TIQO
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 13,787
- 2,078
Wapenzi wengi wa soka walikuwa wanajua kuwa timu ya Azam ndiyo itakuwa mbadala kwa soka letu la bongo kumbe ni danganya toto, hii inatokana na bosi wa Azam kuingilia kazi ya kocha kwa kumpangia wachezaji wa kutumia na alipo kaidi akaamua kumtupia vilago kocha.
Kwa hiyo bosi akinuna tu kwa vile mchezaji kamkumbatia mchezaji wa Yanga au Simba simtaki na kocha akiona hoja haina mashiko na akamchezesha basi mchezaji pamoja na kocha vibarua vinaota nyasi kama hivi tunashuhudia. Mambo ya kupangiwa wachezaji au mambo ya kuingilia uhuru wa walimu tulikuwa tunasikia yapo Simba na Yanga na tulikuwa tunaamini Azam itakuwa timu bora na ya kisasa kumbe nayo ni timu ya kienyeji kwa mtindo huu Azam haifiki mbali itapotea kama ilivyo potea Kajumlo au African Lyon ngoja tusubiri.Mapema leo mchana, Stewart Hall, kocha Muingereza wa Azam FC jana alifukuzwa katika klabu hiyo kwa kosa la kukaidi maagizo ya Bodi ya Ukurugenzi ya klabu hiyo, kumpanga Mrisho katika mechi ya fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.
Habari ambazo BIN ZUBEIRY ilizipata kutoka ndani ya Azam, zilisema kwamba kikao cha jana cha pamoja baina ya Bodi ya Ukurugenzi ya Azam FC, Mwanasheria wa kampuni na kocha Stewart kimeafiki kuvunja ndoa hiyo na sasa Azam FC itakuwa chini ya kocha kutoka India, Vivek Nagul ambaye alikuwa anafundisha timu ya vijana.