Awamu ya Sita Watu wanajenga, mnyonge mnyongeni Haki yake mpeni

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Kwema Wakuu!

Tukiweka itikadi za Siasa pembeni, udini, na ukabila na tofauti zetu pembeni, ukweli usemwe; Watu wanajenga.

Ingawaje Mimi sina kiwanja hata cha 20*20 na pengine hata Nusu ya Pesa ya kununulia hicho kiwanja lakini ukata huo haunifanyi niwe kipofu kuona wengine wakijenga.

Kuna mmoja nilienda kumuuliza, nini kinaendelea? Ninyi Pesa za ujenzi mnazitolea wapi? Akaniambia, huu ndio muda jombaa, changamka, usipojenga sasa hesabu maumivu.
Yeye hajengi kibanda, anajenga nyumba, namaanisha nyumba hasa.

Mtaa ninaoishi na mitaa ya mbali ninayopitaga ninakuta nyumba zikivunjwa na kufanyiwa maboresho, huku vile viwanja vilivyokuwa wazi vikijengwa.

Mafundi wapo busy Mno. Nina marafiki zangu ambao tulimaliza NAO kidato cha nne, Kwa sasa ni mafundi nyumba, wako busy. Ile kawaida yetu ya kukutana kila Jumamosi na Jumapili kwenda Kula Bata ni zaidi ya Mwaka sasa imekoma. Wako busy Mno.

Rafiki yangu mmoja ambaye kiumri tunalingana kabisa, ananiambiaga wewe kalia kuandikaga Huko mitandaoni, ukija kushtuka unageuka mpangaji wangu.

Sasa Mimi Pesa nitatoa wapi? Hamtaki kunifungulia Pattern, anyway. Hongereni nyote ambao Njia zimewafungukia awamu hii.

Yote juu ya yote, Hongera serikali Kwa kuimwaga Pesa mtaani. Mwenye macho haambiwi tazama.
Najua sio wote Pesa zimewafikia(huenda hata Mimi ni mmoja wenu) lakini mwenzako akipata nawe shukuru😊😊.

Tanzania ni yetu site.
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
 
Kweli watu wanajenga, ila kama ndio kujenga kwa 10% ya DPW ni uhuni mtupu.

Siwezi kabisa kufurahia uwepo wa hayo majengo, ni laana kwa kizazi chetu na kijacho.

Mkuu hawa wanaojenga wengi wao hawana mahusiano na serikali Kabisa.

Kuhusu DP world msimamo wangu ni kuwa kama kuna cha kuboreshwa kiboreshwe ili mkataba usiwe wa kihuni
 
Kwema Wakuu!

Tukiweka itikadi za Siasa pembeni, udini, na ukabila na tofauti zetu pembeni, ukweli usemwe; Watu wanajenga.

Ingawaje Mimi sina kiwanja hata cha 20*20 na pengine hata Nusu ya Pesa ya kununulia hicho kiwanja lakini ukata huo haunifanyi niwe kipofu kuona wengine wakijenga.

Kuna mmoja nilienda kumuuliza, nini kinaendelea? Ninyi Pesa za ujenzi mnazitolea wapi? Akaniambia, huu ndio muda jombaa, changamka, usipojenga sasa hesabu maumivu.
Yeye hajengi kibanda, anajenga nyumba, namaanisha nyumba hasa.

Mtaa ninaoishi na mitaa ya mbali ninayopitaga ninakuta nyumba zikivunjwa na kufanyiwa maboresho, huku vile viwanja vilivyokuwa wazi vikijengwa.

Mafundi wapo busy Mno. Nina marafiki zangu ambao tulimaliza NAO kidato cha nne, Kwa sasa ni mafundi nyumba, wako busy. Ile kawaida yetu ya kukutana kila Jumamosi na Jumapili kwenda Kula Bata ni zaidi ya Mwaka sasa imekoma. Wako busy Mno.

Rafiki yangu mmoja ambaye kiumri tunalingana kabisa, ananiambiaga wewe kalia kuandikaga Huko mitandaoni, ukija kushtuka unageuka mpangaji wangu.

Sasa Mimi Pesa nitatoa wapi? Hamtaki kunifungulia Pattern, anyway. Hongereni nyote ambao Njia zimewafungukia awamu hii.

Yote juu ya yote, Hongera serikali Kwa kuimwaga Pesa mtaani. Mwenye macho haambiwi tazama.
Najua sio wote Pesa zimewafikia(huenda hata Mimi ni mmoja wenu) lakini mwenzako akipata nawe shukuru😊😊.

Tanzania ni yetu site.
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Kwan awamu ipi watu walikua hawajengi na kwann?
 
Mkuu hawa wanaojenga wengi wao hawana mahusiano na serikali Kabisa.

Kuhusu DP world msimamo wangu ni kuwa kama kuna cha kuboreshwa kiboreshwe ili mkataba usiwe wa kihuni
Nilitaka nimjibu huyo,watu wengi ni wajinga sana na wataendelea kuwa na mentality za kipumbavu hivyo hivyo wamekalia siasa uchwara za kina Lisu na Mbowe etc badala ya kuchangamkia fursa.

Kwa mtu ambae Hana biashara kubwa basi njia rahisi ya kupata pesa kama una walau mtaji wa mil.5 basi ingia kwenye Kilimo chochote baada ya mwaka una uhakika wa mil.15 ya kuanza ishu nyingine.

Angalizo usilime kwenye Mikoa isiyo na uhakika wa mvua,Nenda Nyanda za Juu Kusini au Kigoma utapata Ardhi ya kukodi bei nafuu..

Mfano saizi gunia la mchele ni 140,000 Sasa Kwa gunia 30 tuu uko mbali.
 
Watu hawataki kufanya makosa

Kipindi cha Msoga wengine walikula bata wakasahau kujenga alipoingia jiwe walijilaumu

Sasa wamejifunza kipindi cha bimkubwa ni kujenga kwa kwenda mbele mifumo ya siasa na uchumi haieleweki ukipata fursa itumie vizuri
Siasa za ccm hazitabikiki na hawana utaratibu mzuri wa kupata viongozi yaani yeyote ananweza kuwa Kiongozi ndio sababu tunakuwa na ups and downs nyingi sana.

Hata hivyo Kwa Sasa Kila sekta imefunguka
 
Back
Top Bottom