Azam TV news: Dira ya dunia BBC wakae sawa

Azam TV news: Dira ya dunia BBC wakae sawa

itawachukua muda mrefu sana kuwapiku itv katika habari.......yaaani taarifa ya habari itv inaangaliwa na 98 % ya wenye tv kwa ving'amuzi mbalimbali.........
 
Hawa wamanga koko wa Azam tv wana ubinafsi sana. Haiingii akilini tv stations nyingine ziko kwenye recoder yake halafu yeye hataki kutoa za kwake. Nawashauri TBC, ITV,CHANEL TEN, STAR TV, ZBC, EATV wote wajitoe kwenye decoder ya Azam tuone kama ataweza kujitosheleza na ku simama mwenyewe. Huu ni ubinafsi na ukiritimba wa ajabu sana. Kwa mbinu hzi za kitoto nitabaki na king'amuzi changu tu.
 
Mi nacho fahamu huyu mmanga atabana weee mwisho ata achia mwenyewe!
 
Waingie kwenye satellite ili Watanzania (na wengineo) wanaoishi/kufanya kazi nje ya nchi nao waweze kupata hizo habari zao murua.
 
Channel 10 wamegoma kupeleka encoder katika king'amuzi cha TING hivyo haionekani. Je kuna malipo kwa channel husika kuonekana katika King'amuzi fulani??
 
daah nacheki azam tv news hapa namuona legend Charles Hillary na mwanadada anaekuja kwa kasi ya juu Ivona Kamuntu
 
Azam mnakosha sana, sahivi habari kama darasa hivi unapata background ya jambo na tuvitu twingi twingi, yaani mpaka raha na ukitoka hapo michezo ndo kuna mafundi usipime ...Aksante Bakhresa!
 
Hakika Mabadiliko yaliyoandikwa na Gazeti la Mwananchi leo yanadhihirishwa na Ukweli juu ya Habari ambayo nimeishuhudia katika dakika 33 zilizopita sasa kwa habari yao ya Saa zima.

Nimependezwa na Muundo wa Habari na mpangilio wa Habari zao; siataki kuzungumzia weledi wa wasomaji wa leo Bw. Charles Hilal na Bi. Ivona Kamuntu kwa maana ujuzi wao si wa kutilia shaka.

Wameweka interviews break jambo ambalo ni nadra sana katika habari za vituo vingine lakini pia zinaletaa maana ya bridging kwenye habari na kucomplement main story.

Wamaeongeza habari za kusomwa moja kwa moja na msomaji Studio na sio zile za Ripota na mkeka wake mwanzo hadi mwisho wa Habari.

Yanahitajika marekebisho madogo sana kama kujali muda wa kuanza maana leo mmeanza mmechelewa kiasi dakika 4 hivi; inawezekana ni sababu ya mabadiliko ila ni vema kuheshimu muda sana.

Kimsingi ni hatua njema sana kwa ubunifu huu na walau Tanzania tutashuhudia habari ya kwetu wenyewe ambayo itakidhi kiu ya watazamaji wenu.

Licha ya kuwa DTH si vibaya mkafikiria namna bora za kujitangaza na masoko zaidi ili watanzania wengi wanufaike na huduma zenu.

ADIOS

kuifananisha azam tv na bbc ni sawa na kumfananisha christiano ronaldo ( bbc ) wa real madrid na malimi busungu wa yanga ( azam tv ).
 
Azam mnakosha sana, sahivi habari kama darasa hivi unapata background ya jambo na tuvitu twingi twingi, yaani mpaka raha na ukitoka hapo michezo ndo kuna mafundi usipime ...Aksante Bakhresa!
 
Sio mbaya mmejitaidi sana azam mnafanya mapinduzi kila sasa sambazeni reporter dunia zima mwanzo wenu ni mzr sana
 
Hivi mimi niache kutazama BBC nitazame tv local simply kwasababu ya kumtazama mtangazaji flani?
 
Back
Top Bottom