ambao hawakuweza hata kujifunza Siasa ya Ujamaa maana yake ni nini. Kwa hiyo, hawakuweza hata kuwafundisha ama kuwaeleza wananchi kinaganaga juu ya manufaa ya Siasa ambayo Chama chao kilikuwa kikifuata.

Wapo wengine ambao walikuwa na imani kubwa na Mwalimu Nyerere kutokana na msimamo aliokuwanao wa kujali sana maslahi ya wanyonge. Wapo pia ambao kwa kutokuwa na elimu ya kutosha na uelewa mdogo wa mambo ya Siasa, walikuwa wakifuata tu alichosema Mwalimu Nyerere bila kuelewa yale kiongozi wao aliyokuwa akiyasimamia. Hawa ndio wale waliokuwa wakiimba kama kasuku “Zidumu Fikra …..” Ukiwauliza ni fikra gani hawajui, hawana cha kueleza.

Lakini kuna kundi lingine ambalo walimchukia Mwalimu kwa kuwa aliwazidi kwa akili na kuwa na upeo mkubwa wa kufikiri na kuelewa mambo. Wengine walikuwa na chuki binafsi kwa kuwa pengine Mwalimu katika kutekeleza kazi zake za uongozi aliwahi kuwachukulia hatua kali ama kuwaumiza wao au jamaa zao. Kundi hili kwa chuki tu, liliweza kubeza na kupinga hata yale mazuri Mwalimu aliyoyasimamia. Wapo na wengine ambao walijiona kwamba hata wao walikuwa na mawazo mazuri kuzidi ya Mwalimu, lakini Mwalimu hakuyatilia maanani ama aliyapinga na akayajengea hoja ya kwake yeye, na kuibuka mshindi wa hoja; ama kwa sababu ndiye aliyeshika rungu la uongozi, kulazimisha yake aliyoyaamini yeye.

Matokeo yake, katika kujadili kushindwa kwa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, na Azimio la Arusha, wakawepo watu ambao bila kujua kwa undani madhumuni ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea iliyozaa Azimio la Arusha, ama kwa sababu nyingine yoyote waliamua kwamba Siasa hiyo ndiyo iliyoliletea umaskini nchini, na Azimio halikuwa muhimu wala halikuwa na manufaa kwa Taifa.

Hivi sasa, viongozi wa vyama vya Siasa, wasomi na wananchi wasioridhika na jinsi Serikali ya CCM inavyoendesha shughuli za nchi, hususan kwenye masuala ya ufisadi na matabaka yaliyojitokeza dhahiri ya Matajiri wa kutupa na Maskini wasiojua kesho watakula nini na watoto wao, na kadhalika, wamegundua kwamba kumbe Azimio la Arusha lilikuwa na mantiki. Pia, wapo wanaogundua kwamba Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea haikuwa na ubaya wowote, isipokuwa viongozi wa TANU na CCM waliopaswa kuwa mstari wa mbele katika kuijua, kuitetea na kuitekeleza hawakufanya hivyo kwa dhati. Kutokana na ubinafsi wao, hawakuwa na waumini wa kweli wa Itikadi waliyoamua wenyewe kuifuata!

Ili tuendelee tunahitaji Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora!

Kwenye waraka wangu niliongelea haya:
Kurudisha na kuimarisha Heshima, Utu na Uadhi ya Mwananchi na Taifa la Tanzania
Kurudisha na kuimarisha Heshima, Wajibu na Hadhi ya kazi na kufanya kazi kwa Watanzania wote, vijijini na mijini
Kuelimisha Wananchi haki zao kama raia, wajibu wao na sehemu yao katika Taifa na Serikali yao kupitia Katiba, Serikali Kuu, Bunge na Mahakama
Kuimarisha Ufanisi na Ustawi wa Jamii katika kupiga vita Ujinga, Umasikini, Njaa na Maradhi
Kuhakikisha kuwa Katiba, Sheria na Kanuni zilizowekwa zinatekelezeka kutokana na nyakati zilizopo, zinafuatwa ipaswavyo na vyombo vyote husika; Serikali, Bunge, Mahakama na Wananchi wenyewe. Aidha kuweka maamuzi na mipango ya Serikali wazi kwa wananchi wote ili kuhakikisha uadilifu na uwajibikaji wa Serikali haufanyiki kwa siri na na kuwapa wananchi wote haki kwa kuwa wao ndio waliotoa dhamana ya kuwepo kwa Serikali na kuruhusu Uongozi uliopo uongoze nchi
Kubuni mbinu za kiuchumi ili kumpunguzia mzigo mwananchi wa kawaida hasa wale wa kipato cha chini na wakulima ili kujenga nguvu kubwa ya taifa kuwa katika Tabaka la kati (middle class)
Kuhakikisha kuwa njia kuu za Uchumi na uzalishaji mali zinaboreshwa na kutumika kwa manufaa ya kila Mtanzania na taifa la Tanzania linanufaika kwanza
Kuhamasisha na kuhakakisha kuwa Uzalishaji mali (kilimo, viwanda, uvuvi, ufugaji, biashara, madini , utalii, biashara, sanaa, michezo, huduma na maofisini) unafanyika kwa dhatgi, kisayansi, kiushindani, kiuwajibikaji, kiufanisi na kwa ubora wa hali ya juu kwa kutumia tija, kuongezeka kwa juhudi na maarifa ya uzalishaji mali huu
Kuhakikisha kuwa huduma za msingi zinaboreshwa na kupewa kipaumbele na kufikishwa kwa wananchi ili kujenga maendeleo ya kweli kwa jamii na Taifa;- Afya, Elimu, Maji safi, Chakula, Uchukuzi na Nishati
Kuhakikisha kuwa vita dhidi ya Rushwa, Ubadhirifu, Udini, Ukabila, Uzembe, Ufisadi, Uhujumu, Uvivu, Uzururaji na Kutowajibika au kutokujituma kwa watendaji wa Serikali na taasisi zake (wakuteuliwa au kuchaguliwa), waajiriwa , wafanyakazi na wakulima ni vita vya Taifa zima na linahitaji ushiriki na kushirikisha Wananchi wote. Wananchi wote bila kujali kabila, rangi, jinsia, umri, elimu au mwelekeo wa kisiasa ni wajibu wao kushiriki katika vita hii

Pamoja na kuwa haya ni kuhusu Mwananchi, lakini ni Uongozi pekee ulio mahiri, adilifu, bunifu, nyenyekevu na chapa kazi unaweza kufanikisha hili.

Nikaendelea kuyasema haya

Kazi tuliyonayo sasa si tofauti na ile ya mwaka 1967, ni ile ile na sana sana ni kulenga Nyenzo kuu za maendeleo yetu kama Taifa na kibinafsi kwa kupitia milango miwili. Ili tujikwamue kutoka hali hii mbaya tuliyonayo kama Taifa, ni wajibu wa kila mmoja wetu kuwajibika na kuwa na nia ya kweli kuyafanya yafuatayo;
  1. Kujenga Uchumi imara na madhubuti. Hili litatusaidia katika vita dhidi ya Umasikini, Ujinga, Maradhi na Njaa
  2. Kuwa na Uongozi mahiri na fanisi. Utawala na uongozi wa nchi unahitaji na unategemea Uongozi mahiri kutekeleza sera na mipango, wenye ufanisi kuhamasisha uzalishaji mali na uwajibikaji na wenye kuwa wanyenyekevu na kuheshimu dhamana walizopewa
Uchumi wetu hauwezi kujengeka kwa kutegemea misaada au wawekezaji kutoka nje kuja na kusukuma gurudumu la uzalishaji mali ili kutuongezea kipato. Aidha uchumi wetu hautajengeka kuwa madhubuti kwa kuanzisha mipango mipya au kufanya makosa yaleyale ya kale yaliyofanyika wakati wa Azimio la Arusha, Mipango ya kufufua uchumi 1985-2000 au mipango ya kuchochea Uwekezaji na kuvutia wageni washike hatamu za Uchumi ya 1992-2010.

Na mwisho nikatoa vipaumbele vya Uongozi bora

Uwezo wa Tanzania kuwa na maendeleo ya kweli utaanza na Uongozi bora.

Uongozi bora ni ule;

· wenye mapenzi ya kweli na dhati na kujivunia Utaifa wake
· wenye kujali na kulinda maslahi ya Taifa lake na watu wake
· wenye uwezo wa kupanda mbegu imara ya Uzalendo kwa kila mwananchi bila kujali itikadi, rangi, kabila, dini, elimu, umri au jinsia
· wenye uwezo wa kuhamasisha na kuchochea juhudi za maendeleo ya jamii, umma na Taifa
· wenye nidhamu, watiifu, kuwajibika, tija, ufanisi, kujituma na ufuatiliaji wa hali ya juu
· wenye usikivu, uungwana na unyenyekevu kukiri makosa, kukubali kukosolewa na kupokea na kufanyia kazi maoni ya wengine
· wenye uwezo wa kufanya kazi, kufikiri, kuwa na upeo na wepesi wa kukabili na kufanya maamuzi magumu
· usiolea uzembe, ubaguzi, unyanyasaji, uhujumu, ubadhirifu, rushwa, kudharau, kudhalilisha, kujuana au kulinda maslahi ya wachache au kikundi Fulani

Wajibu wetu kama Taifa na haki yetu kama wapiga kura kuchagua viongozi kutuongoza unabidi uachane na mfumo duni tulioujenga wa kuangalia sura na chama na tuangalie wagombea wetu wa uongozi kwa vigezo hivyohapo juu ili kuunda tabaka jipya la viongozi ambao ni wachapakazi na watakuwa manahodha wazuri kutuongoza katika safari yetu ya kulijenga Taifa.

Sasa kilichotokea ni kuwa Viongozi wengi walikuwa wakihubiri "Juhudi na Maarifa, Ujamaa na Kujitegemea" lakini wengi wao Juhudi na Maarifa yalikuwa ni kujineemesha matumbo yao na kupiga domo na si kufanya kazi na kuwa mfano wa kuigwa. Ni hao hao ambao badala ya kutumia nyenzo ya kujitegemea na kujiimarisha kuwa huru an kujitegemea, wakaitegemea Serikali kwa kila kitu mpaka karatasi za chooni kwa jina la Uongozi.

Azimio bado ni hai kwa wale wenye imani na ambao wakao tayari kulifanyia kazi.

Niko mstari wa mbele kutamka rasmi kuwa naamini Azimio la Arusha kwa 85% bado ni hai na ni muhimu kufanyiwa kazi kw aTaifa letu!
 
Bibi Ntilie,

Nilishtushwa sana majuzi kusikia kauli ya Mzee wetu Mzee Ruksa akisema kuwa Ujamaa na Azimio vilikuwa ni ndoto, Utopian, kuwa haviwezi kuafanya kazi! Sijui huo Ubepari ambau unakaribia miaka 16 umetuletea maendeleo gani zaidi ya Uhujumu na Ufisadi!
 
Bibi Ntilie,

Nilishtushwa sana majuzi kusikia kauli ya Mzee wetu Mzee Ruksa akisema kuwa Ujamaa na Azimio vilikuwa ni ndoto, Utopian, kuwa haviwezi kuafanya kazi! Sijui huo Ubepari ambau unakaribia miaka 16 umetuletea maendeleo gani zaidi ya Uhujumu na Ufisadi!

Mchungaji Nashukuru kwa shule nzito. You said it all!
 
Ni makosa sana dunia ya leo kuongelea ujinga wa azimio la arusha,limepitwa na wakati na haliteteheki kabisa
 
Rev.Kishoka said:
Ikiwa Azimio lilitambua kuwa jamii ni lazima iwe na Mabepari na Makabaila na zaidi kutambua kuwa kuna kujiwekea akiba na kujipatia kipato kwa kutumia hisa za makampuni, basi ni lazima tukubali Azimio la Arusha lilikuwa na mwamko wa kiuchumi na bora kuliko zile program za kijamaa za China, Cuba, Urusi, Korea Kaskazini na kwingineko.

Rev.Kishoka,

..kutokana na kauli yako hapo juu, kwanini serikali ilitaifisha majumba,mashamba,na viwanda?

..kwamba Ujamaa ulifeli, na Ubepari nao unafeli, inadhihirisha kwamba tatizo liko kwetu sisi WATANZANIA individually and collectively.

NB:

..tuache visingizio, kulikuwa na viongozi wa kutosha waliokuwa na nia ya kutekeleza azimio la arusha.

..kwa mtizamo wangu hata wale waliokuwa na nia nzuri na azimio la arusha hawakuwa na uwezo wa kuongoza, na zaidi kusimamia uchumi na uzalishaji.
 
Fita Lutonja

Tanzania Daima~Sauti ya Watu

NINAIKUMBUKA Februari 5, 1967 kama ni siku ya ukombozi wa wanyonge na changamoto ya kuongeza fikra za maendeleo miongoni mwa Watanzania, kwani siku hiyo kule Arusha, hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alitangaza kukomesha watu waliozoea kunyonya jasho la wanyonge bila huruma.

Hakika siku hiyo ilikuwa ya neema kwa Watanzania, kwani mfumo mpya wa utawala chini ya Azimio la Arusha, uliashiria nyota ya matumaini ya kujikomboa kwa wanyonge na waliokuwa wanadhulumiwa haki zao.

Baada ya Tanganyika kupata uhuru wake mwaka 1961 na kuwa Jamhuri mnamo mwaka 1962, na hatimaye kuungana na Zanzibar mnamo mwaka 1964 na kuunda Tanzania, hatukuwa na maendeleo makubwa.

Lakini Mwalimu kwa kuona baadhi ya viongozi kuwa bado wana fikra za kinyonyaji kama walizokuwa nazo wakoloni, akaamua kuanzisha Azimio la Arusha lililokuwa na misingi ya kulinda haki za wanyonge na kuondoa dhuluma ya tabaka la wanyonyaji.

Mwalimu aliona kipindi hicho umma wa Watanzania ukidhoofishwa kwa kudhulumiwa haki na tabaka la mabeberu na mabwanyenye ambao wengi wao walikuwa ni viongozi serikalini, kitendo hicho cha viongozi kuwanyonya wanyonge kilimkera sana.

Dhuluma haikuwa siri kipindi hicho, viongozi waliwadhulumu Watanzania waziwazi bila hata aibu, huku wakijiona wao ni bora zaidi ya wanyonge, wakiendelea kujikusanyia mirija mirefu ya kunyonya mali na haki za watu wengine. Waliendelea kuwakashifu walipa kodi kwa kuwanyonya jasho lao bila hata kuwahurumia.

Haikumchukua muda Nyerere kubaini kuwa ndani ya serikali yake changa, kuna wanyonyaji; mabepari na mabwanyenye ambao hawakuwahurumia wananchi wanyonge wa kawaida.

Alitambua kumbe ubepari na unyonyaji si rangi ya mtu tu. Ilionekana wazi kuwa hata watu weusi wanaweza kuwa wabaya kama walivyo Wazungu.

Baada ya kuona kuwa wanyonge wanadhulumiwa haki zao, tena hadharani, Nyerere aliamua kulinda haki yao ili isiendelee kudhulumiwa.

Aliunda Azimio la Arusha kama misingi ya kuhakikisha kuwa haki ya mnyonge inalindwa kama inavyolindwa haki ya mwenye nguvu. Aliliwekea Azimio kanuni za kuhakikisha hilo linatendeka.

Ni kweli kuwa Azimio lilisaidia kuleta usawa katika jamii. Kupitia Siasa ya Ujamaa, Azimio la Arusha lilifanikisha wanyonge nao kujiona kuwa wana fursa ya kufaidi matunda ya uhuru. Ujamaa na Azimio liliwataka viongozi kuwa wajamaa kweli, wakiwaona watu wanaowaongoza kama ndugu.

Hii ilisaidia kujenga utawala bora, unaoheshimu misingi ya utu badala ya unyonyaji. Hakukuwa na mtu dhalili na mtu bora. Unyonyaji ulionyeshwa kuwa ni mbaya.

Azimio la Arusha pamoja na misingi yake kwa watumishi wa umma, vilevile lilisisitiza ujamaa kuwa ni imani na njia pekee ya kuondokana na ubaguzi, ubinafsi na dhuluma, na kuwafaidisha wananchi wa aina zote nchini. Azimio, pamoja na Ujamaa viliamsha mori na ari ya kufanya kazi kiasi kwamba nchi ilifanikiwa kujijenga kwa kiasi kikubwa.

Watu walifanya kazi kwa kujitolea na kuanzisha vijiji vya ujamaa hadi viwanda. Tanzania ikageuka kuwa mzalishaji wa bidhaa zilizohitajika sana kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maendeleo.

Azimio lilikuwa na siasa ya kujitegemea pia, ambayo iliboresha utumishi wa umma na uajibikaji wa viongozi na wananchi wa kawaida. Siasa hiyo ilimtaka kila mtu katika nafasi yake, kuhakikisha anazalisha kwa wingi, ili kuepuka kutegemea mtu mwingine.

Hii ilianzia kwa mtu mmoja mmoja mpaka kwa taifa. Taifa nalo lilitakiwa kujitegemea kwa mahitaji yake yote muhimu.

Watu walitakiwa kuwa na fikra kuwa wanaweza kuendesha maisha yao binafsi, au nchi bila hata kutegemea nchi nyingine. Tofauti na sasa, ambapo Azimio limeuawa, nchi imekuwa ni kama ombaomba. Jinsi ambavyo wanavyoongezeka ombaomba wa mitaani, na nchi nayo inazidi kuwa ombaomba na inakuwa kama inashindana na ombaomba wa mitaani.

Sasa hali imebadilika baada ya Azimio la Arusha kuuawa na kuzikwa. Hali imezidi kuwa mbaya na kwa hakika, aliyeliua Azimio la Arusha anastahili kubebeshwa lawama zote na hata ikibidi alaaniwe.

Mtu huyo anapaswa kubeba lawama zote kwa sababu amewasababishia mamilioni ya Watanzania maisha magumu.

Hivi sasa Watanzania wameshaanza kushuhudia unyonyaji na unyanyasaji ndani ya nchi yao wenyewe, licha ya kuwa walipata uhuru miaka zaidi ya 40 iliyopita.

Unyonyaji umerudi kwa kasi kwa njia ya uwekezaji.

Wawekezaji wamegeuka kuwa wanyonyaji ambao wanakamua mali za Watanzania bila huruma.

Watanzania, ambao nchi yao ina rasilimali zisizohesabika, leo wamekuwa wanyonge kama watu wanaoishi jangwani kusiko na kitu chochote.

Hadi hii leo sijaelewa nini ilikuwa misingi ya kuvunja Azimio la Arusha. Na misingi hiyo ilikuwa na masilahi gani kwa umma wa Watanzania?

Inashangaza kuwa wakati Azimio la Arusha lilipoundwa, wananchi walielimishwa maana na faida zake. Lakini walipoamua kulivunja, hawakutokea hadharani kueleza sababu za kufanya hivyo!

Mwalimu alifanya mikutano na kuchapisha vitabu na makala mbalimbali, yote akilenga kuwaelimisha wananchi wa kawaida kuhusiana na mfumo huu mpya wa maisha yao.

Lakini wenzetu hawakuona umuhimu wa kuwaeleza wananchi kwa nini waachane na mfumo wa maisha ambao wamekuwa wakiishi kwa miongo minne iliyopita.

Kimyakimya walikusanyika Zanzibar na kufanya maamuzi makubwa huku Watanzania wenyewe wakiachwa gizani. Kwa nini wananchi hatukuulizwa kabla ya kufikia uamuzi wa kuvunjwa kwa Azimio la Arusha? Au kwa nini mlipoamua kulivunja hamkurudi tena kwetu kutueleza ni kwa nini mmefikia uamuzi huo?

Au mlipoingia madarakani mliona hamupati nafasi ya kutuibia na kutunyonya haki yetu kwa sababu ya kanuni za Azimio la Arusha ziliwabana?

Kwani Azimio la Arusha lilikuwa na kasoro gani? Hivi kutetea haki za wanyonge nacho ni kitu kibaya? Mbona hamkutueleza hizo kasoro?

Azimio la Arusha, lililokataza viongozi kumiliki mali kupindukia limevunjwa na matokeo yake tumekuwa na viongozi mafisadi.

Au sijui ni mafisadi viongozi, maana ni vigumu kujua, kwa sababu wapo viongozi ambao walianza ufisadi kabla ya kupata uongozi na wakatumia mali zao kusaka uongozi, pia wapo viongzoi ambao walitumia nafasi zao kujilimbikizia mali na kuwa mafisadi.

Watu sasa wananyonywa na viongozi wao, dhambi ile ile ambayo Nyerere aliiona na kuiwekea kanuni za kuikataa.

Leo inakumbatiwa na wananchi wamekosa mtetezi kwa sababu viongozi ambao walipaswa kuwa watetezi wao, ndio wanaoongoza kundi linalowanyonya.

Azimio lenu la Zanzibar limeleta nini kwetu sisi Watanzania wa hali ya chini? Mbona limezidi kutuumiza na kutuletea maisha magumu na kutufanya tuwe wanyonge zaidi?

Sasa hivi masuala ya dhuluma, unyonyaji, umwinyi sanjari na ufisadi ndani ya serikali ni vitu vya kawaida.

Walidhani kuwa umaskini uliokuwepo ulikuwa unaletwa na Azimio la Arusha, wakaliua ili kutokomeza umasikini.

Lakini hali ya mambo imethibitisha kuwa hilo si kweli kwa sababu umaskini badala ya kutoweka, unaongezeka.

Na inavyoonekana ni vigumu sana kukuza uchumi wa nchi kwa mfumo walioukubali. Sana sana wanachofanya ni kujenga uchumi wa watu binafsi.

Tunatawaliwa kwa mfumo mpya wa ukoloni mamboleo. Tofauti yake na ukoloni tulioung’oa mwaka 1961 ni ndogo sana lakini madhara yake ni makubwa kuliko ya ule tulioukataa zamani.

Uhuru wetu sasa umegeuka kuwa wa bendera, jambo ambalo Azimio la Arusha lilikuwa linapiga vita kupitia kanuni zake.

Mwalimu katika mkutano wake wa kuelezea ubora wa Azimio la Arusha aliwaambia Watanzania ya kwamba jambo muhimu ni kujitegemea.

Aliwaambia Watanzania kuwa hawapaswi kumtegemea mtu mwingine yeyote. Tumeliua Azimio la Arusha na tumeingia katika mtego wa kuwategemea wafadhili na wahisani!

Azimio lenu la Zanzibar, ambalo kimsingi linatetea viongozi, limetuletea aibu ndani ya nchi yetu kwa viongozi wa umma kujimilikisha mali ya umma kwa kisingizio kuwa ni ujasiriamali.

Azimio lenu la Zanzibar tunalilaani kwa sababu limetuletea EPA, Richmond, unyonyaji, ubeberu, dhuluma, ufisadi, na matatizo chungu nzima ambayo yote haya tungekuwa na Azimio la Arusha yasingetokea kwani misingi yake ilikuwa hairuhusu.

Viongozi wanapaswa kutambua kuwa wananchi wamechoka kweli na EPA, Richmond , unyonyaji, ubeberu, ubepari, ukupe, ukiritimba, umwinyi na wanachotaka ni Azimio la Arusha la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na misingi yake ya utawala bora, ili liunguze tena viongozi vikaragosi waliozoea dhuluma.
 
Mzee Rhuksa anadunda tu. Hukumsikia karibuni akisema kuwa ujamaa ulikuwa ndoto?
 
Bubu,

Wengi wanaolipinga Azimio ambao si viongozi ni watu ambao hawakulisoma vizuri wala kutafakari na kulielewa ndio maana hata humu ndani JF, kuna watu wataendelea kulilaani milele.

Kilichokuwa kibaya kwa Azimio la Arusha ni utekelezaji hasa ule wa kutaifisha mali na matunda ya viongozi kunywa mvinyo wa Azimio na kulazimisha Umasikini ukubalike!

Sidhani kama hilo lilikuwa lengo la Mwalimu, lakini nafikiri alikuwa na mengi yanayomkabili na hivyo akashindwa kuhakikisha kuwa tunajijenga vyema kiuchumi.

Focus kubwa ya Mwalimu siku zote tunajua ilikuwa ni empowerment kutumia Utaifa na fikra, kumbadilisha Mwafrika na Mtanzania mawazo duni ya unyonge yaliyotokana na ukoloni. Huku alifanikiwa ila waliomwangusha ni wasaidizi wake ndani ya Chama na Serikali.

Nchi nyingine, zinapopata Uhuru, hukimbilia kujijenga Kiuchumi na si kujenga Utaifa na uhuru wa Mawazo au kujijenga kujitegemea.

Serikali yetu na Chama tawala (hata vya upinzani) ni sawa na wakoloni. Wanatawala, wanamiliki na wananyanyasa Raia na wafuasi kutumia madaraka ya Uongozi na hivyo kuzima uhuru wa fikra na mawazo ambao ndio ngao kuu ya kujitegemea na kuwa na maendeleo ya kweli!
 
Mzee Rhuksa anadunda tu. Hukumsikia karibuni akisema kuwa ujamaa ulikuwa ndoto?

Anafaa kuwekwa kiti moto na kuulizwa kama ujamaa ulikuwa ni ndoto je, Watanzania wamefaidika vipi baada ya kuvunjwa Azimio la Arusha na kuukumbatia ubepari?
 
Wakuu,
Twende mbele tukitazama nyuma... Nyerere ndiye aliyetuachia urithi huu wote kwa sababu ndiye aliyemchagua Mwinyi na Azimio la Zanzibar lilipitishwa wakati Nyerere mzimaaaaaa!.....Kwa nini alikaa kimyaaaa?
Je, kuna kitu kiliendelea hapo katikati ambacho sisi wananchi hatukielewi!..
 
Bob Mkandara,

Tanzania tunasifika kwa "unyeti" na usiri wa kijinga. Mambo mengine sijui walikuwa wakipikuana hawa Wazee na hivyo kutishiana au nini?

Nakumbuka kabla ya Mwalimu kuachia Uenyekiti, kulikuwa na vijikelele vya chini chini nani mwenye mamlaka na mkubwa wa nchi, Mwenyekiti wa Chama au Rais wa Nchi?

Si ajabu Mwinyi alipovipata vyote washauri wakamwambia kuwa sasa ana nguvu zote na Nyerere asimtishe!

No wonder wakati ule wa kisa cha Tanganyika na OIC Nyerere akawashupalia Makamu Mwenyekiti na Waziri Mkuu Malecela na Katibu Mkuu Kolimba huku akimuacha Rais na Mwenyekiti wa Chama akipeta!
 
Wakuu,
Twende mbele tukitazama nyuma... Nyerere ndiye aliyetuachia urithi huu wote kwa sababu ndiye aliyemchagua Mwinyi na Azimio la Zanzibar lilipitishwa wakati Nyerere mzimaaaaaa!.....Kwa nini alikaa kimyaaaa?
Je, kuna kitu kiliendelea hapo katikati ambacho sisi wananchi hatukielewi!..

Hapana Mkandara, Nyerere hakunyamaza kimya juu ya kuvunjwa kwa azimio la Arusha na kuundwa kwa azimio la Zanzibar. Tatizo lilikuwa alikuwa ametoka kutawala na alitawala muda mrefu watu walikuwa wamechoka, si unajua hata chakula kikiwa kile kitamu kabisa ukila kwa mfululizo kwa muda mrefu unakinai!. Ndivyo ilivyokuw kwa wa Tz walikuwa wamemkinai, na hata aliposema mambo ya maana waliona anamwingilia mwenziwe. Lakini tulipokuja kuona matokeo yake ndio tukaanza kalalamika, unakumbuka hotuba aliyoitoa Nyerere kwenye kilele cha sikukuu ya wafanyakazi Mbeya?. Uwanja ulijaa haujawahi kujaa namna hiyo kwa habari za siasa tena, na hutuba ilikuwa ni azimio la Zanzibar. Jamaa walishaamua ikawa ndio imetoka, na alipokufa tena ikawa ooh! hakuna msalie tena hapo.
 
Nyerere bwana, alijilundikia madaraka yote: Chama kilishika hatamu na yeye akiwa mwenyekiti. Wazo lake ilikuwa halina na nafasi ya upinzani tena: Zidumu fikra za Mwenyeketi.
Huyo ni Nyerere tumwachache na mambo yake aendelee kuula huko pepopi, tuwakabe koo waliopo, ama na tujichanganye ili tujiletee maendeleo kwani tuna sababu zote za kufanya katiba aiandikwe upya ili kutawanya madaraka na kuleta uwajibikaji.

Azimio la Arusha limeshindwa na si vema kurudi huko labda tusibiri tutapofika kwenye stage ya juu ya maendeleo yetu hapo baadaye. Azimio la Arusha si dawa pekee.
Nani alitegemea Wachina wanaweza kuukubali na kuendesha UBEPARI kama walivyofanikiwa H/Kong na Macau. Tunaweza improve tulichonacho ili kufikia maisha bora kwa raia wetu.
 
Nyerere bwana, alijilundikia madaraka yote: Chama kilishika hatamu na yeye akiwa mwenyekiti. Wazo lake ilikuwa halina na nafasi ya upinzani tena: Zidumu fikra za Mwenyeketi.
Huyo ni Nyerere tumwachache na mambo yake aendelee kuula huko pepopi, tuwakabe koo waliopo, ama na tujichanganye ili tujiletee maendeleo kwani tuna sababu zote za kufanya katiba aiandikwe upya ili kutawanya madaraka na kuleta uwajibikaji.

Azimio la Arusha limeshindwa na si vema kurudi huko labda tusibiri tutapofika kwenye stage ya juu ya maendeleo yetu hapo baadaye. Azimio la Arusha si dawa pekee.
Nani alitegemea Wachina wanaweza kuukubali na kuendesha UBEPARI kama walivyofanikiwa H/Kong na Macau. Tunaweza improve tulichonacho ili kufikia maisha bora kwa raia wetu.


Tuko pamoja Tom.
Mwakyembe alitoa tahadhari akisema "tusije tukafika mahala tukaanza kumyooshea raisi kidole" (not his exact words). Jamaa aliniudhi sana. Mwiba akamwita mnafiki, watu hapa JF wakamparamia kwa nguvu zao zote.

Taratibu watanzania upofu umeanza kututoka, na tumeanza kuwa-face wanaotusaliti.

...Zidumu fikra za Mwenyeketi. Hahahahah! I think Mwakyembe has no problem with this statement.


.
 
Anafaa kuwekwa kiti moto na kuulizwa kama ujamaa ulikuwa ni ndoto je, Watanzania wamefaidika vipi baada ya kuvunjwa Azimio la Arusha na kuukumbatia ubepari?

Kama kuna mtu anadhani ujamaa ungetufaa basi huyo anachemsha, ujamaa was very utopian thing hakuna mahali ulipo-prove success. Hata China kwenyewe wanakoendelea kujiita wajamaa ni mabepari na makabaila of chinese type(we can debate) Lakini naungana na kusema kuwa azimio la Arusha lilikuwa na vipengele vinavyofaa sana, hasa vinavyohusu miiko ya uongozi. Waliovunja azimio la Arusha , yaani walioleta azimio la Zanzibar ni viongozi wale waliokuwa na uchu wa utajiri aka mafisadi, na lengo lao tumeliona.
Lakini idea ya kusema watu waombe kibali kununua TV, gari na kununua sukari kwa kupanga mstari na kuwa na maduka ya kaya sio kitu ambacho waliexperience wanapenda kirudi.
 
Nyerere bwana, alijilundikia madaraka yote: Chama kilishika hatamu na yeye akiwa mwenyekiti. Wazo lake ilikuwa halina na nafasi ya upinzani tena: Zidumu fikra za Mwenyeketi.
Huyo ni Nyerere tumwachache na mambo yake aendelee kuula huko pepopi, tuwakabe koo waliopo, ama na tujichanganye ili tujiletee maendeleo kwani tuna sababu zote za kufanya katiba aiandikwe upya ili kutawanya madaraka na kuleta uwajibikaji.

Azimio la Arusha limeshindwa na si vema kurudi huko labda tusibiri tutapofika kwenye stage ya juu ya maendeleo yetu hapo baadaye. Azimio la Arusha si dawa pekee.
Nani alitegemea Wachina wanaweza kuukubali na kuendesha UBEPARI kama walivyofanikiwa H/Kong na Macau. Tunaweza improve tulichonacho ili kufikia maisha bora kwa raia wetu.

How,kwa uongozi gani tulionao? Kumbuka slogan ya sasa ni maisha bora kwa kila mwananchi!
Unaweza kusema kweli kabisa kuwa kuna dalili ya maendeleo kwa mwananchi huko mbele kwa system hii ya kusamehe wezi kama wa EPA?

Azimio la Arusha halikushindwa per se,maadili yalikuwepo wakati ule.Viongozi walikuwa viongozi kweli.Walikuwa hata wana club zao za kukutana,mfano pale Leaders club.Sasa hawa wa sikuhizi tunawasoma kwenye blogs kila siku.Wananchi pamoja na kuboresha maisha yao,pia wanataka kuwa na kiongozi ambaye kweli anawapa mwongozo,sio kusoma kwenye magazeti wizi wa viongozi kila siku
 
Tumeacha ujamaa pamoja na maadili yake yote ya uongozi. Tumeingia kwenye ubepari kichwa kichwa bila kuwa na ethics zozote, Tunasahau kwamba hata nchi za kibepari hawana masihara kwenye suala la maadili ya uongozi.
 
Back
Top Bottom