Mkuu Maganjwa, sera inayofuatwa kwa sasa ni sera ya Uchuuzi mdogo mdogo. wananchi wanaambiwa waunde vikundi ili wapewe mitaji ya kuuza karanga, bamia, kucheza ngoma nk. Viongozi nao wanashindana kuingia mikataba mingi itakayo wapatia vijicent vya kuweka Uswis...
Ni vigumu sana kuirjesha Azimio la Arusha kwa wakati huu; Sera zenye kukinzana tayari tumesha letewa na bunge letu kubariki! Njia kuu za uchumi kumilikiwa na Umma ilifutwa, njia kuu za uchumi zinamilikiwa na akina BWM et al...Tanzania imesha ridhia mikataba feki ya kibiasha za kimataifa, itakuwa vigumu sana kufuta mikataba kama ya dhahabu, uranium, gesi, almasi et al...
Kama nchi tutakachoweza kufanya ni kuweka uwazi katika mikataba na utekelezaji wa bajeti mwanzo mwisho... zaidi ya yote ni kuweka kwenye katiba kuwa adhabu ya Ufisadi ni Kifo na kitekelezwe kwa mtu yeyote hata Rais wa nchi kama walivyofanya Wachina...mwisho na kwa umuhimu: kunahaja ya kureview vipaumbele vyetu ili viwalenge walengwa ambao ni wananchi badala ya kuendelea kuwavutia wanyonyaji...
...Nina matumaini makubwa kuwa hii mikataba ya Wachina inayoingiwa sasa hivi itatusaidia sana kuwabana mataifa ya kimagharibi ambayo huwa wana homola Rasilimali zetu in the name of Jesus na kuwaacha wananchi hoi in the name of shetani...