Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,490
- 2,104
Mwanza Kocha msaidizi wa Stand United, Athumani Bilali ametoboa siri kuwa mfumo wa 4-3-2-1 walioutumia ndio uliofanya Simba washindwe kuondoka na pointi tatu kwenye mechi yao ya Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana.
Timu hizo mbili zilitoka sare ya 1-1 kwenye mchezo huo na bao la Simba likipachikwa na Shabani Kisiga wakati bao la Stand United likiwekwa kimiani na mshambuliaji wake, Kheri Mohamed.
Akizungumza na gazeti hili, Bilali alisema kuwa Simba hawakuwashinda kwa kuwa mfumo waliotumia Stand United wa 4-3-2-1, ambao unatumia mabeki wanne, viungo watano, uliwanyima nafasi.
Alisema katika mchezo huo walicheza kwa kupaki basi zaidi na wakitumia mashambulizi ya kushtukiza jambo lililofanya waweze kupata bao la kusawazisha.
"Huu mfumo tunautumia kwenye mechi ngumu, tunakuwa na wachezaji saba wanaokaba sana na tunashambulia kwa kushtukiza, hivyo ndivyo tulivyofanya katika mechi dhidi ya Simba na wakati mwingine tulitumia mfumo wa total football na ndiyo maana uliona hata hao akina Emmanuel Okwi walishindwa kufurukuta uwanjani," alisema Bilali.
Kocha huyo, ambaye ana rekodi ya kutofungwa na Simba kwa timu alizokuwa akifundisha kwenye Ligi Kuu katika miaka yake yote ya kufundisha klabu, alisema mfumo huo wa kukaba zaidi ndiyo uliowamiza wekundu hao.
"Nilijua Simba hawanifungi, sijawahi kupoteza mechi na hao jamaa nikiwa kama kocha, nilikuwa na Toto African kwenye Ligi Kuu niliwafunga mechi zote," alisema kocha Bilali.
Big Up Bilal; asante kwa kuendelea kutuletea raha tangu enzi za Toto Africans ya Mwanza hadi sasa ukiwa na Stand United (Banyawima) ya Shinyanga.