Azimio la Arusha: Kuzaliwa upya?

Azimio la Arusha: Kuzaliwa upya?

Azimio la Arusha ndio muarobaini wa matatizo yote ya Tanzania pengine kuliko hata wakati wa nyuma, maana at least huko nyuma kulikuwa na vita baridi hivyo tulikuwa na sehemu ya kukimbilia ila kwa sasa hakuna kwa kukimbilia kabisa wote wamekuwa ni rafiki zetu kwa kuwa wanahitaji resources zetu na wote wamekuwa ni adui zetu kwa kuwa wanatuibia resources zetu na kutuacha maskini.

Katika mazingira kama haya ya sasa tunahitaji kuwa na sera zetu binafsi za kiuchumi ili tuweze kuendelea kuliko kuendelea kutumia sera za kiuchumi za nje, ambazo haziendani na mazingira yetu na matokeo yake tunazidi kuwa maskini zaidi badala ya kuendelea. Azimio la Arusha ukilisoma ukalielewa, utaona kwamba ndio dawa pekee ya matatizo yetu ya kiuchumi leo hii, kwa kuwa ndio lilikuwa dira yetu, sasa tumeacha kufuata dira tumepotea nyikani.

Leo hii tunafikiria kutunga sheria kutofautisha biashara na uongozi ya nini? wakati mambo yote hayo yamo ndani ya azimio la arusha?. Tukirejea kwenye azimio la arusha tutaendelea tu, azimio la arusha halizuii mtu kumiliki mali binafsi , bali linataka mtu amiliki mali kwa jasho lake halali, halizuii mtu kuwania uongozi bali linataka kiongozi awe ni mtu wa namna gani sio bora kiongozi bali kiongozi bora.Watu wengi tz wanalisikia tu na kulipinga azimio la arusha bila kulisoma, mimi nimelisoma na kulielewa sijaona ubaya wowote zaidi ya uzuri, watu walisome kwanza ndio walipinge.

Suala la azimio la arusha ni kama katiba kwa sasa, kuna watu wanapiga kelele tu kumbe hata katiba yenyewe hajawahi kuisoma achilia mbali kuiona, hivyo ukimwambia atoe mchango wake katika marekebish ya katiba hana mchango wowote.Hivyo kwa TZ Azimio la Arusha ndio mkombozi wetu wa kweli kama tunataka kuendelea.
 
mzeei nakubaliana na wewe kwamba azimio la arusha ni muhimu sana kwa tanzania hii mpya tunayotaka kuijenga kwasasa, lakini hapo hapo nikiweka angalizo kuwa tuchukue yale mazuri tu kutoka katika hilo azimio na vile vile lazima kuwe na political will kutoka kwa viongozi wetu wa serikali na hii chama kilichopo madarakani juu ya swala zima la kuirudia azimio la arusha
 
Je ni kwa jinsi ganin tutaweza kukabiliana na changamoto kutoka nje ambazo ziko nje ya uwezo wetu? Ni jinsi gani tunaweza kutumia rasilimari zetu kwa maendeleo yetu pasipo kuwategemea wahisani?
 
APRILI 30, mwaka huu, Ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kulifanyika kongamano la miaka 44 ya Azimio la Arusha.

Ni kongamano lililoandaliwa na Sauti ya Vijana Tanzania-Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (SAVITA – UDSM), kwa kushirikiana na Klabu ya Falsafa chuoni hapo.

Kongamano lilihudhuriwa na wengi, baadhi wakiwa mashuhuda wa kuzaliwa kwa Azimio hilo. Mashuhuda hao ni pamoja na Ibrahim Kaduma, Waziri wa zamani katika Serikali ya Mwalimu Nyerere pamoja na Mzee Hashim Mbita.
Profesa Issa Shivji, ambaye naweza kumtambua kama wakili wa Azimio la Arusha lililohujumiwa bila hatia, aliongoza tafakuri ndani ya kongamano hilo.

Kauli mbiu ilihusu; “Tafakuri ya kina juu ya Azimio la Arusha. Je, lina nafasi katika mjadala wa Katiba mpya?”
Kwa kauli mbiu hii, ni dhahiri Azimio lilipuuzwa na hatimaye kuhujumiwa bila hatia, misingi yake sasa inahitajika nchini.

Ni misingi ya utu inayokataa suluhu na viongozi wanaojilimbikizia mali kwa kutambua kuwa utu haulindwi kwa mitutu bali uongozi bora wenye miiko.

Hadi mwisho wa kongamano, ilidhihirika Azimio halikuwa na hatia yoyote mbele ya wanyonge isipokuwa liliwakera baadhi ya viongozi tu.

Madhara yamezidi kujianika. Kwa sasa, si tu viongozi wamejilimbikizia mali; bali wanaitumia mali hiyo kuharibu mifumo nyeti nchini, ikiwamo ya kupata uongozi bora. Wamegeuza, kwa mfano, mchakato wa uchaguzi kuwa gulio la kuuza na kununua kura.

Hujuma dhidi ya Azimio zimeibua viongozi mafisadi. Hakika, Azimio halikuwa na hatia. Ni dhahiri waliolipuuza na kuhujumu ndiyo wenye hatia.

Halikuwa na hatia kwa sababu lililinda maslahi ya wanyonge na kutoa si tu mwongozo, bali pia mwelekeo kuhusu mustakabali wa uongozi bora nchini.

Wananchi mashambani, sokoni, safarini, majumbani na hata ofisini walikuwa na uhakika kuhusu kiongozi gani anastahili kuwajibishwa, kwa sababu gani na kwa wakati gani.

Walikuwa na fursa ya kufahamu hivyo kwa sababu Azimio lisilokuwa na hatia kwao, liliwapa fursa ya utambuzi huo kutokana na kusimika miiko ya uongozi kitaifa, kimkoa, wilaya, kata hadi kijiji au mtaa.

Uongozi ulitengwa na kuwekewa mkondo usiopenyeza wanunuzi au walanguzi wa kura kama ilivyo sasa ndani na nje ya vyama vya siasa.

Naunga mkono mawazo yaliyoibuka kwenye kongamano kwamba; ni wakati muafaka misingi ya Azimio la Arusha isimikwe kwenye Katiba mpya na hasa miiko ya uongozi.

Naunga mkono kwa sababu, hatupaswi kuacha suala la miiko ya uongozi liamuliwe kwa kuzingatia utashi wa vyama vya siasa au sheria za hapa na pale zinazotungwa kwa kuzingatia hisia za serikali au Bunge.

Hatupaswi kuliacha suala la miiko katika hali hiyo. Hatupaswi kutelekeza suala hili nyeti kwa Taifa. Lazima tuwe na masharti ya uongozi na yabainishwe sasa katika Katiba mpya.

Kuna tofauti kubwa ya kiuongozi kati ya enzi zile za utekelezaji wa Azimio la Arusha na miiko ya uongozi na enzi hizi za uongozi bila miiko. Kwa sasa, tunashuhudia kiwango cha juu cha kuvumilia uhuni, ufisadi na uchafu mwingine katika uongozi wa kitaifa.

Tunashuhudia suala la uhuni wa kiuongozi likiachwa kushughulikiwa kwa mujibu wa utashi wa kiongozi mkuu badala ya mfumo ambao ungekuwa bora na imara zaidi kama ungeimarishwa katika misingi ya Azimio la Arusha; yaani miiko ya uongozi.

Bado tunahitaji zaidi misingi ya Azimio la Arusha ambalo pengine si sahihi sana kudai limeuawa. Si busara kusema limeuawa kwa sababu Azimio la Arusha limejikita zaidi katika fikra (hasa fikra sahihi).

Na ukweli ni kwamba, ni vigumu na pengine haiwezekani kuua fikra sahihi ndani ya Azimio la Arusha. Tunaweza kuua mtu mwenye fikra sahihi, lakini hatuwezi kuua usahihi wa fikra zake.

Kwa mantiki hiyo ya uwezekano wa kuua mtu mwenye fikra sahihi lakini kamwe kutoweza kuua usahihi wa fikra zake, nahimiza wazalendo wote ndani na nje ya nchi, kuamini kuwa Azimio la Arusha na hasa misingi yake, ni suala la kifikra zaidi, tena fikra sahihi.

Kama ilivyoelezwa katika kongamano, misingi ya Azimio la Arusha ilikuwa ni utu uliowekewa mipaka ya nidhamu kiuongozi. Hizi ni fikra sahihi. Ni fikra hai kuliko msimu wa uhai wa binadamu.

Azimio lilibainisha nani awe kiongozi na nani asiwe kiongozi. Kazi ya kumtafuta kiongozi haikutupwa au kutelekezwa mikononi mwa wapiga kura wenye kuhangaikia tonge la siku kiasi cha kukosa muda wa kupima kwa busara nani kiongozi bora.

Kazi ya kumtafuta kiongozi bora, na hivyo kujenga uongozi bora nchini ilirahisishwa ndani ya Azimio la Arusha kupitia miiko ya uongozi.

Mgombea alijipima ubavu kama atamudu kuongoza bila kujilimbikizia mali, kama atazingatia misingi ya utu na hasa kwa vitendo kwamba; binadamu wote ni sawa.

Mgombea hakupewa fursa ya kujipima kwa kutazama kigezo cha fedha au ukubwa wa biashara zake. Alilazimishwa kujipima kwa kigezo cha miiko ya uongozi kwa mujibu wa Azimio la Arusha lisilo na hatia kwa wanyonge.

Ndani ya Azimio la Arusha, kutokujilimbikizia mali halikuwa suala la kwenda kuamuliwa mahakamani ambako si ajabu hata baadhi ya majaji au mahakimu wakawa ni sehemu ya wenye hatia.

Kwangu, kongamano hili lilinipa nafasi ya kuwatambua waliohujumu Azimio la Arusha bila hatia kuwa ni sawa na walioshiriki mauaji ya wanafunzi ya Soweto, Afrika Kusini.

Wanafunzi wale walijitokeza kuandamana Juni 16, 1976 wakipigania utu na haki kama ambavyo Azimio la Arusha lilivyokuwa likijinadi. Walipigania msingi wa utu kwa kupinga ubaguzi. Lakini bila hatia, maisha yao yalizimwa. Wakauawa.

Waliandamana kudai haki na misingi ya utu, uongozi bora usio wa kibaguzi. Kwa wakati huo, Azimio la Arusha lilikuwa likiishi bila kuhujumiwa. Tanzania iliyokuwa ikiisaidia Afrika Kusini, kwa hali na mali, kupinga ubaguzi wa rangi pia ilikuwa ikiishi katika falsafa ya Azimio la Arusha lililotambua binadamu wote ni sawa.

Ilikuwa katika mitaa ya Soweto, wanafunzi takriban 20,000 wa shule mbalimbali walijitokeza kwa ujasiri mkubwa kutetea haki na utu. Hawakujua mwisho wa uamuzi wao huo, baadhi yao 176 waliuawa.

Hata hivyo, waliouawa na ambao hawakuuawa, kwa pamoja hawakujua kitakachowapata, lakini walijua wanapigania haki.

Kwa hali ilivyo na hasa katika kupigania urejeshwaji wa miiko ya uongozi, ni lazima tuwe na upande. Tuchague upande. Wanaounga mkono wajitokeze, wanaopinga pia tuwajue. Wasiokuwa na upande tutawaweka kundi moja na wanaopinga urejeshwaji wa miiko ya uongozi.

Nimalizie kwa kunukuu mtazamo wa mmoja wa raia wa Marekani waliopata kuwa watetezi wa Ujamaa, Max Eastman aliyepata kusema:

“People who demand neutrality in any situation are usually not neutral but in favor of the status quo.”
Max, aliyezaliwa Januari 4, 1883 na kufariki Machi 25, 1969 anajenga mantiki kwamba; wanaojidai hawana upande katika masuala ya msingi, si kweli kwamba hawana upande, isipokuwa wananufaika na hali ilivyo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika
hs3.gif
 
“Kwa kuwa serikali ya nchi inawajibika kwa wananchi, basi, endapo serikali hii itahujumu maslahi ya pamoja, itakuwa ni haki ya wananchi kuyapinga maamuzi ya serikali au kuivunja serikali hiyo na kusimika serikali mpya, serikali ambayo itawajibika kuzingatia masharti yote, kama ambavyo yatawekwa na wananchi kwa ajili ya kukuza na kuhami maslahi yao ya pamoja.”

Mbona naona kama alikuwa amewatega viongozi woooote watakaofuatia baada yake?
Hivi tukijifanya kwamba Azimio la Arusha Bado lipo, na ndio linalotuongoza, hali itakuwaje Jamani?
Nadhani DR SLAA naye alirefer hapa (Kumbuka mahojiano yake na MM)
 
Hivi tukijifanya kwamba Azimio la Arusha Bado lipo, na ndio linalotuongoza, hali itakuwaje Jamani?
Risasi za moto zimejaa tele vituo vya Polisi, na Askari wetu wamepewa Haki ya Kuua Raia wakati wowote...
Cha Muhimu tuanze kutoa elimu ya Uraia kwa Askari wetu, kila mwana-JF ambaye ana ndugu au Jirani ambaye ni Askari ampe Darasa juu ya Umuhimu wa Raia kudai haki zao kwa njia ya maandamano. Kisha tuwaeleze juu ya Umuhimu wa wao kulinda Raia badala ya kuwafyatulia risasi kwa kufuata maagizo ya wakubwa,, Kisha tuendelee........
 
"Kwa kuwa serikali ya nchi inawajibika kwa wananchi, basi, endapo serikali hii itahujumu maslahi ya pamoja, itakuwa ni haki ya wananchi kuyapinga maamuzi ya serikali au kuivunja serikali hiyo na kusimika serikali mpya, serikali ambayo itawajibika kuzingatia masharti yote, kama ambavyo yatawekwa na wananchi kwa ajili ya kukuza na kuhami maslahi yao ya pamoja."

Mbona naona kama alikuwa amewatega viongozi woooote watakaofuatia baada yake?
Hivi tukijifanya kwamba Azimio la Arusha Bado lipo, na ndio linalotuongoza, hali itakuwaje Jamani?
Nadhani DR SLAA naye alirefer hapa (Kumbuka mahojiano yake na MM)

Yule Mzee alikuwa na vision ya mbali sana. Hotuba zake nyingi ukizisikiliza bado ziko relevant hata leo hii miaka 26 tangu angàtuke madarakani. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi...AMEN
 
Kwa Tunisia askari si walikuwa na silaha za kutosha. Nguvu ya umma ikiamua hakuna mtu au taasisi inayoweza kuzuia mapinduzi. kuizuia
Risasi za moto zimejaa tele vituo vya Polisi, na Askari wetu wamepewa Haki ya Kuua Raia wakati wowote...
Cha Muhimu tuanze kutoa elimu ya Uraia kwa Askari wetu, kila mwana-JF ambaye ana ndugu au Jirani ambaye ni Askari ampe Darasa juu ya Umuhimu wa Raia kudai haki zao kwa njia ya maandamano. Kisha tuwaeleze juu ya Umuhimu wa wao kulinda Raia badala ya kuwafyatulia risasi kwa kufuata maagizo ya wakubwa,, Kisha tuendelee........
 
Kwa Tunisia askari si walikuwa na silaha za kutosha. Nguvu ya umma ikiamua hakuna mtu au taasisi inayoweza kuzuia mapinduzi. kuizuia

Umma upi?
Hawa wabongo ninao wajua mimi ?
Mh sidhani kama wanauwezo huo zaidi ya kuongea kwa kificho kificho ( kiunafiki nafiki)
 
ni bora ukaongoza nchi kidectator lakini mambo na uchumi unasonga,kuliko kuongoza nchi kwa urafikihuku mambo na uchumi ukidumaa kipi bora sasa

hata Idd Amin wakati wa uongozi wake uchumi ulikuwa ukisonga,tatizo ni kwamba alikuwa tofauti na wamarikani na waingereza ivi fikilia mpaka Idd amin aliamuwa kuichangia serikali ya uingereza pesa na chakula inja maana jamaa alikuwa mbali, Pia mzee Nyerere aliwapa chakula wachina enzi hizo

lakini sasa hatuwezi hata kujilisha wenyewe,
nyerere daima bana
 
"Kwa kuwa serikali ya nchi inawajibika kwa wananchi, basi, endapo serikali hii itahujumu maslahi ya pamoja, itakuwa ni haki ya wananchi kuyapinga maamuzi ya serikali au kuivunja serikali hiyo na kusimika serikali mpya, serikali ambayo itawajibika kuzingatia masharti yote, kama ambavyo yatawekwa na wananchi kwa ajili ya kukuza na kuhami maslahi yao ya pamoja."

Mbona naona kama alikuwa amewatega viongozi woooote watakaofuatia baada yake?
Hivi tukijifanya kwamba Azimio la Arusha Bado lipo, na ndio linalotuongoza, hali itakuwaje Jamani?
Nadhani DR SLAA naye alirefer hapa (Kumbuka mahojiano yake na MM)
Huwa sihitaji hata kulisikia hili jina la huyo jamaa. Umasikini huu tulionao yeye ni anasehemu kubwa ya mchango wake.
 
Huwa sihitaji hata kulisikia hili jina la huyo jamaa. Umasikini huu tulionao yeye ni anasehemu kubwa ya mchango wake.

Ndugu yangu,

Hili somo la uongozi wa mwalimu na hatma ya Tanzania ni refu, kubwa, pana na muhimu,
Ila unakosea kumlaani baba yako kwa kipara chako ilhali unaweza kuvaa kofia.

Licha ya mapungufu mengi ya mwalimu tukumbuke mema yake basi.

Halafu ulinganishe na waliomfuatia (sio kwenye uraisi tuu, na nafasi nyingine pia).

"Mwalimu alikuwa na ataendelea kuwa jiwe walilolikataa waashi kumbe ndio jiwe kuu"
 
“Kwa kuwa serikali ya nchi inawajibika kwa wananchi, basi, endapo serikali hii itahujumu maslahi ya pamoja, itakuwa ni haki ya wananchi kuyapinga maamuzi ya serikali au kuivunja serikali hiyo na kusimika serikali mpya, serikali ambayo itawajibika kuzingatia masharti yote, kama ambavyo yatawekwa na wananchi kwa ajili ya kukuza na kuhami maslahi yao ya pamoja.”

Mbona naona kama alikuwa amewatega viongozi woooote watakaofuatia baada yake?
Hivi tukijifanya kwamba Azimio la Arusha Bado lipo, na ndio linalotuongoza, hali itakuwaje Jamani?
Nadhani DR SLAA naye alirefer hapa (Kumbuka mahojiano yake na MM)

Kwanini useme aliwatega wenzake. Je un kilichoandikwa hapo kinakukwaza wapi au kipi si sahihi ktk hilo tamko?

Nikufahamishe tu kuwa Nyerere akuwa achtect pekee ktk kutengeneza Azimio la Arusha.
 
Kwanini useme aliwatega wenzake. Je un kilichoandikwa hapo kinakukwaza wapi au kipi si sahihi ktk hilo tamko?

Nikufahamishe tu kuwa Nyerere akuwa achtect pekee ktk kutengeneza Azimio la Arusha.

But he had the guts to allow it to be printed, can the current regime hint its people that
they have authority and power over it???
 
Lakini alishaacha madaraka na akatoweka duniani mbona bado hamuendelei kama yeye alikuwa ni kikwazo?

Well said Masuke!
Nimeipenda hiyo...wanakazania mabaya yake mazuri hawayaoni....haya basi azimio lake la arusha mmelichoma moto-fine.
Viwanda na Mashirika yake mmeuza-fine.
Muungano wake nao vunjeni-fine.
Madini aliyoyalinda mnagawa tu bure.
Uongozi sasa ni fedha kwenda mbele.
Wataalam wanaacha taaluma zao wanakimbilia siasa.

HAYO MAENDELEO ALIYOWAZUIA MSIYAPATE NDIO HAYA MLIYONAYO SASA HIVI????
.
 
jamani kwa enzi za nyerere ni sawa kabisa, ni mwenye heri wa kweli. namlaumu kukataa mabadiliko baada ya dunia kubadilika na namlaumu kwa ajli ya mletaji wa mabadiliko hayo Sokoine, na namlaumu kwa maagizo yake Lowassa asipate cheo kikubwa na ni shahidi wa Sokoine
 
Ndio akitajwa tu nyerere mie huwa namlaani. Laana za mungu ziwe juu yake huko akhera alipo mungu amuingeze ktk moto mkali kabisa sijui ni jahannam au haamiya mie cjui lkn mungu nakuomba huyu nyerere mtie ktk moto mkali kabisa ni adui wa waislam na wazenj
Uadui na wazanzibari pamoja na waislam aliuanza lini huyu Mwalimu Nyerere?

Hivi inawezekana kukaa meza moja ya majadiliano na adui yako na mkajadiliana bila kulazimishwa?

Mimi nadhan ungekuwa sahihi zaidi kama ungejipambanua na kusema ama wewe pamoja na hao unaotaka kuwasemea ndio maadui wa Mwalimu Nyerere na yeye hakuwa na uadui na nyie wala hakujua kama kuna uadui.

Labda mkuu ungetueleza kitu gani kibaya kiasi hicho hasa ambacho Mwalimu Nyerere alikifanya hadi ufike kuandika maneno mabaya hivyo juu yake.
 
Umma upi?
Hawa wabongo ninao wajua mimi ?
Mh sidhani kama wanauwezo huo zaidi ya kuongea kwa kificho kificho ( kiunafiki nafiki)

Mimi naona mtu anapokuwa masikini zaidi ndiyo anavyokuwa mwoga zaidi wa kupigania haki yake hata zile za msingi! CCM imewafanya watanzania kuwa masikini zaidi ili wawe waoga zaidi wa kutetea haki zao na wao waendelee kutukandamiza wapendavyo!

Sisi masikini hatuna cha kupoteza zaidi sana tutapoteza unyonge wetu
tukiamua kudai haki hata kwa kumwaga damu, ni jambo la KUAMUA kama mbwai na iwe mbwai kwani nini!
 
"Kwa kuwa serikali ya nchi inawajibika kwa wananchi, basi, endapo serikali hii itahujumu maslahi ya pamoja, itakuwa ni haki ya wananchi kuyapinga maamuzi ya serikali au kuivunja serikali hiyo na kusimika serikali mpya, serikali ambayo itawajibika kuzingatia masharti yote, kama ambavyo yatawekwa na wananchi kwa ajili ya kukuza na kuhami maslahi yao ya pamoja."

Waliogopa hayo maneno wakaamua kuunda azimio la Zanzibar ambalo halina mikwaruzo.
 
Back
Top Bottom